Nilivyomshauri rafiki yangu aliyeachwa na mpenzi wake

Thomas10

JF-Expert Member
Mar 9, 2017
841
2,268
Rafiki yangu wa karibu, aliachwa na mwenzi aliyemhudumia kwa miaka takribani sita (6) hivi. Alianza nae mahusiano binti akiwa amemaliza kidato cha nne, aliapata ufaulu wa daraja la nne (div 4 point 28)

Alijitoa kumlipia ada na mahitaji mengine ya kibinadamu tangu alipoanza masomo ya ngazi ya cheti, akaunganisha stashahada, na kisha akaunga shahada.

Kwa kipindi chote hicho, ahadi kuu ya mahusiano yao ilikuwa kuoana. Baada ya binti kumaliza, aliamua kumwambia jamaa kuwa hawezi tena kuendelea naye na hivyo atafute mwanamke mwingine. Kwakuwa binti tayari alipata kazi kwenye taasisi fulani, akamuomba amrudishie pesa yake kidogokidogo hadi itakapokwisha.

Jamaa alikosa cha kuamua, akaja kwangu amevurugwa mno, amejawa roho ya kuua, akaniomba ushauri. Hapo nilikumbuka mafunzo ya mjomba wangu kuhusu mke na maisha ya ndoa. Nikalazimika kumpa ushauri ambao ulikuwa kwa mtindo wa maswali ambapo sikumtaka ajibu, bali atafakari na akipata majibu, afanye uamuzi;

Kwako wewe (rafiki) mke ni nani na ndoa ni nini?
Unapofikiria kuhusu kuoa, unalenga kuoa ili iweje?
Mke utakayemuoa, unataka akutimizie wajibu gani?
Katika wanawake uliowahi kuwa nao na unaowaona mtaani, wamepungukiwa nini linapokuja suala la mke?
Unataka kuoa kutimiza hisia au kutengeneza familia?
Ukimuoa mwanamke uliyemgharamia utakuwa umepata mke bora au umepata mwanamke wa kuoa?

Maswali hayo mepesi kabisa, nilimwambia aende akayajibu moyoni mwake usiku ule, hata wiki hadi mwezi. Akiona majibu yote yanaangukia kwa huyo mwanamke aliyemgharamia, basi amuue (kama alivyopanga) na akiona wapo wanawake wengi wanajibu hayo, basi amsamehe na aendelee na maisha yake.

Sasa ni miezi miwili, ameamua kumsamehe yule binti, amemwambia hata pesa asimrudishie.

Anaumia sana, lakini anaamini itaisha.

1623318478222.png
 
Hapo ni sawa aliingilia majukumu ya wazazi wa mwanamke. Wala asiwaze kuua mtu.

Ajipige kifuani mara tatu kisha aweke akilini mwake kuwa alikuwa anamsomesha yatima. Wala asifikirie malipo ya msaada wake ni Mungu tu atamlipia thawabu kivingine.

Tena akizingatia huu ushauri wangu baada ya miaka kadhaa huyo Binti mambo yake yakiwa mazuri atarudi kumshukuru kwa namna nyingine au huyo Binti atakuja kupitia mapito ya mahusiano mabaya.
 
Swala la kuachana na mwenzi linauma sana ijapokua ni hali ya kawaida na kutokea mara kwa mara tu.


Wakati mwingine hata mwanamke unawezakuta umemuoa na akakuchoka kabisa au ukamchoma kabisa ila unajikuta kuvumilia sababu ya mtoto au kushikilia tu ndoa isivunjike.


Kinachotoa uhalali wa mwanamke kumuacha Jamaa hapo ni Kua hawana ndoa, ila hata kama wangekua Kwenye ndoa basi ingekua tu ni kuishikilia isivunjike ila iko wazi Kua mwanamke alishamchoka jamaa hapo
 
Swala la kuachana na mwenzi linauma sana ijapokua ni hali ya kawaida na kutokea mara kwa mara tu.


Wakati mwingine hata mwanamke unawezakuta umemuoa na akakuchoka kabisa au ukamchoka kabisa ila unajikuta kuvumilia sababu ya watoto au kushikilia tu ndoa isivunjike.


Kinachotoa uhalali wa mwanamke kumuacha Jamaa hapo ni Kua hawana ndoa, ila hata kama wangekua Kwenye ndoa basi ingekua tu ni kuishikilia isivunjike ila iko wazi Kua mwanamke alishamchoka jamaa hapo
 
Dah pole sana kwa huyo Rafiki yako hakika anapitia maumivu makali sana

anyway ulimshauri vizuri na uamuzi aliofikia ni mzuri pia

na akaze hivyo hivyo kwa sababu hakuna hali au jambo ambalo ni la kudumu katika hii dunia kila jambo na hali ni za kupita tu,hata hilo litapita na itabaki kuwa historia

kwenye Maisha kuna kanuni ambazo ukizivunja lazima uyapate matokeo yake huna namna ya kukwepa nenda uendako,

