Nilimfumania, sasa ananitishia kuniua

Nilimfumania, sasa ananitishia kuniua

elyza

Senior Member
Joined
Oct 9, 2016
Posts
155
Reaction score
327
Pole na shughuli za siku wakuu.

Nilikuwa na mchumba ambaye tumedumu nae kwa miezi tisa. Pia uchumba wetu ulishakuwa wazi kwa wazazi wa pande zote mbili, japo bado hakikuwa kimefanyika chochote katika kuhalalisha mahusiano yetu.

Mwezi uliopita nilikwenda nyumbani kwa mchumba wangu bila kumtaarifu, nilikuta mlango umerudishiwa tu, nikataka kuingia mama mwenye nyumba akanifanyia ishara ya kuniita kwa mkono nikaenda kumsikiliza.

Alichoniambia eti nirudi nyumbani nisiingie kwani mpenzi wangu hajisikii vizuri na ameagiza mtu yoyote akija asiingie. Nikatafakari nikaona kama mtu hajisikii vizuri kwanini nisijue shida yake.

Nikamuitia yule mama na kumshukuru kwa taarifa lakini nikaingia ndani, kweli sebuleni hapakuwa na mtu.

Nikasukuma mlango wa chumbani na kuingia. Sikuamini macho yangu nilichokiona inauma sana nilimkuta mpenzi wangu akifanya mapenzi na binti wa mama mwenye nyumba wake.

Niliona hakuna haja ya kugombana kwakuwa hakuwa mume wangu nilichomwambia aendelee na huyo mimi basi tena.

Siku iliyofuata alikuja home alipogonga geti nilichungulia nilipotambua kuwa ni yeye nilimuuliza anasemaje.

Alinijibu kwa dharau kwamba amekuja kunipa taarifa kuwa yule niliyemkuta nae ndiye chaguo lake mimi sina hadhi ya kuwa nae sikuwa na maneno mengi nilimjibu kifupi asante kisha nikafunga geti nakurudi ndani.

Nilipata uchungu sana nililia hata kesho yake sikuweza kwenda kazini
Nikaamua kumtoa moyoni na kwakweli nilimtoa kabisa, nilichukua zawadi zote alizonipa nikamtuma mdada wa kazi ampelekee. Nikajua ndo mwisho wa mawasiliano.

Baada ya wiki kupita akajirudisha nimekataa na simtaki sasa anatishia kuniua nimeripoti polisi na nimepewa RB.

Je, hapo mimi nina makosa?
 
Jamani huyo mwanaume wako si mzima inawezekana kati ya wale wanne yeye ndio mmoja wapo.Haiingii akilini mtu ufumaniwe halafu wewe tena utake kuua.
Ila na wamama sisi tuna tabia mbaya sana sasa huyo mama mwenye nyumba anabariki kabisa mwanae kubanduliwa humo humo ndani ilihali anajua mkaka ana mchumba mbali na hilo yeye ndio anakuwa mlinzi wao aiseeee kweli ni shidaaa
 
Kweli ww ulikuwa mchumba mwema yaani wasichana wengi yaani 92% wanakuwa na washika dau wa pembeni lakini ww ulimthamini sana mpenzi wako ila yy hakujitambua lakini kuna uwezekano mkubwa Mama mwenye nyumba alimpigia debe mwanae ili awe naye kuja kwako mama kilimuuma wakati yy anamwanae!
 
Jamani huyo mwanaume wako si mzima inawezekana kati ya wale wanne yeye ndio mmoja wapo.Haiingii akilini mtu ufumaniwe halafu wewe tena utake kuua.
Ila na wamama sisi tuna tabia mbaya sana sasa huyo mama mwenye nyumba anabariki kabisa mwanae kubanduliwa humo humo ndani ilihali anajua mkaka ana mchumba mbali na hilo yeye ndio anakuwa mlinzi wao aiseeee kweli ni shidaaa

Struggle for the fittest, only the strong will survive
 
Pole na shughuli za siku wakuu.

Nilikuwa na mchumba ambaye tumedumu nae kwa miezi tisa.

Pia uchumba wetu ulishakuwa wazi kwa wazazi wa pande zote mbili,
japo bado hakikuwa kimefanyika chochote ktk kuhalalisha mahusiano yetu.

Mwezi uliopita nilikwenda nyumbani kwa mchumba wangu bila kumtaarifu, nilikuta mlango umerudishiwa tu, nikataka kuingia mama mwenye nyumba akanifanyia ishara ya kuniita kwa mkono nikaenda kumsikiliza.

