Nimeamini CCM inang'ooka! Sasa asiyeamini kuwa CCM inang'ooka Oktoba mwaka huu, akubali kwa uchungu!

Not_Yet_Uhuru

JF-Expert Member
Oct 11, 2010
1,304
431
Wadau;

Hii Sio siri tena! Tumekuwa tukilisema hili na kurudia kuwa, ili wanaoiamini sana CCM ya sasa wajirudi na kuwa upande wa umma, wawe wazalendo. Na kuwa, watanzania wa sasa sio wale ambao walikuwa 'wanaleweshwa' na nyimbo za CCM, na kulewa sifa za kutungwa, kupewa hongo za pombe, khanga, t-sheti, kofia, pilau na kubebwa ktk magari ya matarumbeta na nyimbo za TOT na kuambulia kushiba kwa siku mbili au tatu huku wakiuza Kura zao kwa 'ujira wa mlo' au 'uniform' na kuteseka kwa miongo na miongo ya miaka!

Kauli hizi nzito, zinatoka kwa baadhi tu ya watu 'nguli' ambao ndio 'wenye CCM' na zinawahakikishia washabiki wanaoiamini sana CCM ya kuwa itabaki madarakani, 'wajiandae' maana CCM haielekei kuhimili mabadiliko, na Kimbunga cha hasira ya Umma, na kuvuka salama ktk Kura Oktoba 2015!

  • Jaji Joseph Warioba na Joseph Butiku kwa nyakati tofauti, walishaitahadharisha CCM na uongozi wake kuwa kwa walipoifikisha CCM na taifa kwa sasa, hii sio CCM waliyoijua ya wakulima na wafanyakazi, wananchi wanaweza kuiondoa madarakani. Baadhi ya Viongozi wa sasa wa CCM wakawabeza na kusema wamezeeka vibaya.


  • Mh. Cleopa David Msuya (waziri mkuu mstaafu), amesema mara kadhaa na kurudia tena wiki hii kuwa CCM isipoangalia vyema ina uwezekano mkubwa wa kuondolewa Madarakani mwaka huu.


  • Mh. Frederick Sumaye (waziri mkuu mstaafu), naye ameshasema mara kadhaa kuwa kwa jinsi CCM ilipofikia sasa, isipofanya maamuzi sahihi, kuna wasiwasi wa kushinda hapo Oktoba Mwaka huu.


  • Mama wa Taifa, mama Maria Nyerere alishawaambia CCM kuwa kwa jinsi walivyokwishavuruga maadili ya Taifa yalivyoasisiwa na Baba wa Taifa, wananchi wa sasa sio wa enzi za Mwalimu, na wanaweza kuchagua Vyama vungine kutawala.


  • Mh Balozi Paul Ndhobo; aliyekuwa mtu muhimu sana ktk Uongozi na Utawala wa CCM awamu wa 1 na 2, alisema wazi kuwa kwa jinsi CCm ilipofikia pabaya, na nguvu ya Upinzani kukua, kuna hatari ya CCM kung'olewa.


  • Mh. Njelu Kassaka; ameshasema na kurudia mara kadhaa kuwa Mwaka huu CCM ipo ktk hatari kubwa ya kuondolewa Madarakani kwa kushindwa kuona nini jamii imekuwa ikikitafuta na sasa Wapinzani wanayo majibu.


  • Mh. Rais JK; katika matukio mbalimbali, JK amesisitiza akirudia kuwaambia wanaCCM wenzake kuwa "siwatishi ila ukweli ni kuwa 'Watanzania wa sasa wameamka' na CCM ijiangalie sana" na hivi juzi tu ktk Vikao vya CCM Dodoma, ameongea 'macho makavu' akirudia yaleyale, ...watanzania wa sasa sio wale waliokuwa 'wanaelekezwa' tu kuichagua CCM...kuwa CCM inaweza kuondoka, na ikiondoka hairudi tena, na akatoa mifano ya Vyama vya Ukombozi ktk mataifa kadhaa vimetokweka kabisa baada ya kung'olewa.


  • Mh Edward Lowassa (Waziri Mkuu aliyejiuzulu); ambaye sasa ndiye anayeonekana tishio ktk watakaogombea Urais kupitia CCM, Hapo jana tu, amesema yale yale Rais JK aliyosema majuzi ktk Vikao vya CCM. Lowassa amesema wazi kuwa 'hali sio njema' hata kidogo, kwa Mwenendo wa CCM, na "Upinzania wamejiandaa na Wanajiandaa sana", akasema, "tusipojiangalia vizuri, historia ya CCM itaondoka, tutaondolewa ktk uchaguzi Oktoba" naye akasisitiza na akatoa mifano ya Vyama vya Ukombozi ktk mataifa kadhaa vimetoweka kabisa baada ya kung'olewa! Akaitahadharisha CCM.


  • Kauli hizi na nyingine kali za waanzilishi wa CCM, ni ishara ya kuwa 'Malaika wa Ukombozi' anawaangazia na hivyo MKiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva atambue 'maono' haya, alinde HAKI, asiharibu huu Ukombozi.

