alexmahone
JF-Expert Member
- Apr 8, 2011
- 482
- 406
Hapo nahisi M bongo atakula risasi bila hata kuulizwa kitu,
Imetumwa via WhatsApp...
Mbongo, Mganda, na Mkenya walikamatwa na makosa Uchina.
Wakaambiwa adhabu ni ama kifo cha moja kwa moja au adhabu nyingine ambayo atakayeifaulu atakuwa huru, atakayeshindwa atauawa.
Basi wao wakaomba wapewe hiyo adhabu nyingine wajaribu bahati yao.
Wakapelekwa msituni wakaambiwa kila mmoja aende kwa njia yake halafu arudi na matunda kumi ya kufanana.
Wakaingia msituni kila mtu njia yake.
Mganda akarudi wa kwanza na machungwa kumi. Akaambiwa adhabu yake ni kumeza moja moja likiwa zima bila kufumba macho bila kulia wala kucheka wala kujitikisa mpaka yote kumi yaishe. Akameza la kwanza. Safi. Kumeza la pili, akashindwa kuvumilia akafumba macho. Akapigiwa risasi akafa.
Mkenya akaja. Ana vitunda vidogo vidogo kama pili vilaini. Akasomewa masharti. Akaanza kumeza bila kufumba macho wala kulia, wala nini... alipofika cha tisa akashindwa kuvumilia akaangua kicheko! Akapigwa risasi pia akafa.
Wakiwa kuzimu Mganda akamwuliza Mkenya, Vipi, mbona ulishindwa kuvumilia wakati kilibaki kitunda kimoja tu?
Mkenya akamjibu: Mkuu, nilishindwa kuzuia kicheko maana nilimwona Mbongo anakuja na matikiti maji!
hivi unamsema rais wetu namna hivi wewe kweli una maadili,baba yako unaweza kumsema namna hii.thats not a jokeAlipofika mbongo yale matikiti yakaonekana yamepasuka kumbe ndani kuna unga walipo mhoji kumbe alikuwa ni r i z o n e, ikabidi babayake aitwe, muafaka uka wekwa TZA ikawekwa rehani. r i z o n e akaachiwa huru. wabongo tunatisha kwa ujanja