Habari ndugu zangu,
Poleni na majukumu ya kila siku.Nahitaji ushauri wenu ni muhimu.
Tukiwa kwenye uchumba na huyu mke wangu kuna kitu kilijitokeza mpaka nikafanya yaliyotokea.Ni miaka miwili imepita sasa tangu tukio litokee ila hata ndugu zangu hawajui. Huyu mke wangu alikuwa anataka kubeba mimba kabla hatujakamilisha taratibu zote hiyo kunilazimu na mimi nikubaliane naye.
Nilimwambia haina uharaka lakini yeye akawa anasisitiza tulijaribu mara kadhaa bila mafanikio mpaka akaanza kujihisi ana matatizo na akawa na wasiwasi hii ilinitia hofu na mimi kuwa yawezekana nina matatizo kwani sikuwahi kumpa ujauzito binti yeyote katika mapito yangu.
Ilinibidi nichepuke na binti mmoja kwa kumvizia mpaka siku zake za hatari na akapata ujauzito. hapo nikawa na uhakika kidogo niko fit huyu mwenzangu nikaendelea kumsisitizia kuwa kuna vitu Mungu ndie anapanga aafu ili ijulikane una tatizo kuna muda ambao ni lazima uwe umepita mkishirikiana na jamaa yako.
Mtoto alipozaliwa anafanana nami ila nilimwambia mama yake anilindie ndoa yangu na kaweka siri.Nimeoa niko na huyu mke wangu na ana mtoto sasa hivi na tunaishi kwa amani yule mtoto mwingine namlea kwa siri sana kwani namtumia tu matumizi mama yake na tunaishi mbali mbali.
Nataka ifike kipindi niweke mambo wazi kwani sitapenda iendelee kuwa siri mke wangu nampenda sana, naogopa ataumia sana ni presha zake ndio zilinitia hofu na mimi mpaka yakatokea yaliyotokea nitaanzaje kulihalalisha hili suala?
Naombeni mawazo yenu
Habari ndugu zangu,
Poleni na majukumu ya kila siku.Nahitaji ushauri wenu ni muhimu.
Tukiwa kwenye uchumba na huyu mke wangu kuna kitu kilijitokeza mpaka nikafanya yaliyotokea.Ni miaka miwili imepita sasa tangu tukio litokee ila hata ndugu zangu hawajui. Huyu mke wangu alikuwa anataka kubeba mimba kabla hatujakamilisha taratibu zote hiyo kunilazimu na mimi nikubaliane naye.
Nilimwambia haina uharaka lakini yeye akawa anasisitiza tulijaribu mara kadhaa bila mafanikio mpaka akaanza kujihisi ana matatizo na akawa na wasiwasi hii ilinitia hofu na mimi kuwa yawezekana nina matatizo kwani sikuwahi kumpa ujauzito binti yeyote katika mapito yangu.
Ilinibidi nichepuke na binti mmoja kwa kumvizia mpaka siku zake za hatari na akapata ujauzito. hapo nikawa na uhakika kidogo niko fit huyu mwenzangu nikaendelea kumsisitizia kuwa kuna vitu Mungu ndie anapanga aafu ili ijulikane una tatizo kuna muda ambao ni lazima uwe umepita mkishirikiana na jamaa yako.
Mtoto alipozaliwa anafanana nami ila nilimwambia mama yake anilindie ndoa yangu na kaweka siri.Nimeoa niko na huyu mke wangu na ana mtoto sasa hivi na tunaishi kwa amani yule mtoto mwingine namlea kwa siri sana kwani namtumia tu matumizi mama yake na tunaishi mbali mbali.
Nataka ifike kipindi niweke mambo wazi kwani sitapenda iendelee kuwa siri mke wangu nampenda sana, naogopa ataumia sana ni presha zake ndio zilinitia hofu na mimi mpaka yakatokea yaliyotokea nitaanzaje kulihalalisha hili suala?
Naombeni mawazo yenu
Habari ndugu zangu,