Nimeamua kuachana na CHADEMA

Nimeamua kuachana na CHADEMA

Eboo nimekwambia sina chama wala sikuwa na chama,nilipenda na kukubali walichokuwa wakipigania CHADEMA.
Hapo kwenye msisitizo - kwani sasa walichokuwa wanapigania kimebadilika?
 
Kuna msemo heri lawama kuliko fedhea... Mbowe alishasoma fedhea inayokuja, imagine unaingia mtaani na watu kumi wanaokuunga mkono wengine wapo pembeni wanashangaa na kuchukua picha za kurusha insta na fb... Kiukweli Chadema ya leo sio Chadema ya Dr Slaa.. Kuna siku mtakuja kumkumbuka Slaa japo leo mnamtusi matusi yote ila kile kichwa kilishafanya calculations na kuona yote haya wakati nyie mnawaza kura za ulipo tupo.
wamekuelewa mkuu...
 
Hapo kwenye msisitizo - kwani sasa walichokuwa wanapigania kimebadilika?

Walitakiwa kukipigania hata kama ni kumwaga damu hawakutakwa kurejea nyuma.
 
Eboo nimekwambia sina chama wala sikuwa na chama,nilipenda na kukubali walichokuwa wakipigania CHADEMA.
Umeanzia kuisapoti kwenye UKUTA? Au ulikuwa mwanaCHADEMA tangu zamani?
 
Umehama chadema kama katika soka ulivyotuhama arsenal??

Hakuna namna ukiona jambo linakukera unasepa watu wanawaacha wanawake tena kwa viapo itakujakuwa chama !.
 
Walitakiwa kukipigania hata kama ni kumwaga damu hawakutakwa kurejea nyuma.
Sababu walizotoa kuahirisha nadhani zina mashiko lakini ishu ya mustakabali wa wale walio mahabusu ndio wanatakiwa washikie bango waachiwe.!
 
Hakuna namna ukiona jambo linakukera unasepa watu wanawaacha wanawake tena kwa viapo itakujakuwa chama !.
Kadi yao usisahau kurudisha.....oooh sorry umesema hukuwa mwanachama wao Bali uliwaunga tu mkono.!
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Leo tarehe 31/08/2016 nimeamua kuachana na CHADEMA na kujishuhulisha na masuala ya michezo tu hasa mpira wa miguu.

Nilikuwa shabiki wa siasa bila kuunga mkono chama chochote cha siasa,kama mtanzania hata kama si mpenzi wa vyama bado nilikuwa na wajibu wa kuunga mkono jambo ninaloliona lina manufaaa kwa taifa.Tamko la viongozi wa CHADEMA la kututaka tuandamane nilikubaliana nalo kwa asilimia 100%, kwasababu madhumuni yake yalikuwa kupigania utawala wa sheria,kulinda uhuru wa kupasha habari,uhuru wa kusikia maoni kutoka vyama vyote si chama kimoja tu uku vingine vikizuiliwa hii ni hatari sana.

Viongozi wa CHADEMA walitangaza rasmi tarehe 01/09/2016 yangefanyika maandamano na mikutano nchi nzima.Makamanda walitumwa sehemu mbali mbali za jamhuri ya Tanganyika (Zanzibar ni nchi nyingine hainihusu) Ngongo na wapigania demokrasia hawakuhitaji kuhamasishwa na makamanda toka makao makuu tayari tulishafanya maandalizi ya kutosha ikiwa ni pamoja na kufanya mazoezi ya kukimbia kilometa kumi kila siku asubuhi ili kuuweka mwili katika hali ya utayari kukabilia na nginja nginja ya Polisi.

Tulishanunua mafuta (sina uhakika kama yangesaidia) kwaajili ya kuilinda ngozi dhidi ya maji ya washawasha,tulisha nunua miwani isiyopitisha hewa kwaajili ya kujilinda na mabomu ya machozi (sina hakika kama zingesaidia) kwa ujumla maandali yalikuwa yamefikia 95% ghafla bini vuuu Kamanda anahairisha maandamano ?

Hii haikubaliki nasema haikubaliki kabisaa lazima viongozi watambue wajibu wao katika kila matamko yao si unatamka leo hivi kesho unatenda vingine.

Mwezi mmoa aliotoa kamanda wetu Mbowe hauna maana makamanda wameswekwa rumanda, wanachama na wapenzi wamejiandaa vya kutosha hatuna uhakika na hizo siku 30.
Kina Mbowe wenyewe wanagombea kila uchaguzi kwa sababu wanaujua utamu wa maisha mazuri. Nani haogopi kufa?
 
Kamanda Ngongo hasira hasara.

