Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,741
Kabila langu ni Mkwe.re. Nilizaliwa katika Kijiji cha Mdaula, Chalinze, miaka ishirini na nne iliyopita. Wazazi wangu walinipa jina la Tunu.
Nilikuwa mtoto wa kwanza katika familia ya mzee Rajab Athumani. Tulizaliwa wawili tu mimi na mdogo wangu aliyeitwa Inana. Tulipishana kuzaliwa kwa miaka mitatu.
Nilipofikia umri wa miaka saba nilipelekwa shule nikaanza darasa la kwanza. Mpaka ninafika darasa la nne Inana alianza darasa la kwanza. Wakati nipo darasa la saba Inana alikuwa darasa la nne.
Sikutegemea kuwa ningefaulu kwenda sekondari lakini ukweli ni kuwa nilifaulu nikaanza masomo ya sekondari. Wakati nipo kidato cha tatu na Inana akiwa darasa la sita wazazi wetu walifariki dunia ghafla kutokana na ajali ya gari.
Umauti uliwakuta kwa pamoja wakiwa katika basi wakitokea Morogoro. Basi hilo liligongana uso kwa uso na lori la mafuta. Basi lilipinduka mara tatu. Baadhi ya abiria wakiwemo baba na mama yetu walikufa hapohapo.
Huo ukawa mwisho wa masomo yetu. Mimi nilikomea kidato cha tatu, Inana alikomea darasa la saba. Hatukuwa na ndugu wa kutuhudumia wala kutuongoza. Ndugu waliokuwepo hawakutujali. Tukawa tunaishi kivyetuvyetu mimi na mdogo wangu.
Nilikuwa ninatoka asubuhi kwenda Chalinze kutafuta vibarua ili tupate pesa za kutuwezesha kuishi. Nilikuwa napata vibarua vya kufua mashuka kwenye magesti mbalimbali na ninaporudi nyumbani jioni tunaanza kupika na mdogo wangu.
Kwa muda wa miaka mitatu tukawa tunaishi kwa kuhangaika. Mwisho nikawa namchukua mdogo wangu na kwenda naye Chalinze kufanya naye vibarua.
Ile nyumba tuliyokuwa tunaishi pale Mdaula ilikuwa ya udongo. Wakati wa mvua ilikuwa
inavuja. Iliendelea kuvuja na mwisho ikaanza kubomoka kidokidogo. Hatukuwa na uwezo wa kuijenga kwa sababu pesa tulizokuwa tunapata ziliishia kwenye chakula tu.
Katika msimu mmoja wa masika nyumba yetu ilibomoka yote na kubakia chumba kimoja tulichokuwa tunalala sisi ambacho kuta zake zilikuwa zimejaa matundu. Mtu akipita nje unamuona.
Usiku mmoja tulikuwa tumechutama kwenye pembe moja ya chumba chetu. Mvua ilikuwa inanyesha na chumba kizima kilikuwa kinavuja. Tulikuwa tumejifunika shuka moja lililokuwa limeloa maji tukiisikiliza mvua. Godoro lilikuwa limeloa chapachapa. Ndani ya
chumba kulikuwa kumejaa vidimbwi vya maji hadi uvunguni mwa kitanda.
Ghafla ukuta wa upande mmoja wa chumba ukaanguka. Kwa bahati njema uliangukia nje. Kama ungeangukia ndani ungetuua.
Ulianguka kwa kishindo kikubwa. Mimi na Inana tulishituka tukajua tumeshakufa. Tukataka kukimbia lakini hatukujua tukimbilie wapi kwani mvua bado ilikuwa ikinyesha kwa nguvu na ilikuwa usiku. Tukabaki palepale.
Kwa vile kulikuwa wazi, ubaridi ulikuwa ukitupiga na vile tulivyokuwa tumeshaloa tulikuwa tunatetemeka kwa baridi. Inana alikuwa akiweweseka.
"Vumilia mdogo wangu. Yote yatapita. Hakuna lisilo na mwisho," nikamwambia kumfariji.
Inana akanitazama. Mdomo wake ulikuwa wazi. Meno yake yalikuwa yakichezacheza na uso wake ulijaa michirizi ya maji.
"Ukuta umeshaanguka dada'ngu, tutafanyaje?" Akaniuliza kwa sauti ya kutetemeka kama mwenye homa.
"Itabidi tuuzibe kabla hakujakucha."
"Tutauziba na nini?"
"Tutafunga nguo ambazo hatuzitumii. Tusubiri mvua iache."
Mvua ilipoacha tukatoa maji yaliyokuwa yamejaa mle chumbani. Tulikuwa tunayachota na kuyamwaga nje. Tulipomaliza tulikamua nguo zetu zilizokuwa zimeloa tukaenda kuzianika.
Baada ya hapo tukaanza kazi ya kuuziba ule ukuta. Tulichimbia tena miti ya ukuta huo kisha tukaanza kufunga nguo ambazo zilikuwa hazitumiki tena.
