Nilikuwa nawatetea sana singo mama lakini kwa hili la huyu mama limenikata maini kabisa

Hata ukiwa nyumbani kwake bado haiathiri chochote kwa mwanaume tena ndio itaonyesha ukomavu wake wa akili na upeo wa maisha sote tunapita vitu kama misiba sio vya kuleta kupishana kauli
Sasa km mwanaume hataki iweje mwanamke akupangie cha kufanya yeye abebe maiti ya mwanae akazike kiislam na msiba uwekwe kwa huyo baba wa mtoto sio nyumbani kwa mumewe kwanza kuoa single mama ni ujinga kwani umekosa wanawake ambao hawana watoto mpk ukaoe single maza!!
 
Sasa km mwanaume hataki iweje mwanamke akupangie cha kufanya yeye abebe maiti ya mwanae akazike kiislam na msiba uwekwe kwa huyo baba wa mtoto sio nyumbani kwa mumewe kwanza kuoa single mama ni ujinga kwani umekosa wanawake ambao hawana watoto mpk ukaoe single maza!!
Yaani nakuunga mkono hapo tu kwenye kutooa singo maza lakini haya mengine kama mwanamke kataka mwanae azikwe kiislamu na sio mtoto wako kwann usimpe nafasi akamaliza maziko kwani itapunguza nn kwenye nyumba yako
 
Yaani nakuunga mkono hapo tu kwenye kutooa singo maza lakini haya mengine kama mwanamke kataka mwanae azikwe kiislamu na sio mtoto wako kwann usimpe nafasi akamaliza maziko kwani itapunguza nn kwenye nyumba yako
Haipunguzi chochote ila km jamaa aliweza kulea mtoto toka ana miez 6 mpk hapo alipofikia huyo mama kwanini asingesema ww ni mkristo huyo mtoto ni muislam haitakiwi kumtunza leo hii kafa ndio anajua mtoto ni muislamu? Ningekua ni mm ningemwambia huyo mama mtt kua nenda kazike mwanao kiislam ila sitaki kukuona nyumbani kwangu tena wala msiba kua kwangu
 
HUyu mwanamke aliolewa akiwa na mtoto mwenye umri wa miezi 6 na jamaa mkatoriki

Mtoto kafariki akiwa mkubwa,huyo mwanamke anataka mtoto azikwe kwa imani ya kiislamu

Ebu fikiria nyumbani kwako kufanyike ibada ya imani tofauti na yako,wewe baba wa familia utajisikiaje

Jamaa kaamua kwenda polisi kuzuia maziko.

--

View attachment 2665378

Taharuki kubwa imeibuka huko Mkoani Mwanza baada ya mwili wa marehemu kufikishwa msikitini kuswaliwa kwa maziko lakini baba wa marehemu akazuia asizikwe.

Kwa mujibu wa maelezo ya mama wa marehemu huyo, kabla ya kuolewa mwanaume huyo alimkuta akiwa na mtoto wa miezi sita na kwamba mtoto huyo ana baba yake mwingine ambaye ni Mchaga na ni Muislamu.

Mara baada ya kufariki kwa mtoto huyo, mwanaume huyo ameibuka na kusema kwamba hataki mtoto huyo azikwe kiislamu huku mama wa mtoto akiweka wazi kwamba mtoto huyo siyo mkristo na hivyo anaomba mtoto wake azikwe kwa kufuata taratibu za dini yake ambayo ni dini ya kiislamu.

Aidha, kutokana na mvutano huo, Jeshi la Polisi limelazimika kuingilia kati na kuahirisha mazishi hayo mpaka pale mwanaume huyo aliyedai kwamba mtoto huyo asizikwe kiislamu ataporejea.
Dah Wewe hapo umeona tatizo wapi mpaka unaanzisha Uzi? Mtoto sio wake hivyo mtoto anafuata dini ya babaake mzazi na sio mlezi. Kumbe shida sio mwanamke shida mwanaume huyo ambaye ameshwindwa waza kiuharisia... Au wewe ambaye uwenda haujaleta maelezo halisi. Ila kama maelezo ndo hayo Basi Hadi wewe Akili mgando
 
HUyu mwanamke aliolewa akiwa na mtoto mwenye umri wa miezi 6 na jamaa mkatoriki

Mtoto kafariki akiwa mkubwa,huyo mwanamke anataka mtoto azikwe kwa imani ya kiislamu

Ebu fikiria nyumbani kwako kufanyike ibada ya imani tofauti na yako,wewe baba wa familia utajisikiaje

Jamaa kaamua kwenda polisi kuzuia maziko.

--

View attachment 2665378

Taharuki kubwa imeibuka huko Mkoani Mwanza baada ya mwili wa marehemu kufikishwa msikitini kuswaliwa kwa maziko lakini baba wa marehemu akazuia asizikwe.

Kwa mujibu wa maelezo ya mama wa marehemu huyo, kabla ya kuolewa mwanaume huyo alimkuta akiwa na mtoto wa miezi sita na kwamba mtoto huyo ana baba yake mwingine ambaye ni Mchaga na ni Muislamu.

Mara baada ya kufariki kwa mtoto huyo, mwanaume huyo ameibuka na kusema kwamba hataki mtoto huyo azikwe kiislamu huku mama wa mtoto akiweka wazi kwamba mtoto huyo siyo mkristo na hivyo anaomba mtoto wake azikwe kwa kufuata taratibu za dini yake ambayo ni dini ya kiislamu.

Aidha, kutokana na mvutano huo, Jeshi la Polisi limelazimika kuingilia kati na kuahirisha mazishi hayo mpaka pale mwanaume huyo aliyedai kwamba mtoto huyo asizikwe kiislamu ataporejea.
Wote ni wapumbavu kwanini wasiruhusu tu azikwe kwa imani yoyote wakati ni maiti!!!!
 
Dah Wewe hapo umeona tatizo wapi mpaka unaanzisha Uzi? Mtoto sio wake hivyo mtoto anafuata dini ya babaake mzazi na sio mlezi. Kumbe shida sio mwanamke shida mwanaume huyo ambaye ameshwindwa waza kiuharisia... Au wewe ambaye uwenda haujaleta maelezo halisi. Ila kama maelezo ndo hayo Basi Hadi wewe Akili mgando
Umeolewa wewe na mwanao mkatunzwa miaka yote hyo na mkatoriki leo mnajifanya mmekuwa waislamu,kama mnataka kuzikana kiislamu nendeni kwenu huko hapa ni kwa mkatoriki
 
Kwahiyo jamaa aliwapigia simu polisi na kuwaagiza waende msikitini kuzuia mazishi? Kwa polisi Hawa ninaowajua Mimi hapo itakuwa katembeza mpunga mrefu sana, alafu huyo jamaa hajielewi maana mtoto sio wake ni wa mwanamme mwenzake ambaye ni muislamu sasa anampangiaje namna ya kumzika?
Akazikwe kwa mwanaume ambaye ni baba wa mtoto shida iko wapi sasa
 
Umeolewa wewe na mwanao mkatunzwa miaka yote hyo na mkatoriki leo mnajifanya mmekuwa waislamu,kama mnataka kuzikana kiislamu nendeni kwenu huko hapa ni kwa mkatoriki
Mtoto wake? Malezi hayaathiri dini halali ya mtoto... Kwa Akili hizi Acha wabunge watuone wajinga kwenye mikataba finyu
 
Dadeki hiyo ni nguvu ya pesa..
Jamaa sio baba wa mtoto ila anamamlaka juu ya mtoto asie wake, na mwamba hayupo jeshi la polisi linamsubiri aje atoe tamko alooo.

Mchaga anaporwa mtoto hivihivi aisee , ama kweli yani mwanao anaweza badilishwa hadi ubini kabisa.

Na wewe mleta uzi huyo singo maza ana kosa gani?? Mbona yeye ndio kaonewa sasa kwanini unamshutumu??
 
Kwahiyo jamaa aliwapigia simu polisi na kuwaagiza waende msikitini kuzuia mazishi? Kwa polisi Hawa ninaowajua Mimi hapo itakuwa katembeza mpunga mrefu sana, alafu huyo jamaa hajielewi maana mtoto sio wake ni wa mwanamme mwenzake ambaye ni muislamu sasa anampangiaje namna ya kumzika?
Waende wakafanyie ayo mazishi kwa baba yake muislamu.Watoke kwa uyo jamaa
 
Baba mzazi wa mtoto anasemaje?
Asichokijua mzazi wa kufikia ni kwamba mbinguni hauendi kwa kuzikwa kikristo. Ni maisha kabla ya kufa ndiyo yanayoamua utakakokwenda. Ingekuwa arusi sawa.Ila siyo jinsi ulivyozikwa .Mungu huwa hapokei roho ya mtu aliyekufa kabla ya kutubu.So mashindano ya hivyo hayana maana yoyote kabisa
Acha kumsemea Mungu. Eti hapokei roho iliyo...
Dini ni ujinga kabisa
 
Back
Top Bottom