Nimefichua siri

Nimefichua siri

Kwa wanaojua njia zaidi ya kutunza siri nahitaji mawazo ili niweze kuwa mtunza siri mzuri..:embarrassed:

Chukua kijembe, toka nje ya nyumba yako, chimba kijishimo kidogo, taja siri zako zote humo ndani ya kishimo, halafu fukia...
 
Kwani huna mzazi wako? mimi msiri wangu mkubwa ni Mamangu,na sio siri tuu hata jambo langu lolote liwe siri au la dhahiri sipendi kuongea,akinisema yeye kwa mtu ujue tena hapo ndio nimesha maliza kwenye maisha ntakua sina msiri tena....
 
Huo ni unafiki wako na kiherehere chako cha kushindwa kutunza mambo yako.
Tuache ujinga jamani humu ndani hivi kuna yeyote amewahi kuckia kama kuna njia za kutunia kutunza Sirius? Hii ni tabia ya mtu japo c si yako tu hata wenzako huwa unayafanya vivyo hivyo.
 
Huo ni unafiki wako na kiherehere chako cha kushindwa kutunza mambo yako.
Tuache ujinga jamani humu ndani hivi kuna yeyote amewahi kuckia kama kuna njia za kutunia kutunza Sirius? Hii ni tabia ya mtu japo si yako tu hata ya wenzako huwa unayafanya vivyo hivyo.
 
kama wew ni mwanaume uko na kazi kubwa kubadilika upesi
 
Siri nayo ina muda wa kuwa valid kama siri. Muda huo ukipita inakuwa siyo valid tena so inakuwa haina madhara. Kwa kipindi kile ipo valid huwezi isema hata iwaje. So ukiona kitu ulichosema ni siri sana halafu ukasema ujue unyeti wake umeisha, ni kama chumvi isiyo na ladha.
 
Habari zenu wana jamii, poleni na majukumu.

Kuna kitu kinanitatiza ni bora mnisaidie mawazo niwe na amani. Binafsi nina kanuni zangu flani za maisha, na kuna baadhi ya mambo ambayo ni binafsi sana napenda yawe ni siri ya moyo.

Sasa kilichotokea ni kwamba nilijikuta nikimwambia mtu wangu mmoja wa karibu siri yangu ambayo hua sipendelei baadhi ya watu wajue. Nilipomueleza niliumia sana nikasema ni mistake imetokea nitajitahidi nizibe mdomo.

Sasa hii mara ya pili nimejikuta nikimuelezea mtu mwingine siri nyingine tena sio ile ya kwanza, nimeumia sana lakini ndo imeshatokea sasa sijui nifanyaje.

Maana ni mambo binafsi sana sipati picha akiamua kushea na watu wengine japo sio mabaya lakini ndo hivo sipendi yafahamike. Siri nimeshindwa kutunza sasa najihisi vibaya.

Kwa wanaojua njia zaidi ya kutunza siri nahitaji mawazo ili niweze kuwa mtunza siri mzuri..:embarrassed:

Tuambie na sisi ili isiwe siri tena!!!! na hapo hutaumia kamwe!!!
 
Pole, inategemeana Kuna wakati mwingine vitu vingine unaweza kufikiri kuwa ni siri kumbe unahitaji ku share,Kuna Tofauti ya Neno siri kati ya mtu na mtu, Kuna kitu unaweza kuona kuwa ni siri kwako lakini kwa mwinginee sio siri,Lakini lazima uwe na mtu ambaye anaweza kubeba mambo yako na uwe na uhakika naye!. Mfano mimi Kuna vitu nashare na Mke wangu tu, vingine rafiki tu. Ndugu? Kwa ndugu ni vitu vya kindugu mara nyingi hata nikigombana na mke wangu sitaki ndugu wajue.

wow! asante, nitajitahidi kuanagalia na mtu wa kushare nae na ni aina gani ya issue. asante kwa ushauri na kushare experience yako. Nimepata moyo
 
Hongera kwa kutua mzigo mzito uliouweka moyoni kwa siku nyingi. Nadhani sasa umwepesiiiiiii.....
 
tuwekee hizo siri hapa jamvini tukusaidie kuzintunza .........

Grand PA
 
Back
Top Bottom