Je, nini kilendelea? Usikose kufuatilia
Nilikuwa mtoto wa kwanza katika familia ya mzee Rajab Athumani. Tulizaliwa wawili tu mimi na mdogo wangu aliyeitwa Inana. Tulipishana kuzaliwa kwa miaka mitatu.
Nilipofikia umri wa miaka saba nilipelekwa shule nikaanza darasa la kwanza. Mpaka ninafika darasa la nne Inana alianza darasa la kwanza. Wakati nipo darasa la saba Inana alikuwa darasa la nne.
Sikutegemea kuwa ningefaulu kwenda sekondari lakini ukweli ni kuwa nilifaulu nikaanza masomo ya sekondari. Wakati nipo kidato cha tatu na Inana akiwa darasa la sita wazazi wetu walifariki dunia ghafla kutokana na ajali ya gari.
Umauti uliwakuta kwa pamoja wakiwa katika basi wakitokea Morogoro. Basi hilo liligongana uso kwa uso na lori la mafuta. Basi lilipinduka mara tatu. Baadhi ya abiria wakiwemo baba na mama yetu walikufa hapohapo.
Huo ukawa mwisho wa masomo yetu. Mimi nilikomea kidato cha tatu, Inana alikomea darasa la saba. Hatukuwa na ndugu wa kutuhudumia wala kutuongoza. Ndugu waliokuwepo hawakutujali. Tukawa tunaishi kivyetuvyetu mimi na mdogo wangu.
Nilikuwa ninatoka asubuhi kwenda Chalinze kutafuta vibarua ili tupate pesa za kutuwezesha kuishi. Nilikuwa napata vibarua vya kufua mashuka kwenye magesti mbalimbali na ninaporudi nyumbani jioni tunaanza kupika na mdogo wangu.
Kwa muda wa miaka mitatu tukawa tunaishi kwa kuhangaika. Mwisho nikawa namchukua mdogo wangu na kwenda naye Chalinze kufanya naye vibarua.
Ile nyumba tuliyokuwa tunaishi pale Mdaula ilikuwa ya udongo. Wakati wa mvua ilikuwa
inavuja. Iliendelea kuvuja na mwisho ikaanza kubomoka kidokidogo. Hatukuwa na uwezo wa kuijenga kwa sababu pesa tulizokuwa tunapata ziliishia kwenye chakula tu.
Katika msimu mmoja wa masika nyumba yetu ilibomoka yote na kubakia chumba kimoja tulichokuwa tunalala sisi ambacho kuta zake zilikuwa zimejaa matundu. Mtu akipita nje unamuona.
Usiku mmoja tulikuwa tumechutama kwenye pembe moja ya chumba chetu. Mvua ilikuwa inanyesha na chumba kizima kilikuwa kinavuja. Tulikuwa tumejifunika shuka moja lililokuwa limeloa maji tukiisikiliza mvua. Godoro lilikuwa limeloa chapachapa. Ndani ya
chumba kulikuwa kumejaa vidimbwi vya maji hadi uvunguni mwa kitanda.
Ghafla ukuta wa upande mmoja wa chumba ukaanguka. Kwa bahati njema uliangukia nje. Kama ungeangukia ndani ungetuua.
Ulianguka kwa kishindo kikubwa. Mimi na Inana tulishituka tukajua tumeshakufa. Tukataka kukimbia lakini hatukujua tukimbilie wapi kwani mvua bado ilikuwa ikinyesha kwa nguvu na ilikuwa usiku. Tukabaki palepale.
Kwa vile kulikuwa wazi, ubaridi ulikuwa ukitupiga na vile tulivyokuwa tumeshaloa tulikuwa tunatetemeka kwa baridi. Inana alikuwa akiweweseka.
"Vumilia mdogo wangu. Yote yatapita. Hakuna lisilo na mwisho," nikamwambia kumfariji.
Inana akanitazama. Mdomo wake ulikuwa wazi. Meno yake yalikuwa yakichezacheza na uso wake ulijaa michirizi ya maji.
"Ukuta umeshaanguka dada'ngu, tutafanyaje?" Akaniuliza kwa sauti ya kutetemeka kama mwenye homa.
"Itabidi tuuzibe kabla hakujakucha."
"Tutauziba na nini?"
"Tutafunga nguo ambazo hatuzitumii. Tusubiri mvua iache."
Mvua ilipoacha tukatoa maji yaliyokuwa yamejaa mle chumbani. Tulikuwa tunayachota na kuyamwaga nje. Tulipomaliza tulikamua nguo zetu zilizokuwa zimeloa tukaenda kuzianika.
Baada ya hapo tukaanza kazi ya kuuziba ule ukuta. Tulichimbia tena miti ya ukuta huo kisha tukaanza kufunga nguo ambazo zilikuwa hazitumiki tena.
Je, nini kilendelea? Usikose kufuatilia