Rafiki yako ameitumia kanuni ya kusamehe na kutenda mema bila kutegemea malipo,hii kanuni ukiishi kamwe haiwezi kukuangusha kwa hiyo jamaa yako atarajie kupata malipo ya kuiishi hii kanuni

huyo mchumba wa jamaa kavunja kanuni kama mbili muhimu sana,kwanza kamwe usicheze na hisia za mwingine,ya pili usimlipe uovu yule aliyekutendea wema,kwa hiyo ajipange kusbiria matokeo ya maamuzi yake na huwa hayakimbiliki

sema zidi kumshuri huyo mkaka akaze na asonge mbele ili baadae dada akianza kuvuna matokeo ya mamuzi yake asije akarudi kumghilibu jamaa warudiane ili washiriki pamoja matokeo yake ya kuvunja kanuni hizo mbili

kila la kheri kwa mwenzetu.
 
eheeee hapo tulia kwanza ,hakusikia kuwa usisomeshe mchumba, ngoja nimalizie story then nikushauri ukamshauri
 
Swala la kuachana na mwenzi linauma sana ijapokua ni hali ya kawaida na kutokea mara kwa mara tu.


Wakati mwingine hata mwanamke unawezakuta umemuoa na akakuchoka kabisa au ukamchoma kabisa ila unajikuta kuvumilia sababu ya mtoto au kushikilia tu ndoa isivunjike.


Kinachotoa uhalali wa mwanamke kumuacha Jamaa hapo ni Kua hawana ndoa, ila hata kama wangekua Kwenye ndoa basi ingekua tu ni kuishikilia isivunjike ila iko wazi Kua mwanamke alishamchoka jamaa hapo
yaaap kwa upande mwingine bora alivokataa mapema kuliko kuoana then michepuko ianze ndo zinakuja habari za kuleteana watoto sio wako
 
Rafiki yangu wa karibu, aliachwa na mwenzi aliyemhudumia kwa miaka takribani sita (6) hivi. Alianza nae mahusiano binti akiwa amemaliza kidato cha nne, aliapata ufaulu wa daraja la nne (div 4 point 28)

Alijitoa kumlipia ada na mahitaji mengine ya kibinadamu tangu alipoanza masomo ya ngazi ya cheti, akaunganisha stashahada, na kisha akaunga shahada.

Kwa kipindi chote hicho, ahadi kuu ya mahusiano yao ilikuwa kuoana. Baada ya binti kumaliza, aliamua kumwambia jamaa kuwa hawezi tena kuendelea naye na hivyo atafute mwanamke mwingine. Kwakuwa binti tayari alipata kazi kwenye taasisi fulani, akamuomba amrudishie pesa yake kidogokidogo hadi itakapokwisha.

Jamaa alikosa cha kuamua, akaja kwangu amevurugwa mno, amejawa roho ya kuua, akaniomba ushauri. Hapo nilikumbuka mafunzo ya mjomba wangu kuhusu mke na maisha ya ndoa. Nikalazimika kumpa ushauri ambao ulikuwa kwa mtindo wa maswali ambapo sikumtaka ajibu, bali atafakari na akipata majibu, afanye uamuzi;

Kwako wewe (rafiki) mke ni nani na ndoa ni nini?
Unapofikiria kuhusu kuoa, unalenga kuoa ili iweje?
Mke utakayemuoa, unataka akutimizie wajibu gani?
Katika wanawake uliowahi kuwa nao na unaowaona mtaani, wamepungukiwa nini linapokuja suala la mke?
Unataka kuoa kutimiza hisia au kutengeneza familia?
Ukimuoa mwanamke uliyemgharamia utakuwa umepata mke bora au umepata mwanamke wa kuoa?

Maswali hayo mepesi kabisa, nilimwambia aende akayajibu moyoni mwake usiku ule, hata wiki hadi mwezi. Akiona majibu yote yanaangukia kwa huyo mwanamke aliyemgharamia, basi amuue (kama alivyopanga) na akiona wapo wanawake wengi wanajibu hayo, basi amsamehe na aendelee na maisha yake.

Sasa ni miezi miwili, ameamua kumsamehe yule binti, amemwambia hata pesa asimrudishie.

Anaumia sana, lakini anaamini itaisha.

Mke hasomeshwi, ana mzazi wake, mwache amalize kusomeshwa na mzazi wake uoe, kumbuka unategemea akuzalie watoto ili uwasomeshe kwa hiyo usijibebeshe majukumu ya wazazi wengine wakati majukumu yako kama mzazi bado yanakusubiri
 
Kwahyo wakat tunakata pindi la MCHUMBA HASOMESHWI alikuwa wapi??...!!anaturudisha nyuma...atasoma tuition
 
Kumsomesha mchumba ni sawa na mpangaji kukarabati nyumba alafu akataka iwe yake
 
Nlioa, nikaweka mimba, na sasa nasomesha mtu na mama ake ili kuwajengea uwezo. Akinizingua matunda atakula dogo safiii sina kinyongo wala maumivu, tunasomesha mke!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Toa kama unasaidia ila sio kwa ahadi ya kuoana/ kutegemea kupata kitu fulani toka kwa huyo mwenza wako.

Mfano mpenzi wako kakwama kiasi fulani cha ada mpe kama unamsaidia na kiwe ndani ya uwezo wako sio ukakukuruka kupata iyo hela, moyoni ukijiambia et huyu ni mke wangu mtarajiwa lazma nimsaidie kwasababu tu ndie ntakae muoa. Huo ndio ujuha ndio maana wanajinyonga.
 
Back
Top Bottom