My Take;
Taifa linakwenda kukombolewa ifikapo Oktoba. Welcome Tanganyika Mpya!
Huu ndio ujumbe wa Ukombozi kwa wazalendo na UKAWA chini ya LOWASSA! Bado wale 'wachumia tumbo' Lizaboni, Simiyu Yetu, MwanaDiwani, Ritz et al..na 'vitendea kazi' wengine wa Gamba's kuwa huu ni wakati wao 'kujiunga na ukombozi wa Umma', MAKOMEA atawahi kulala tarehe 25/10/2015 '...Utawala wa UKAWA ni Mpango wa Mungu...hauna muda wa kulipiza kisasi!' - by F. A. Mbowe, [UKAWA, 24 May 2015]

Tunakumbushia tu na kuweka dira sawa...Ndiko tunakoelekea??


 
Pia Nyerere aliwahi kusema kuwa "Watanzania wasipopata mabadiliko ndani ya CCM basi watayatafuta nje ya CCM" Naam kama ndoto ya king Luther ilivyotimia ndivyo ndoto ya Nyerere itakavyotimia!
 
Tutafika kweli
 

Attachments

  • 1432627495129.jpg
    1432627495129.jpg
    44.5 KB · Views: 922
  • 1432627504220.jpg
    1432627504220.jpg
    41.1 KB · Views: 870
  • 1432627514293.jpg
    1432627514293.jpg
    36.4 KB · Views: 844
  • 1432627524170.jpg
    1432627524170.jpg
    47.1 KB · Views: 810
  • 1432627533249.jpg
    1432627533249.jpg
    25.7 KB · Views: 806
Ccm inapendwa mno na watz. Itakaa madarakani milele na milele.

Mh!!!!Alichoumba Mungu tu kina mwisho.Wewe hapo ulipo maisha yako mwisho kabisa ni miaka 75,sembuse CCM.

Hongera sana kwa kufikiria hivyo, mwenyekiti wako ameanza mapema kuwaandaa nduguze, msije mkakimbilia JWTZ shauri yenu.
 
Mimi mpenzi na mwanachama mtiiifu wa CCM,wazee wangu ni makada wa kubwa wa CCM, huna lakuwambia kuhusu chama tawala,chama tawala CCM ni kila kitu kwao wao,,, lakini kutokana na siasa mbovu na kejeli kwa watanzania naona bora CCM kiachie madaraka kikajipange upya kwa sasa watanzania tumekichoka nacho.....
 
Uchambuzi umekaa vizuri, tuendeelee kuuelimisha umma,huu c mda wa kushabikia CCM ambayo imeshindwa kuwepeleka watanzania kwenye matamanio ya maisha bora
 
Good analysis.! kuna jambo moja huwa ccm wannajiaminisha nalo 'eti ccm INA hazina kubwa ya viongozi' na wapinzani wana safu nyembamba ya viongozi.

Wanadai eti mwalimu alisema upinzani wakweli utatoka ndani ya ccm, kwa mantiki hiyo wanaamini muda bado pia wanajitahidi kudhibitiana ili wasimeguke, ingawakuna makundi mengi yanayotofautian kimtazamo na kiitikadi,

Wanashindwa kufanya hesabu rahisi tu, ya kuwa wakati uliopita ccm ilihodhi kila kitu na ilidhibiti kila MTU, mambo ni tofauti sana kwa sasa, mfumo huria umefungua mambo mengi,

kwanza population imeongezeka sana hii imepelekea kuwa na kundi kubwa LA watu ambao hawana vyama, na ndani ya kundi hili kubwa LA wananchi halina hofu na ccm na hadhibitiwi na halichangamani na itikadi yoyote,

kundi hili litaiondoa ccm madarakani, ukawa wamejaribu kulishawishi kundi hili. ccm wameshindwa lulidhibiti na kulishawishi, hili kundi Lina wasomi wazuri.wafanyakazi,wanafunzi wakulima,

Kundi hili litatoa wanasiasa wapya wengi sana bungeni na madiwani,
Ccm hawataamini kitakachotokea October 25, zile njozi zao eti wao ndo wana wanasiasa mahiri wa kuongoza nchi zinaenda kuyeyuka,

Kwa jinsi ninavyoona upinzani unaweza uchukue nchi bila ya mpasuko ndani ya ccm, upinzani unajitosheleza, kila idara,
 
Historia haitufundishi hivyo.Sisiemu itang'oka tu kwani watz sasa wameamka.Watu wamechoka na chama cha ccm kwa sababu hakina lake jambo ila kutaka kuwa na madaraka ili kiwe na madaraka.
 
unajua bhana , hii tahadhari tumeitoa miaka mingi sana lakini Wameziba masikio , hata hivyo tunamshukuru Mungu kwa kusikia kilio cha umma .
 
Pamoja sana Mkuu mliberali na kwa taarifa tu ni kuwa UKAWA ukiunganisha vichwa makini vilivyopo CHADEMA, CUF, NCCR na NLD, kuna viongozi na Wanasiasa wakali wapatao zaidi ya 250, nje ya tunaowaona majukwaani, ambao hadi sasa wapo 'invisible' kwa sababu fulani za kimsingi, tunazozijua, na wengine wamesisitiza 'kutokuwekwa wazi sasa', na itakapofikia kuidondosha CCM na kuunda Serikali Mpya ya UKAWA, hapo CCM wenyewe hawataamini kuwa UKAWA inalo kundi wa viongozi na wanasiasa wengi kama itakavyotokea...! watabakia macho na midomo wazi wasiamini!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom