Nilizaa nje ya ndoa, nitahalalishaje hili suala?

Nilizaa nje ya ndoa, nitahalalishaje hili suala?

Mkuu mwambie ukweli kama uliosema hapa kuwa ulienda kujaribisha kama uko fit baada ya yeye mwenyewe kukutia wasiwasi, aaah sipati picha hivyo reaction yake!! ila ndo ukweli wenyewe kwa mujibu wa maelezo yako.

Hahaaa hizi ndoa zina vituko jamani loh!!

Hahahaaaa! Yaani hizi ndoa jamani!! Hivi kumbe ukihisi unatatizo hutakiwi kwenda hospital ila ni kuchepuka tu!! Ye aseme tu ukweli wote kama alivyoueleza hapa, mengine atajua baada ya kuueleza huo ukweli.
 
Hahahaaaa! Yaani hizi ndoa jamani!! Hivi kumbe ukihisi unatatizo hutakiwi kwenda hospital ila ni kuchepuka tu!! Ye aseme tu ukweli wote kama alivyoueleza hapa, mengine atajua baada ya kuueleza huo ukweli.

Ndo ushangae na wewe sista
 
Mbona hiyo ipo open tu , mwache mtoto akue kidogo afu badae akifika miaka 5 mchukue , mweleze mkeo huyu ni mtoto

wangu full stop sitaki maswali , ujue sisi wanawake tuna roho ya korosho ila wee kuwa mbishi ni mtoto wako there is no

way utamkwepa DNA content zako na huyo dogo. mwambie live tu japo ataumia
We nae utakua umezaa na mume wa mtu na hujaolewa si bure....eti amchukue then hataki maswalI.?? Ndoa haiendi hivyo nikwambie..ni swala la kufikisha ujumbe na kujadiliana..lkn sio ukatili km wako eti full amri khaaa kwani umeahakikishiwa mwanamke atakataa..mumewe akiongea nae kwa ustaarabu ishu itasovika...hujaolewa hujui ndoa ni nini
 
Mkuu weka ukweli wazi utakuwa huru so usiogope we sema ilimradi ni damu yako
 
Habari ndugu zangu,

Poleni na majukumu ya kila siku.Nahitaji ushauri wenu ni muhimu.

Tukiwa kwenye uchumba na huyu mke wangu kuna kitu kilijitokeza mpaka nikafanya yaliyotokea.Ni miaka miwili imepita sasa tangu tukio litokee ila hata ndugu zangu hawajui. Huyu mke wangu alikuwa anataka kubeba mimba kabla hatujakamilisha taratibu zote hiyo kunilazimu na mimi nikubaliane naye.

Nilimwambia haina uharaka lakini yeye akawa anasisitiza tulijaribu mara kadhaa bila mafanikio mpaka akaanza kujihisi ana matatizo na akawa na wasiwasi hii ilinitia hofu na mimi kuwa yawezekana nina matatizo kwani sikuwahi kumpa ujauzito binti yeyote katika mapito yangu.

Ilinibidi nichepuke na binti mmoja kwa kumvizia mpaka siku zake za hatari na akapata ujauzito. hapo nikawa na uhakika kidogo niko fit huyu mwenzangu nikaendelea kumsisitizia kuwa kuna vitu Mungu ndie anapanga aafu ili ijulikane una tatizo kuna muda ambao ni lazima uwe umepita mkishirikiana na jamaa yako.

Mtoto alipozaliwa anafanana nami ila nilimwambia mama yake anilindie ndoa yangu na kaweka siri.Nimeoa niko na huyu mke wangu na ana mtoto sasa hivi na tunaishi kwa amani yule mtoto mwingine namlea kwa siri sana kwani namtumia tu matumizi mama yake na tunaishi mbali mbali.

Nataka ifike kipindi niweke mambo wazi kwani sitapenda iendelee kuwa siri mke wangu nampenda sana, naogopa ataumia sana ni presha zake ndio zilinitia hofu na mimi mpaka yakatokea yaliyotokea nitaanzaje kulihalalisha hili suala?

Naombeni mawazo yenu

Habari ndugu zangu,

Poleni na majukumu ya kila siku.Nahitaji ushauri wenu ni muhimu.

Tukiwa kwenye uchumba na huyu mke wangu kuna kitu kilijitokeza mpaka nikafanya yaliyotokea.Ni miaka miwili imepita sasa tangu tukio litokee ila hata ndugu zangu hawajui. Huyu mke wangu alikuwa anataka kubeba mimba kabla hatujakamilisha taratibu zote hiyo kunilazimu na mimi nikubaliane naye.

Nilimwambia haina uharaka lakini yeye akawa anasisitiza tulijaribu mara kadhaa bila mafanikio mpaka akaanza kujihisi ana matatizo na akawa na wasiwasi hii ilinitia hofu na mimi kuwa yawezekana nina matatizo kwani sikuwahi kumpa ujauzito binti yeyote katika mapito yangu.

Ilinibidi nichepuke na binti mmoja kwa kumvizia mpaka siku zake za hatari na akapata ujauzito. hapo nikawa na uhakika kidogo niko fit huyu mwenzangu nikaendelea kumsisitizia kuwa kuna vitu Mungu ndie anapanga aafu ili ijulikane una tatizo kuna muda ambao ni lazima uwe umepita mkishirikiana na jamaa yako.

Mtoto alipozaliwa anafanana nami ila nilimwambia mama yake anilindie ndoa yangu na kaweka siri.Nimeoa niko na huyu mke wangu na ana mtoto sasa hivi na tunaishi kwa amani yule mtoto mwingine namlea kwa siri sana kwani namtumia tu matumizi mama yake na tunaishi mbali mbali.

Nataka ifike kipindi niweke mambo wazi kwani sitapenda iendelee kuwa siri mke wangu nampenda sana, naogopa ataumia sana ni presha zake ndio zilinitia hofu na mimi mpaka yakatokea yaliyotokea nitaanzaje kulihalalisha hili suala?

Naombeni mawazo yenu
Ushawah kumwambia mkeo ikitokea una mtoto wa nje utampenda?U never know akampenda mwanao ...Wangapi tunawaona wanalelewa vizuri tu.
 
usimweleze chochote,endelea kumlea kwa siri hadi wakati muafaka utakapofika,kwa sasa hutakuwa na ndoa au atakulipizia
 
kwa mioyo ya wanawake wengi ilivyo,hata akimweleza.ngoma iko palepale,tabia zitabadilika,mtoto atachukiwa,amani itavunjika,na mara nyingine hata huduma za ndani hatapata,ni bora iwe siri tu
 
Mkuu, nakushauri,
Mwanaume kaumbwa kifua..kifua kina sifa yake...kaza mambo kama haya moyoni ..
istoshe unaonekana upo katika ndoa mbichi..so kausha ...usimlopokee..subiri mifika walau miaka hamsini..umpasulie yai
unasubiri mpaka watoto wote wakue waanze chuo japo
 
Back
Top Bottom