Tate Mkuu
JF-Expert Member
- Jan 24, 2019
- 44,276
- 129,843
Dah! Naona hao jamaa wa Mbengo zetafongoka hapo pembeni wanakaribia kupasuka aisee!! Ni fungu ka 10 hilo bila shaka!!Kunonu Teknolojia walinituma nikampelekee mteja 'memory card' ya kamera. Nikiwa namsubiri mteja tuonane, macho yangu yakashuhudia ya kwenye 'muvi'. Mwanamke aliyembeba mtoto mdogo mgongoni huku kichwani kabeba ndoo angavu iliyojaa 'juisi za kandoro'. Akasimamishwa na mwanaume mmoja aliyeonakana ametoka 'lanchi'.
Huku akiongea na simu, mwanaume akatoa 'nyekundu' moja akampa yule mwanamke. Yule mdada akatua ndoo ampe 'juisi', lakini yule mwanaume alitikisa mkono ishara ya kutosheka na akaendelea na safari.
Yule mdada hakuamini kilichotokea, aligeuka kumwangalia jamaa zaidi ya mara mbili pasi macho kugongana. Alivuka barabara na kugeuka tena, jamaa aliendelea tu.
Nikajisemeza moyoni, ivi zile 'juisi za kandoro' hata zingeuzwa zote bado zisingefikia ile hela. Na yule mdada angetumia muda gani kumaliza huo mzigo? Na vipi kuhusu mtoto, na hili jua kali la jiji la Wazaramo? [emoji848]
Nikajiambia nikiwa mkubwa nataka niwe kama yule 'braza' wa Keko.
Simulizi hii imedhaminiwa na Kunonu Teknolojia , wauzaji wa memory cards, USB Flash Drives hard disks na SSDs.
Wasiliana nasi #0629831936 au #0765542197 tukuletee bidhaa yako popote Tanzania. View attachment 2392562
Siku zote hata mimi falsafa yangu ni kusaidia wenye uhitaji, badala ya kwenda kuwafurahisha viongozi wa dini.