Chama cha siasa ni mbinu. UKUTA umefanikiwa kwa 80%. Wote tumeona reaction ya serikali na vyombo vya dola; hii inaonyesha nguvu ya CHADEMA Tanzania. Hata hivyo operesheni UKUTA haijafutwa bali imesogezwa mbele kwa ushauri wa viongozi wa dini.
Aluta continua!
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Leo tarehe 31/08/2016 nimeamua kuachana na CHADEMA na kujishuhulisha na masuala ya michezo tu hasa mpira wa miguu.

Nilikuwa shabiki wa siasa bila kuunga mkono chama chochote cha siasa,kama mtanzania hata kama si mpenzi wa vyama bado nilikuwa na wajibu wa kuunga mkono jambo ninaloliona lina manufaaa kwa taifa.Tamko la viongozi wa CHADEMA la kututaka tuandamane nilikubaliana nalo kwa asilimia 100%, kwasababu madhumuni yake yalikuwa kupigania utawala wa sheria,kulinda uhuru wa kupasha habari,uhuru wa kusikia maoni kutoka vyama vyote si chama kimoja tu uku vingine vikizuiliwa hii ni hatari sana.

Viongozi wa CHADEMA walitangaza rasmi tarehe 01/09/2016 yangefanyika maandamano na mikutano nchi nzima.Makamanda walitumwa sehemu mbali mbali za jamhuri ya Tanganyika (Zanzibar ni nchi nyingine hainihusu) Ngongo na wapigania demokrasia hawakuhitaji kuhamasishwa na makamanda toka makao makuu tayari tulishafanya maandalizi ya kutosha ikiwa ni pamoja na kufanya mazoezi ya kukimbia kilometa kumi kila siku asubuhi ili kuuweka mwili katika hali ya utayari kukabilia na nginja nginja ya Polisi.

Tulishanunua mafuta (sina uhakika kama yangesaidia) kwaajili ya kuilinda ngozi dhidi ya maji ya washawasha,tulisha nunua miwani isiyopitisha hewa kwaajili ya kujilinda na mabomu ya machozi (sina hakika kama zingesaidia) kwa ujumla maandali yalikuwa yamefikia 95% ghafla bini vuuu Kamanda anahairisha maandamano ?

Hii haikubaliki nasema haikubaliki kabisaa lazima viongozi watambue wajibu wao katika kila matamko yao si unatamka leo hivi kesho unatenda vingine.

Mwezi mmoa aliotoa kamanda wetu Mbowe hauna maana makamanda wameswekwa rumanda, wanachama na wapenzi wamejiandaa vya kutosha hatuna uhakika na hizo siku 30.
Kama unaona CHADEMA wamefanya kosa kuhahiirisha maandamano na Kama unaona yanafaida hakuna asiyependa faida wala CHADEMA hawajakukata miguu tarehe 1 ikifika komaa beba unachoona kinafaa ingia barabarani andamana mkuu.
 
Eboo nimekwambia sina chama wala sikuwa na chama,nilipenda na kukubali walichokuwa wakipigania CHADEMA.
chama chetu sikivu kimewasikia viongozi wetu wa dini natunawaheshimu si kama yule anaye omba kuombewa lakini ni mkaidi akiitwa na viongozi hao
 
Kaboa kweli lakin mi nampenda Tu Lowassa
 
Umeanzia kuisapoti kwenye UKUTA? Au ulikuwa mwanaCHADEMA tangu zamani?

Nimekwambia sina chama ila naunga mkono mambo ya maana yawe yamefanywa na chama chochote.Mfano niliunga mkono wazo la serekali ya CCM ya kufufua shirika letu la ndege,majuzi wameleta ndege mpya si mtumba toka Canada.Naunga mkono uhakiki wa wafanyakazi hewa,naunga mkono suala la kumaliza uhaba wa madawati,naunga mkono ujenzi wa reli Dar to Rwanda & Burundi lakini napinga ujenzi wa uwanja wa ndege CHATO,napinga matamshi ya Makonda wakati wa kuaga miili ya askari waliouwawa (ningekuwa mimi ni Rais ningetengua uteuzi wake mara moja)Nalaani matumizi mabovu ya jeshi la polisi hasa katika masuala ya kisiasa upooo ndugu yangu.
 
CDM wamefaniliwa sawa kwa sababu lengo la maandamano ni kutoa attention kwa watu ili wajue nini kitakwenda zungumzwa mwisho wa hayo maandamano sasa kwamuda wote huo cavarage waliyoipata ni zaidi ya hayo maandamano kwa kuwa walichotaka kukisema kimesemwa na kila kada kuanzia kijiji mpaka taifa kuna makundi yamefanya maandalizi ya vitendo hadharani namna ya kuzuia sasa ki kawaida ukiona unajiandaa sana maana yake unajua umahiri wa mpinzani wako
 
Huyu Anakwenda Kule Kwa Ng'Ombe Waliokatika Mikia Machungani Unadhani
Chadema Ni Chama Kidogo
Huko Chadema Kuna Viongozi Wenye Mbinu
 
Back
Top Bottom