Drone Camera
JF-Expert Member
- Jul 25, 2017
- 14,157
- 14,120
Ni kuhusu OpenAI. Karibuni hapa imetangaza kwamba developers wa China hawataweza kutumia API zao kutengeneza products.
Ikumbukwe kwamba nchi hizi mbili zipo kwenye vita ya kiuchumi na kiteknolojia. Na katika sekta ya teknolojia, hakuna ubishi kwamba akili mnamba ndo iliyoshika hatamu kwa sasa. Ila ni wazi kaka mkubwa anataka kushika portion kubwa ya keki hii kwa muda mrefu.
Mtandao wa kurank hizi LLMs (The tech powering ChatGPT) uitwao Hugging Face umeonyesha LLMs kutoka China umezishinda baadhi ya LLMs za kampuni kubwa za Marekani. Mfano, Qwen2 ya Alibaba imeishinda hata Llama 3 ya Meta.
China ndo taifa linaloweza kukabiliana na Marekani sekta hii. Na ni kama kaka mkubwa anaogopa kasi ya bwana mdogo hapa.
Mimi najiuliza, kama lengo la Marekani ni kulinda taarifa za raia wake dhidi ya washindani wake (kama ilivyokuwa ishu ya TikTok) basi ingependezwa na matumizi ya OpenAI China maana hii kampuni nasikia hata lengo lake la kuifanya gtp-4 iwe free ni ili waweze kukusanya data zaidi kisha wazitumie kutrain na kuzifanya GPTs zijazo ziwe more powerful. Sasa nashangaa inakuaje wanaacha kutumia hii chance ya kukusanya data za wachina.
Kama lengo ni kuifanya China iwe nyuma katika sekta hii, basi naona ni kama wamechelewa maana imeshapiga hatua sana uwanja huu kiasi cha kuwapa challenge halisi.
Siichukii Marekani wala si shabiki wa haya mabavu wanayooneshana ila penye ukweli ni vema kutia neno.
Hii pia ni alarm kwa nchi zingine kujipanga katika teknolojia hii ili kuepuka mambo haya siku za mbeleni kama source ilivyoshauri.
Source: The Batch, deeplearning.ai
Full Article: OpenAI Blocks China, Tests for Human-Level Models, Music Industry Sues AI Startups, Model Merging Evolves
Ikumbukwe kwamba nchi hizi mbili zipo kwenye vita ya kiuchumi na kiteknolojia. Na katika sekta ya teknolojia, hakuna ubishi kwamba akili mnamba ndo iliyoshika hatamu kwa sasa. Ila ni wazi kaka mkubwa anataka kushika portion kubwa ya keki hii kwa muda mrefu.
Mtandao wa kurank hizi LLMs (The tech powering ChatGPT) uitwao Hugging Face umeonyesha LLMs kutoka China umezishinda baadhi ya LLMs za kampuni kubwa za Marekani. Mfano, Qwen2 ya Alibaba imeishinda hata Llama 3 ya Meta.
China ndo taifa linaloweza kukabiliana na Marekani sekta hii. Na ni kama kaka mkubwa anaogopa kasi ya bwana mdogo hapa.
Mimi najiuliza, kama lengo la Marekani ni kulinda taarifa za raia wake dhidi ya washindani wake (kama ilivyokuwa ishu ya TikTok) basi ingependezwa na matumizi ya OpenAI China maana hii kampuni nasikia hata lengo lake la kuifanya gtp-4 iwe free ni ili waweze kukusanya data zaidi kisha wazitumie kutrain na kuzifanya GPTs zijazo ziwe more powerful. Sasa nashangaa inakuaje wanaacha kutumia hii chance ya kukusanya data za wachina.
Kama lengo ni kuifanya China iwe nyuma katika sekta hii, basi naona ni kama wamechelewa maana imeshapiga hatua sana uwanja huu kiasi cha kuwapa challenge halisi.
Siichukii Marekani wala si shabiki wa haya mabavu wanayooneshana ila penye ukweli ni vema kutia neno.
Hii pia ni alarm kwa nchi zingine kujipanga katika teknolojia hii ili kuepuka mambo haya siku za mbeleni kama source ilivyoshauri.
Source: The Batch, deeplearning.ai
Full Article: OpenAI Blocks China, Tests for Human-Level Models, Music Industry Sues AI Startups, Model Merging Evolves