Nilim-cheat Mpenzi wangu in 2012

Nilim-cheat Mpenzi wangu in 2012

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
61,204
Reaction score
99,943
Mara saba nilimdanganya kuwa nina vikao vya ofisi na hivyo nitachelewa kurudi home, mara tatu nilimdanganya kuwa nasafiri kikazi ila kwa kweli nilikua kwenye hotel kadha wa kadha hapa hapa, mara mbili nilimdanganya kuwa naumwa na nahitaji kupumzika, hivyo nikabaki home na HG nikamtafuna wakati yeye akiwa kazini, mara tano nilimdanganya kuwa niko LUNCH kumbe nilitoka na Secretary wa Ofisi pale nanihii pale, mara nne nilimdanganya kuwa gari imeharibika wakati narudi toka Job kumbe nilikua na Binti wa Jirani tukila "RAHA", mara saba nilidanganya kuwa naenda sokoni na mdogo wake, kumbe tulichanganya na safari za gesti pia....

Mara kadhaa nilitoka na Rafiki yake mke wangu ambae ni Jirani yetu, sababu zilikua nyingi ikiwepo yeye (Jirani) kuja kuomba msaada wa gari nimempeleke Hospital but ukweli hakukua na ugonjwa wala mgonjwa zaidi ya kuishia Gesti/Hotel. Kuna katoto kashule kalikuja Likizo kwangu, ni ndugu wa mke wangu kwa Baba yake mdogo, nikawa natoka nako kimtindo, mara kibao nilijifanya nimechelewa kwenye foleni but ukweli nilikua kwenye mambo yangu, wengine sikukumbuki.

Nimejitahidi kuona mke wangu alini-cheat wapi sijaona hivyo nimeamua kutubu na kuomba msamaha kwa Jamii inisamehe na kunipokea mie mkosaji....Je wewe ulim-cheat Mpenzio? kwanini usitubu japo komoyomoyo tu na kubadilisha mwenendo wako? Mie nimetubu, jiunge na Mimi leo tuanze maisha mapya kwenye familia zetu, Heri ya mwaka Mpwa 2013. (Hainihusu mimi Elli) Jipime mwenyewe
 
ni vizuri kuwa hivyo ni moja kati ya watu wachache wasema kweli..
 
Kesho asubuhi wahi ANGAZA kwenda kucheck usalama wa afya yako...
Soma mistari ya mwisho, nimetoa angalizo kwa kujitolea mfano Mpwa ila sio mimi...ningekutolea mfano najua ungekua mkali sana ndio maana nikajitolea mfano mwenyewe...sio kitu halisia
 
Soma mistari ya mwisho, nimetoa angalizo kwa kujitolea mfano Mpwa ila sio mimi...ningekutolea mfano najua ungekua mkali sana ndio maana nikajitolea mfano mwenyewe...sio kitu halisia

Najua sio wewe mkuu na ndio maana hujaona mahali nimeku-mention nia ya ujumbe wangu ilikua umfikie yoyote alieishi hivyo kama ulivyotabanaisha.
 
Mpwa nimekugongea Ze Like fasta fasta, haya tuyatengeneze maisha yetu, naona akina Dada wote wa hapa JF wameshalala mapema kabisa au labda wako viwanja
Najua sio wewe mkuu na ndio maana hujaona mahali nimeku-mention nia ya ujumbe wangu ilikua umfikie yoyote alieishi hivyo kama ulivyotabanaisha.
 
Mpwa nimekugongea Ze Like fasta fasta, haya tuyatengeneze maisha yetu, naona akina Dada wote wa hapa JF wameshalala mapema kabisa au labda wako viwanja

Hahah siku ya leo kila mtu anatambika kivyake...wengine nyumba za ibada na wengine wapo viwanja
 
Hahah siku ya leo kila mtu anatambika kivyake...wengine nyumba za ibada na wengine wapo viwanja

Na mie niko home, nimeshafanya ibada na mke wangu, tumetubu na kusameheana yaliyopita tunaangalia yajayo
 
Hongera kwa kutubu na kuuanza mwaka vizuri. Lakini umenipa mashaka ulipoamua kucheat mpaka kwa housegel na rafiki wa mke wako! Hapo ulikuwa umefikia level ya juu kabisa ya dharau kwa mkeo.
Kitu muhimu ni vyema usirudie tena yale uliyoyatubia leo.
 
Mpwa nimecheka sana, dhambi haina level ya juu wala ya chini, ndogo wala kubwa hubaki kuwa dhambi tu....hata hivyo sio mimi bhana ni changamoto kwetu sote
Hongera kwa kutubu na kuuanza mwaka vizuri. Lakini umenipa mashaka ulipoamua kucheat mpaka kwa housegel na rafiki wa mke wako! Hapo ulikuwa umefikia level ya juu kabisa ya dharau kwa mkeo.
Kitu muhimu ni vyema usirudie tena yale uliyoyatubia leo.
 
hivi unafunga zipu ya suruali wewe? Unatembea mpaka na ndugu wa mkeo? Rafiki wa mkeo? Hausigirl? Loh pole maalum imuendee mkeo......

Ndo maana wanawake siku hizi wanagawa sana huko nje, maana waume zao loh ......

Anyway napita tu, heri ya mwaka mpya....

Watembezaji wotw nawatakia mtembezo mwema...

nimesahau kumbe haikuhusu wewe.....mweh
 
Ya mkeo huwezi yajua hadi akuambie mwenyewe. Sasa ndugu, una kidaftari cha kuwekea hizi hesabu za cheatibgs? Manake wakati wa kuvuna ulichopanda utahitaji kukumbuka na huenda ukawa umedata ukakwama!
 
Back
Top Bottom