Mahatma Gandhi
Member
- Jan 16, 2012
- 25
- 15
Mambo vipi Wanajamii Forum???Naomba musome hapa kwa makini kisha tujadili katika hili.Juzi nilikuwa nasoma ripoti ya UNDP ya mwaka 2011 kuhusu hali ya maendeleo katika nchi 187 wanachama wa UN.Ripoti hiyo imezigawa nchi hizo katika makundi makuu manne;yaani nchi zenye maendeleo ya juu sana,ya kati,chini na maskini sana.Nchi za Norway,Australia,Uholanzi,Marekani,New Zealand,Canada,Ireland,Liechtenstein,Ujeruman na Uswisi ziko katika kumi bora kimaendeleo.Barani Afrika nako Ushelisheli ni ya 52 na ni ya kwanza katika Afrika ikifuatiwa na Libya(ya 64 ingawa kulitokea mapinduzi mwaka jana) na ya tatu ni Mauritius(ya 77).Tanzania yenye madini kibao (hususani Tanzanite),mito,maziwa,bahari na misitu inashika nafasi ya 152 na ni kati ya nchi zilizo katika kundi maskini sana pamoja na DRC yenye Diamond,misitu(kwa ajili ya mbao),mto Congo,ziwa kivu n.k inashika nafasi ya mwisho (187).Ebu waungwana sisi kama wadau wakubwa wa maendeleo ya nchi yetu na bara la Afrika kwa ujumla tufanye tafakuri.Hivi hizi rasilimali (nilizotaja hapo juu) zipo kwa ajiri ya kutufanya tuwe maskini wa kutupwa kila kukicha?,au Mungu alitupa kama laana bila sisi kujua(lakini nisingependa kumkufuru Mungu wangu)?,na je hatuwezi kuzitumia kujiletea utajiri kama Norway na Australia?? Hivi katika hili,tatizo ni nini????