Alichoniambia et nirudi nyumban nisiingie kwani mpenz wangu hajisikii vizuri na ameagiza mtu yoyote akija asiingie.
Nikatafakari nikaona kama mtu hajisikii vizuri kwann nisijue shida yake.

Nikamuitia yule mama na kumshukuru kwa taarifa lkn nikaingia ndan, kweli sebuleni hapakuwa na mtu.

Nikasukuma mlango wa chumbani nakuingia. Sikuamini macho yangu nilichokiona....inauma sana ..nilimkuta mpnz wangu akifanya mapenzi na binti wa mama mwenye nyumba wake.

Niliona hakuna haja ya kugombana kwakuwa hakuwa mume wangu..nilichomwambia aendelee na huyo mm basi tena.

Siku iliyofuata alikuja home alipogonga geti nilichungulia nilipotambua kuwa niyeye nilimuuliza anasemaje.

Alinijibu kwa dharau kwamba amekuja kunipa taarifa kuwa yule niliyemkuta nae ndiye chaguo lake mm sina hadhi ya kuwa nae..sikuwa na maneno mengi nilimjibu kifupi Asante kisha nikafunga geti nakurudi ndani.

Nilipata uchungu sana nililia hata kesho yake sikuweza kwenda kazin..
Nikaamua kumtoa moyoni na kwakweli nilimtoa kbsa..nilichukua zawad zote alizonipa nikamtuma mdada wa kazi ampelekee. Nikajua ndo mwisho wa mawasiliano ..

Baada ya WK kupita akajirudisha nimekataa na simtaki sasa anatishia kuniua..nimeripoti polisi na nimepewa rb.

Je hapo mm Nina makosa?

Yaani miezi tisa ushamwita mchumba na kumtambulisha kwa wazazi?!
Hapo lazima jamaa alikuingia kwa gia ya kukuoa fasta nawe ukaingia mkenge.

Chukua hilo kama funzo na achana nae huyo hakufai kabisa
 
Jamani huyo mwanaume wako si mzima inawezekana kati ya wale wanne yeye ndio mmoja wapo.Haiingii akilini mtu ufumaniwe halafu wewe tena utake kuua.
Ila na wamama sisi tuna tabia mbaya sana sasa huyo mama mwenye nyumba anabariki kabisa mwanae kubanduliwa humo humo ndani ilihali anajua mkaka ana mchumba mbali na hilo yeye ndio anakuwa mlinzi wao aiseeee kweli ni shidaaa
Yaani nilimdharau sana
 
Pole na shughuli za siku wakuu.

Nilikuwa na mchumba ambaye tumedumu nae kwa miezi tisa.

Pia uchumba wetu ulishakuwa wazi kwa wazazi wa pande zote mbili,
japo bado hakikuwa kimefanyika chochote ktk kuhalalisha mahusiano yetu.

Mwezi uliopita nilikwenda nyumbani kwa mchumba wangu bila kumtaarifu, nilikuta mlango umerudishiwa tu, nikataka kuingia mama mwenye nyumba akanifanyia ishara ya kuniita kwa mkono nikaenda kumsikiliza.

Alichoniambia et nirudi nyumban nisiingie kwani mpenz wangu hajisikii vizuri na ameagiza mtu yoyote akija asiingie.
Nikatafakari nikaona kama mtu hajisikii vizuri kwann nisijue shida yake.

Nikamuitia yule mama na kumshukuru kwa taarifa lkn nikaingia ndan, kweli sebuleni hapakuwa na mtu.

Nikasukuma mlango wa chumbani nakuingia. Sikuamini macho yangu nilichokiona....inauma sana ..nilimkuta mpnz wangu akifanya mapenzi na binti wa mama mwenye nyumba wake.

Niliona hakuna haja ya kugombana kwakuwa hakuwa mume wangu..nilichomwambia aendelee na huyo mm basi tena.

Siku iliyofuata alikuja home alipogonga geti nilichungulia nilipotambua kuwa niyeye nilimuuliza anasemaje.

Alinijibu kwa dharau kwamba amekuja kunipa taarifa kuwa yule niliyemkuta nae ndiye chaguo lake mm sina hadhi ya kuwa nae..sikuwa na maneno mengi nilimjibu kifupi Asante kisha nikafunga geti nakurudi ndani.

Nilipata uchungu sana nililia hata kesho yake sikuweza kwenda kazin..
Nikaamua kumtoa moyoni na kwakweli nilimtoa kbsa..nilichukua zawad zote alizonipa nikamtuma mdada wa kazi ampelekee. Nikajua ndo mwisho wa mawasiliano ..

Baada ya WK kupita akajirudisha nimekataa na simtaki sasa anatishia kuniua..nimeripoti polisi na nimepewa rb.

Je hapo mm Nina makosa?
Pole sana dada yangu haya ni mapito na yataisha.
Watu wengi huwa hawatambui thamani ya kupendwa ndiyo maana wanapopendwa huchukulia kawaida sana mpaka pale yule aliyempenda atakapoondoka.

Hakika huyu hakupendi, mm nilitegemea hata angekuomba msamaha na kujuta kwa kile alichokifanya ila akazidi kukuumiza.

Huyu ukimrudiana atakutesa sana na inavyoonekana ni tabia yake. Mwache aende mpendwa sabb wapo wenye upendo na wanaojua kujali.
Kumbuka kuna mwenzio humu alikuwa anapigwa lkn akawa anajipa moyo ipo siku atabadilika lkn kilichompata kinasikitisha sana.
Mwache aende zake na makengele yake
 
Dah dada una akili mno.... Safi sana dah.

Heko kabisa. Umefanya jambo la maana sana... Hivyo ulivyofanya ndio sawa kabisa.
 
pole mkuu huyo playboy achana nae bado huja mfuma na UKIMWI akwambie ukisema atakuzika!!!.
bora usepe tu.
 
Dude must have a hella game. Bangin' the daughter, her mama on the lookout? Can't beat that.

Anyway, elyza tuna group letu whats app tunakutana wahanga wa mapenzi kama wewe, tunashauriana na kufarijiana. Karibu.
 
Pole sana dada yangu haya ni mapito na yataisha.
Watu wengi huwa hawatambui thamani ya kupendwa ndiyo maana wanapopendwa huchukulia kawaida sana mpaka pale yule aliyempenda atakapoondoka.

Hakika huyu hakupendi, mm nilitegemea hata angekuomba msamaha na kujuta kwa kile alichokifanya ila akazidi kukuumiza.

Huyu ukimrudiana atakutesa sana na inavyoonekana ni tabia yake. Mwache aende mpendwa sabb wapo wenye upendo na wanaojua kujali.
Kumbuka kuna mwenzio humu alikuwa anapigwa lkn akawa anajipa moyo ipo siku atabadilika lkn kilichompata kinasikitisha sana.
Mwache aende zake na makengele yake
Asante mkuu kwa ushauri wako
 
Haya mama tafuta huyo wa peke yako......
Ushaambiwa mwanaume ni kama baba ntilie, mwiko mmoja vyungu vingi.

Jambo la msingi ungemuuliza tu " Honey mwiko umeuosha? "
Kama ndio nae uutumie zako na maisha yangeendelea.

Haya tafuta wa peke yako uone kama halija kuchwea
 
kuna uzoefu mmoja ambao nimekuwa naupata katika kesi kama hizi na siku zote huwa nawauliza na kuwashauri machache kadri ya mengi ambayo huwa ninayo.
kwanza je ukweli wa mioyo yao na hao wenzi wao ukoje? wasiangalie emotional zao na kufanya maamuzi yasiyokubaliana na matakwa yao.
kuna swli linawasumbua siku zote hivi watu watanifikiriaje siwataniona mimi ni mdhaifu? na hii ni kutokana kuwa wanawake wengi wanapenda kuishi maisha ya watu watawaonaje na si wao wanataka nini kwa wakati huo.
hivyo fanya maamuzi ya busara amua kizazi hiki wanaume walio wengi ni player angalia usichelewe ukaolewa na referee tena wakati mpira umeisha (nadhani umenielewa).
hivyo maamuzi yako ndio yafuate.
vigezo vya kuoana sio vigezo vyakuendelea kuishi hivyo kuwa makini pia na hilo download taarifa zake zaidi kisha fikiria upya kama unamwitaji na anakupenda.
lakini mwisho wa yote tazama na wewe umekosea wapi badala ya kupeleka lawama. swala la kuolewa sio dogo siku hizi ni vita na wakati mwingi linahitaji maombi zaidi kuliko unavyofikiria.
mchango huu unakutosha finginevyo ni pm
 
Back
Top Bottom