Wakuu heshima kwenu!
Nimejikuta napata wakati mgumu sana kukutana na mtu ambaye niliwahi kumsumbua hata kujaribu kumtishia kwa namna moja...
Kuna dada mmoja, ambaye tulifahamiana kwenye workshop moja hivi mwanzoni mwa mwaka huu, ilikuwa inafanyikia mkoa wa Tanga nilikuwa nae kiukundi kimoja katika kazi na kwa bahati nzuri mimi na huyu dada tulikuwa tunatoka mkoa mmoja.
Offcoz ile kazi ilikuwa ngumu kidogo na ilihitaji akili na nguvu kuifanya!! Sasa huyu binti akawa anatega sana, na unakuta kazi zote nafanya mimi, ni binti mrembo! na kwa kweli anajua kutega kazi. Workshop ilikuwa ni ya muda mrefu kidogo, almost 4weeks!.
Kazi ikaendelea but ilifika mahali ikabidi nimbane binti ili afanye kazi, na nikajaribu kumlimit hata kwenye maswala ya muda, muda wa kula na muda wa mapumziko.
Hali ilimwia ngumu kidogo na ilifika kipindi akaamua kutofautiana na misimamo yangu katika kile kikundi chetu! akawa anawaambia members wengine kuwa mimi namdharau sana namwona legelege!! Mrembo kila akiniona lazima aongee maneno ya kulalamika na kusema namwonea, nilianza kumdharau kimtindo so kuna baadhi ya sehemu ilibidi nimpuuze na nilijaribu kuwaambia baadhi ya wadau pale wasimsaport, kuna kazi nyingine ni za serikali lakini ni ngumu.
Kwenye hiyo workshop tulikuwa tunalipwa 80,000/= per day malazi na meals excluded. Kadri siku zilovyokuwa zinaenda kazi ikawa inaongezeka ugumu, hapo ilibidi watu tuwe serious kweli kweli, kulala saa 5 usiku kuamka saa kumi na moja asubuhi.
Sasa msaada kwa huyu mrembo ukazidi kupungua kwa wale members wachache waliokuwa bado wanampampa support, sasa ikabidi aliamshie kwangu seriously kwa sababu alinichukulia mimi kama chanzo cha yeye kukosa msaada na mara nyingi akawa anatishia kujitoa kwenye ile project!!
Asubuhi moja mdada ikabidi ashuke tuu, aongee na mimi vizuri ili mambo yaende, nikaamua kukaza ili kazi iende na tuimalize kwa wakati.
Hakupenda nilivyomkazia, kuna wakati nilikuwa namaliza mapema nampiga tough kimtindo!!
Wakati tunakaribia mwisho hee, mrembo akaanza kuniletea kashfa sikupenda ile hali, nilimjia juu sana kidogo nimkate vibao mbele za watu! bahati nzuri mratibu alikuwa karibu na ndiye aliyeokoa kile kisanga.
Kazi ikaisha kila mtu akasambaa kivyake!!
Sasa leo mchana nakutana na yule mrembo ofisini afu ndiyo mkuu wa idara (sijui kapandishwa lini cheo)...
Afu kuna kaworkshop kengine tena kanguvu kuliko kale ka kwanza na huyu binti kwa namna moja au nyingine anashiriki kwenye kuratibu!!
Sijui itakuwaje yaani huyu binti sasa anapower regardless kazi yake alikuwa anafanya kivivu sana!!
Nimeshindwa ku define hali yake juu yangu kwa sababu hatujaongea sana zaidi ya salamu na mambo ya kazi.
Hapa wakuu mnashauri nini? niuchune tu, au nimwombe msamaha kwa kujaribu kumpiga? ili mambo yaende sawa...
Najua nilimkosea kwa kushindwa kutuliza hasira zangu kwake!! Nahisi anaweza kunisumbua na nikatemana na kazi yenyewe, japokuwa ni deal la maana...
Nimejikuta napata wakati mgumu sana kukutana na mtu ambaye niliwahi kumsumbua hata kujaribu kumtishia kwa namna moja...
Kuna dada mmoja, ambaye tulifahamiana kwenye workshop moja hivi mwanzoni mwa mwaka huu, ilikuwa inafanyikia mkoa wa Tanga nilikuwa nae kiukundi kimoja katika kazi na kwa bahati nzuri mimi na huyu dada tulikuwa tunatoka mkoa mmoja.
Offcoz ile kazi ilikuwa ngumu kidogo na ilihitaji akili na nguvu kuifanya!! Sasa huyu binti akawa anatega sana, na unakuta kazi zote nafanya mimi, ni binti mrembo! na kwa kweli anajua kutega kazi. Workshop ilikuwa ni ya muda mrefu kidogo, almost 4weeks!.
Kazi ikaendelea but ilifika mahali ikabidi nimbane binti ili afanye kazi, na nikajaribu kumlimit hata kwenye maswala ya muda, muda wa kula na muda wa mapumziko.
Hali ilimwia ngumu kidogo na ilifika kipindi akaamua kutofautiana na misimamo yangu katika kile kikundi chetu! akawa anawaambia members wengine kuwa mimi namdharau sana namwona legelege!! Mrembo kila akiniona lazima aongee maneno ya kulalamika na kusema namwonea, nilianza kumdharau kimtindo so kuna baadhi ya sehemu ilibidi nimpuuze na nilijaribu kuwaambia baadhi ya wadau pale wasimsaport, kuna kazi nyingine ni za serikali lakini ni ngumu.
Kwenye hiyo workshop tulikuwa tunalipwa 80,000/= per day malazi na meals excluded. Kadri siku zilovyokuwa zinaenda kazi ikawa inaongezeka ugumu, hapo ilibidi watu tuwe serious kweli kweli, kulala saa 5 usiku kuamka saa kumi na moja asubuhi.
Sasa msaada kwa huyu mrembo ukazidi kupungua kwa wale members wachache waliokuwa bado wanampampa support, sasa ikabidi aliamshie kwangu seriously kwa sababu alinichukulia mimi kama chanzo cha yeye kukosa msaada na mara nyingi akawa anatishia kujitoa kwenye ile project!!
Asubuhi moja mdada ikabidi ashuke tuu, aongee na mimi vizuri ili mambo yaende, nikaamua kukaza ili kazi iende na tuimalize kwa wakati.
Hakupenda nilivyomkazia, kuna wakati nilikuwa namaliza mapema nampiga tough kimtindo!!
Wakati tunakaribia mwisho hee, mrembo akaanza kuniletea kashfa sikupenda ile hali, nilimjia juu sana kidogo nimkate vibao mbele za watu! bahati nzuri mratibu alikuwa karibu na ndiye aliyeokoa kile kisanga.
Kazi ikaisha kila mtu akasambaa kivyake!!
Sasa leo mchana nakutana na yule mrembo ofisini afu ndiyo mkuu wa idara (sijui kapandishwa lini cheo)...
Afu kuna kaworkshop kengine tena kanguvu kuliko kale ka kwanza na huyu binti kwa namna moja au nyingine anashiriki kwenye kuratibu!!
Sijui itakuwaje yaani huyu binti sasa anapower regardless kazi yake alikuwa anafanya kivivu sana!!
Nimeshindwa ku define hali yake juu yangu kwa sababu hatujaongea sana zaidi ya salamu na mambo ya kazi.
Hapa wakuu mnashauri nini? niuchune tu, au nimwombe msamaha kwa kujaribu kumpiga? ili mambo yaende sawa...
Najua nilimkosea kwa kushindwa kutuliza hasira zangu kwake!! Nahisi anaweza kunisumbua na nikatemana na kazi yenyewe, japokuwa ni deal la maana...