Nimechelewa dakika 5 kwenye interview

Mie nakuombea uipate hii kazi, fundisho katika siku za usoni kama huifahamu ofisi itakayofanyika interview basi ni vizuri ukaenda kuitafuta siku mbili/tatu kabla ya interview ili kuepuka kuchelewa. Kila la heri.

kweli nimepata funzo.sitafanya hii mistake tena..
 

ee bana ee..hii yako noma hata afadhali mimi.najua how it feels.thank mkubwa for consoling me...
 

kingasti i should have thought of that.I always observe time.but this particular day was just screwed up..
 
Usijali kuwa optimistic na utaupata. Anza kumwambia Mungu hata kama waliona kikwazo but kila mmoja wa panel aone ni wewe tu. Amini umeshapata. Let us cross our fingers.
 
Ukikosa usije ukajipa moyo kwamba ni kwa sababu ya kuchelewa..
 
Teh me yalinikuta nilienda wrong place ingawa ni kampuni moja,.. uzuri HR wa pale ilibidi ampigie hr husika aliyeenda kuinterview kuwa kuna watu wawili wamekuja ofisi yao nyingine, tukaelekezwa mahali husika good thing nilikuta zamu yangu bado maana HR alisema walisahau kuniambia muda siku wamenipigia simu hali iliyopelekea nikaenda sehemu tofauti, yule mwenzangu kwenye simu aliambiwa asubuhi akakuta zamu ake imepitaa though walimruhusu ila hawakumpa kazi.
 
pole sana ila usikate tamaa, ila nitakulaumu sana kama simu unayotumia ni smartphone au simu yoyote ambayo ina google map alafu ukapoteza muda mwingi kuzunguka au kuuliza watu wakati ramani unatembea nayo... ulimwengu wa sasa hata si wakuulizauliza hasa kwa sehemu zinazofahamika wakati location zipo kwa simu.
 
Kumbe ndio wewe niliokuelekeza siku ile!
 
Duh mkuu nakumbuka na mimi ilinikuta kuna shirika la wazungu flani waliniita kwenye usaili nikaamka mapema sana na nilitakiwa saa 3:00 asbh ile nataka kutoka mvua kubwa ikaanza nikapiga simu za madereva tax wote holaaaaa nikasogea kituo cha daladala nikapoteza muda mpaka napata bajaji ni saa 2:50 nafika eneo la tukio nimechelewa dakika 25 na jina langu limeitwa nikaomba nafasi kwa upole sana nikapewa,amini leo hii nafanya kazi na hao jamaa na kwenye usaili tulikua 43 nikapenya mwenyewe naamini utafanikiwa mkuu kama ulitulia kwenye kujibu maswali yao.
 
Mkuu ni kweli unachosema Muumba ndy kila kitu,ninakumbuka mm sikumaliza maswali ya interview ya practical na

nilimsumbua sana yule jamaa aliyekuwa anasimamia kwa kumuuliza maswali na tatizo lilikuwa mm sikuwa makini sana

vitu vinagoma halafu najifanya mtaalam namwambia setting zenu mmekosea mbona mambo yanagoma jamaa akija

anakuta kumbe nimekosea herufi moja hadi akaniambia kwa ukali "Hii mara ya mwisho ukinisumbua nakutoa" na

practical alikuwa anasahihisha yeye palepale lakini mwisho wa siku nikapata kazi,ningemaliza yale maswali ningetamba

ni ujanja wangu maana maswali yote yalikuwa yanatembea.

 
kama wamekupenda wanakuchukua no worries pray hard ila sasa next time, unatafura ofice zilipo kabla ya siku ya intaview, yaan hy siku ya intavyuu ni kuelekea tu mkuu..ila sio ishu, ka wamekuoenda utapata...
 
USIPANIKI kijana,
nakushauri kazi ya kutafuta mahali ofisi iliko ni siku moja au mbili kabla ya siku ya usaili.Siku ya usaili unatakiwa kufika pale dk5 kabla ili uwe na muda wa kuvuta pumzi
 
Na mimi jinsi nisivyo muongeaji, huwa nawauliza google tu, ila sasa kuisoma hiyo ramani ni suala jingine kabisaa!
 
Mambo za kazi hizi! Majanki wananyanyasika sana!
 
Na mimi jinsi nisivyo muongeaji, huwa nawauliza google tu, ila sasa kuisoma hiyo ramani ni suala jingine kabisaa!

Sio issue sana kama sehemu inajulikana kwenye ramani ukishapata njia unaweka my location mshale unakuonyesha unakoelekea ukitembea nao una move.
 
Sio issue sana kama sehemu inajulikana kwenye ramani ukishapata njia unaweka my location mshale unakuonyesha unakoelekea ukitembea nao una move.

wow, nilikuwa sijajua hili mkuu, asante sana!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…