Nimefikia muda wa kuoa, nakosa mke mwenye sifa zifuatazo

ndege JOHN

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
19,568
44,786
Habarini,niende moja kwa moja kwenye mada. Mimi Ni kijana nimefikia umri wa kuoa na hali zangu zote zinaniruhusu kuoa lakini mpaka sasa sijawahi kuwa na msichana ambaye nimemuweka level za uchumba na kila nikimtafuta nakosa wote najikuta hatuendani nao.

Pia kwa kuwa nilichelewa kujihusisha na mahusiano sikuwahi kupata mwanamke ninayemtazamia ambaye nilikuwa namuwaza kwa kipindi kirefu aje kuwa mke wangu wa ndoa. Wote ninaowapata tunazinguana nao kwa sababu ya sababu fulani fulani hivyo tunadumu kwa muda mfupi kwa sababu ya baadhi ya vitabia ambavyo sipendi my future wife awe navyo

1. Sipatani na mwanamke muongeaji sana. Bahati mbaya wanawake nilioweza kuwabahatisha wote kuwa wapenzi wangu sikuweza kufikiria kuwaoa kwa sababu wana kidomodomo sana, nikaachana nao kimya kimya. Mtu anaongea kama chiriku, anajifanya much know akiamua hakusikilizi. Hii sio sifa ya mwanamke ninayemuhitaji forever.

2. Sipatani na wanawake wanaonuna nuna hovyo. Yaani mtu akiamua anakaa kimya week nzima hamuongei kitu mpo kimya, mtu hakwambii shida zake. Nikaona hawa miyeyusho watakuja kunieleta uboya mie kutwa niwe nabembeleza.nikaona mapenzi ya hivyo sio kweli. Awe angalau ana-create mazingira ya yeye kuwa free kukueleza mtazamo wake.

3. Wanawake wasiojua kiasi; hapa nikawatumbua wengi. Kuna wanawake nilikuwa nawapata wenyewe pigo zao kujiremba tu muda wote wanataka waonekane wazuri. Mimi sipendi mwanamke wa hivyo, nataka mwanamke anayejua maana ya kiasi na anayeweza kusimamia uasili wake. Nikaachana na wachumba kibao.

4. Wengine nikagundua hawawapendi ndugu zangu. Yaani mwanamke mnakuwa naye kwenye mahusiano hajawahi hata kumuulizia mama yangu anaendeleaje? Sasa hayo ni mapenzi ya kweli au uasherati tu? Nikaachana na nyota hizo.

Mpaka sasa bado mwanamke wa kumkabidhi moyo wangu, kumuoa na kuzaa naye sijaona. Kiukweli wananitisha wanawake wa bongo natamani hata nibadilishe mwanamke nikatafute mwanamke wa kizungu au nchi tofauti na Tanzania.

Walio vifungoni tayari wengi wanatamani kujuta, wao watanishauri nisiendelee kuchagua kwamba sitapata mwenye sifa hizo lakini mimi nina uhakika nitampata tu wa kwangu mwenye sifa zote kisha tuwe wawili maana ni bora kuwa wawili mmoja akianguka mwenzake atamnyanyua.
 
Bado mdogo sana kuanza mahusiano ya ndoa kwa miaka hii ya sasa......ingekuwa zamani sawa....ila kwa miaka hii ili uweze tulia na kupata mtu mwenye afadhali inabidi uwe na at least 29 kwenda juu na hapo utoke na msichana ambaye maisha hayaja mchakachua na ambaye at least utakuwa umemgap kama miaka 5 au zaidi isizidi 8!

Binti wa namna hii ni rahisi kuishi nae kwa akili na kumuelekeza vizuri.
 
Bado mdogo sana kuanza mahusiano ya ndoa kwa miaka hii ya sasa......ingekuwa zamani sawa....ila kwa miaka hii ili uweze tulia na kupata mtu mwenye afadhali inabidi uwe na at least 29 kwenda juu na hapo utoke na msichana ambaye maisha hayaja mchakachua na ambaye at least utakuwa umemgap kama miaka 5 au zaidi isizidi 8!

Binti wa namna hii ni rahisi kuishi nae kwa akili na kumuelekeza vizuri.
Nashukuru kwa ushauri mzur wenye kunufaisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom