Nilimwona Mbongo anakuja na.....

Nilimwona Mbongo anakuja na.....

Imetumwa via WhatsApp...

Mbongo, Mganda, na Mkenya walikamatwa na makosa Uchina.

Wakaambiwa adhabu ni ama kifo cha moja kwa moja au adhabu nyingine ambayo atakayeifaulu atakuwa huru, atakayeshindwa atauawa.

Basi wao wakaomba wapewe hiyo adhabu nyingine wajaribu bahati yao.

Wakapelekwa msituni wakaambiwa kila mmoja aende kwa njia yake halafu arudi na matunda kumi ya kufanana.

Wakaingia msituni kila mtu njia yake.

Mganda akarudi wa kwanza na machungwa kumi. Akaambiwa adhabu yake ni kumeza moja moja likiwa zima bila kufumba macho bila kulia wala kucheka wala kujitikisa mpaka yote kumi yaishe. Akameza la kwanza. Safi. Kumeza la pili, akashindwa kuvumilia akafumba macho. Akapigiwa risasi akafa.

Mkenya akaja. Ana vitunda vidogo vidogo kama pili vilaini. Akasomewa masharti. Akaanza kumeza bila kufumba macho wala kulia, wala nini... alipofika cha tisa akashindwa kuvumilia akaangua kicheko! Akapigwa risasi pia akafa.

Wakiwa kuzimu Mganda akamwuliza Mkenya, “Vipi, mbona ulishindwa kuvumilia wakati kilibaki kitunda kimoja tu?”

Mkenya akamjibu: “Mkuu, nilishindwa kuzuia kicheko maana nilimwona Mbongo anakuja na matikiti maji!”


mkuu umejitahidi kutumia tafsida kwa kuwa original version ya hayati Prof. Seith Chachage kwenye kitabu chake cha Makuwadi wa soko huria hakutumia kumeza kama wewe. Bravo for editing
 
hahahahahahahaha
tehtehtehtehtehteh
kwikwikwikwikwikwi
a e i o u
abcdefghijklmnopqrstuvwxyz
ma me mi mi mu
ta te ti to tu.
 
Du umetisha maana nimecheka mpaka machozi.
 
ha ha ha ha kuna mtu alikuwa amenichukiza yaani hasira zote zimeisha dah
 
Alipofika mbongo yale matikiti yakaonekana yamepasuka kumbe ndani kuna unga walipo mhoji kumbe alikuwa ni r i z o n e, ikabidi babayake aitwe, muafaka uka wekwa TZA ikawekwa rehani. r i z o n e akaachiwa huru. wabongo tunatisha kwa ujanja
hivi unamsema rais wetu namna hivi wewe kweli una maadili,baba yako unaweza kumsema namna hii.thats not a joke
 
DAAAAA wabongo kwa sifa sijui alidhani wanataka wao wale....
 
Wabongo hawashindwi kuja hata na fenesi

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Wachina walishindwa kufanya lolote......ilibidi wa mwambie we rudi tuu home tz kariakoo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom