mkulimamwema
Senior Member
- Apr 14, 2011
- 153
- 18
Mimi ni mwanaume wa miaka 26,nimekuwa kwenye uchumba kwa muda wa mwaka sasa.Niliamua kumpenda huyu bibie pamoja na kuwahi kuumizwa na bwana mwingine kiasi cha kumharibia maisha hilo sikulijali.Siku zote sikupenda akumbuke yaliyompata na nilijitahidi kuwa karibu kadri nilivyoweza,maneno matamu na kila apendalo mwanamke nilimpa.Mimi nilichofanya ni kuwa mwaminifu sana na kuwa mkweli sana.Yeye hudai hawezi kuongea kiasi kwamba nabaki naongea kwenye simu muda mrefu nikimbembeleza angalau aniambie maneno ya faraja hubaki kusema hana cha kusema,nilivumilia sana.Hivi karibuni nilisafiri toka dar hadi mwanza kumwona yeye na nilifikia hotelini kwa kuwa sina ndugu kule.Kuna mambo alinidanganya nilimhoji sana ila hakuonyesha kujutia hata kuniomba msamaha,jana usiku namtakia usiku mwema alipokea simu na kunyamaza kimya,niliongea muda mrefu hata hakusema kitu,nimejitahidi kumjali mno na kweli nampenda sana na akinisikiliza napenda sana awe mke wangu maana sitaki kuwa na mwanamke mwingine,ingawa inaniuma sasa nataka kuachia ngazi,ndugu wana familia kaka zangu shemeji yenu anataka kutoka na nyie dada zangu wa hapa JF wifi yenu anasumbua nifanye nini?