Nimehamishwa kutoka kufundisha Sekondari na kupelekwa primary kisa sielewani na mkuu wa shule

Master sio elimu ya kutisha labda PhD ndio natishika kidogo na Phd iwe niya Ivy League School au Europe na Australia tena best universities zilizobobea kwenye tafiti ndio nitatishika. Marekani elimu ya master hata muhudumu wa hotel na supermarket wanazo tena na bongo siku hizi hata kwa kusoma jioni na kufanyiwa research unapata masters yako.


Lukwafya
 
Nenda kspige kazi mshaambiwa maslahi yenu yanabaki pslepale tatizo walimu wa sekondari mnapenda sifa mbona hamna chochote huko
 
Mimi ni mwalimu mwenye shahada ya elimu leo nmepata barua ya kuhamishiwa shule ya msingi kisa hatuelewani na mkuu wa shule.mkataba wangu unaeleza wazi kua nimeajiriwa kufundisha sekondari,sasa leo nahamishiwa msingi bila makubaliano yeyote nmepewa barua jumatatu nikaripot ..sijapewa hela ya uhamisho je huu ni uungwana,sijapewa mafunzo maalum ya kufundisha msingi..naombeni ushauri wenu.mwenye email ya waziri wa tamisemi naomba niwasiliane nae kwa kweli sijatendewa haki.
Kafundishe were,acha kulialia hivi huo mkataba wako umeusoma vizuri? Kipengele cha mwisho kabisa kinampa mamlaka mkurugenzi kukupangia kazi nyingine yeyote itakapobidi hata kama hakuna sababu muwe mnasoma mikataba yenu vizuri.
 
Hahaha mshahara si unaingia?wasomi muwe makini the ego destroys,mtu km huyu ht ukimwambia tulime mchicha tutapata faida atakuja kusema humu nina degree lkn sijui nikubali biashara kilimo cha mchicha...
 
Sikia ndugu yangu,kwanza usiogope,nenda s/m kafanye kazi!kwani Kule hakuna kazi ya kuumiza kichwa kama sec,ni kuhamisha material tu!!halafu kumbuka kila ashushwaye na mwanadamu,hupandishwa na Mungu!huyo ni binadamu tu,anaekuwazia mabaya,,Bali Mungu huku wa za Mimi na mema Siku zote,kubali,nyenyekea,tii,timiza wajibu!utamuona Mungu akikuinua zaidi!!huna haja ya kuhangaika na hili na lile,,huenda ndiko milango ya mafanikio yko ilipo!kwani si rahisi kufanikiwa ktkt ya rafiki zako wasio kupenda!!jikubali,nenda!na Mungu itakuwa nawe!
 
Wewe ndio una mawazo ya kipumbavu! Kama ww ungekuwa mkuu wa shule ukaambiwa upendekeze mwalimu wa kumtoa Shuleni kwako ungemtoa yupi? Mkorofi(ambapo sifa hii mtoa uzi ameshaonesha viashiria vya kuwa nayo), wa masomo ya Sanaa(ambapo wako wengi) na kilaza(siyo kila mwl anajua kufundisha). Kama hutaangalia sifa hizi ili kumtoa mwalimu aondoke basi ww ndo utakuwa kiongozi wa kipumbavu
Nakuunga mkono kabisa hata yeye
 
Mimi ni mwalimu mwenye shahada ya elimu leo nmepata barua ya kuhamishiwa shule ya msingi kisa hatuelewani na mkuu wa shule.mkataba wangu unaeleza wazi kua nimeajiriwa kufundisha sekondari,sasa leo nahamishiwa msingi bila makubaliano yeyote nmepewa barua jumatatu nikaripot ..sijapewa hela ya uhamisho je huu ni uungwana,sijapewa mafunzo maalum ya kufundisha msingi..naombeni ushauri wenu.mwenye email ya waziri wa tamisemi naomba niwasiliane nae kwa kweli sijatendewa haki.
Hili ndio tatizo la kuchangia demu. Madhara yake ndiyo haya...
 
Inauma sana kufundisha shule za primary mtu kama una degree yako, inauma sana mashule ya primary ya umma ni sehemu za kidhalili sana ni aibu kuu kufundisha shule hizo, kuanzia kimazingira na kimorali ya ufanyi kazi
 
Lengo la serikali ni zuri saana na wakati wote maamuzi huwa ni mazuri saana karibu ktk mambo mengi.

Tatizo ni utekelezaji kwa wale waliokasimiwa shughuli husika. Sifa ya kwanza kwa Mwalimu kuhamishwa ni kwa wale waliojiendeleza toka Shule ya Msingi na kufundisha Sekondari.

Sifa nyinginezo ni za waalimu wa sanaa, na sifa zingine za ndani, lkn hili la kutokuelewana halitakiwi kupewa nafasi. Maana taifa mbele baada ya kazi ndo mengine yafuate.

Tukiishi kwa kukomoana hatufiki popote hali hii IKEMEWE ni pepo.
Samahani mkuu kama hao was msingi hakuna na ikama hairuhusu afanyeje
 
Master sio elimu ya kutisha labda PhD ndio natishika kidogo na Phd iwe niya Ivy League School au Europe na Australia tena best universities zilizobobea kwenye tafiti ndio nitatishika. Marekani elimu ya master hata muhudumu wa hotel na supermarket wanazo tena na bongo siku hizi hata kwa kusoma jioni na kufanyiwa research unapata masters yako.Na kwa ufupi nchi zilizoendelea walimu wenye masters wanafundisha mpaka primary ni nchi za ulimwengu wa tatu ndio tunampa mtu mwenye certificate alifeli kidato cha nne kucheza na future za watoto wetu.Kwa wenzetu kuwa mwalimu, nesi au Daktari sio mchezo mchezo unaiva kweli kweli ndio upewe leseni ya kuwa mwalimu dokta au nesi, kwa sababu wanangalia future ya kizazi chao.
Point! Kula tano mkuu!
 
Muongo,,,,ila hata hivyo mkuu wa shule yuko sasa nitaachaje kumtoa mtu ambaye sina maelewana napendekeza uondoke tuu
sio uongo ni sahihi, unapigiwa simu unaambiwa shule yako Luna walimu kadhaa wa somo fulan na fulan pendekeza majina ya unaotaka wapungue
 
Samahani mkuu kama hao was msingi hakuna na ikama hairuhusu afanyeje
Ikama inahusisha Mkoa mzima shule za msingi na sekondari.

Hakuna cha kufanya zaidi ya kuchapa kazi na kuomba semina elekezi, uhamisho huu ili ulete tija mafunzo kazini ni lazima.
 
sasa atakuachaje wakati mna bifu,,,,
hapo Mimi sijazungumzia sababu ya kupendekezwa MTU kwa sababu fulan laaaa! nimethibitisha kuwa wakuu wanahusika kwa upande mwingine na sio km alivyokanusha niliemquoet akikanusha kuwa hawahusiki kabisa, kukupendekeza au kutokukupendekeza inategemeana na mahsiano yenu,umuhimu wako ktk kaz no.
 
Nasema shuleni kwako walimu wa idara ya lugha wamezidi afanyeje huyo mkuu was shule
 
Back
Top Bottom