Nimechanganyikiwa jamani, naombeni ushauri

Nimechanganyikiwa jamani, naombeni ushauri

Arrabella

Member
Joined
May 25, 2014
Posts
15
Reaction score
3
Nilikuwa kwenye mahusiano kwa miaka 2, kweli nampenda sana japo yeye siku zote alikuwa ananiambia kuwa ananiona simpendi . Sasa hayuko tayari tena na mimi na zaidi nina ujauzito hata sijui nifanyaje ?

Nampenda sana na naumia mwenzenu.
 
kaa chini uongee na mwenzako vizuri na umueleze hali halisi naamini mtaelewana 2.
 
Usichanganyikiwe binti,kaa chini zungumza nae mweleze unavyojisikia na namna unavyohitaji mtoto apate malezi yenu,akigoma ujue seriously hakuhitaji..
Akikataa uje uniambie nikunong'oneze kitu
 
Pole sana Arrabella,,hongera kwa kuwa mjamzito!Wengi sana wanatafuta hata mimba za kusingizia bila mafanikio!

Kuna mabadiliko huwa yanajitokeza katika kipindi cha ujauzito especially mimba inapokuwa changa,kuna wengine huwa wanafikia kuwafukuza waume zao nyumbani,hii ni hali ya kawaida Arrabella!

Mtafute rafike yake,au mtu mzima aongee naye ampe elimu ya ujauzito,kuwa hayo yote yanayotokea kipindi hiki hata umtukane matusi au umtamkie kabisa kuwa humtaki na umpendi,sio wewe ni hali uliyonayo ya ujauzito,akuvumilie na hasa azidi kujitahidi kuongeza upendo katika kipindi hiki!

Nakutakia malezi mema ya hicho kiumbe cha Mwenyezi Mungu
 
Last edited by a moderator:
Pole sana,lakini kwanini ulijisahau sana hivyo mpaka unapata mimba? ulihisi ndio njia yakumuonyesha kama unampenda sana au? chakufanya kaanae chini umueleze hali halisi na ukubali uamuzi wake kama atasema hakutaki tena sawa ila mimba lea mwanao zaa uanze maisha mapya... kumbuka usilazimishe PENZI .... ..........hata kama unampenda piga moyo konde wewe ni mwanamke usiuendekeze moyo sema nao utakusikia... kila la kheir.........................
 
Oh maama!
Mh..walai nimekosa cha kusema, naomba tu nikupe POLE!

Too sad you never saw the signs early enough..ama uliziona ukazipuuzia! Unanikumbusha thread ya NANDERA.
 
Last edited by a moderator:
nimejaribu kuongea nae sana na nakubali kuwa ni kosa nimefanya

Mimba ina miezi mingap?tatizo kubwa sana wadada mnafanya kutega mimba kwa kudhani ndio penzi litapatikana...kabla ya kubeba mimba lazima uongee na mwenzio la sivyo inakula kwako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom