Nilifanya Mapenzi Na Maiti 20 Nitajirike – sehemu ya 1

MziziMkavu ulipo huko njoo na huku tunakuhitaji kwa muendelezo wa simulizi.
 
Nilifanya Mapenzi na Maiti 20 Nitajirike – 9


ILIPOISHIA SEHEMU YA NANE


Tulikwenda mpaka tulipofika sehemu iliyokuwa imeunganishwa na barabara moja ya vumbi, tukaingia nayo, tulikwenda zaidi mpaka tukaanza kuingia sehemu iliyokuwa na miti mingi.

Sikuwa na uhakika kama huko kulikuwa na watu walikuwa wakiishi, kulikuwa kimya sana, hatukusimama, tuliendelea kuifuata barabara hiyo ya vumbi mpaka kufika sehemu ambayo barabara ilifika mwisho, sasa tukaanza kuelekea katika njia ambayo hakukuwa na njia rasmi, nikaanza kushikwa na hofu, nikahisi kuna hatari mbele yangu! Mzee Hassani hakutaka kuzungumza tena, naye alikuwa kimya, macho yake yalikuwa mbele, hakuonekana kuwa na hofu hata kidogo, ila kwangu, nilitamani nirudi. Eti huko ndipo kulipokuwa na utajiri! Nikasubiri nione nini kingetokea.

MWAGIKA NAYO HAPA…

Tuliendelea na safari mpaka tulipofika sehemu fulani ambayo ilikuwa na miti mingi na kwa mbali kulikuwa na nyumba ndogo ya udongo. Nilibaki na mshangao, sikuamini sehemu kama hiyo kungekuwa na mtu anaishi, niliogopa, wakati mwingine nilihisi kama nilikuwa kwenye sehemu mbaya, yenye kutisha ambayo ingenifanya nitekwe na watu wenye roho mbaya.

“Ila si natafuta utajiri, haina jinsi..” nilijisemea.

Mzee Mudi akaniambia niteremke na tuanze kwenda kule kwenye kile kijumba, wakati natembea, mwili wangu ulikuwa unatetemeka mno na wakati mwingine nilihisi ningeweza hata kuanguka.

“Mbona unatetemeka?” aliniuliza.

“Hakuna kitu.”

“Kweli?”

“Ndiyo!”

Japokuwa nilimficha lakini nilikuwa na uhakika kwamba alinigundua. Tuliendelea kusogea mbele mpaka tulipokifikia kijumba kile ambapo akaniambia kwamba hatukutakiwa kuingia moja kwa moja bali tulitakiwa kusubiri nje, tukafanya hivyo.

Baada ya dakika kama mbili, tukasikia sauti ndani ikitukaribisha, tukasimama na kuanza kuingia ndani. Huko, tulimkuta mzee mmoja, kwa kumwangalia harakaharaka, alikuwa na miaka kama sabini ila alikuwa amechoka sana kimaisha.

Kichwa changu kikaanza kujiuliza, je, mzee yule angeweza kunifanya niwe tajiri kama nilivyotaka? Wakati najiuliza hayo, nikashangaa mzee yule akisimama na kunishika kichwa changu.

“Usijiulize swali hilo, nitakufanya kuwa tajiri mkubwa sana,” aliniambia huku akiwa amenikazia macho.

Kwanza nikashtuka, ilikuwaje ajue kile nilichokuwa nikijiuliza, mpaka hapo, nikajua kwamba huyo mzee alikuwa na nguvu za ziada. Nikatulia na kumwangalia usoni. Kwa jinsi chumba kile kilivyokuwa, kiliniogopesha mno, kulikuwa na tunguli kila kona, harufu mbaya ambayo ilinifanya kutamani kuziba pua zangu.

“Unataka kuwa tajiri?” aliniuliza mzee huyo.

“Ndiyo!”

“Una uhakika?” aliniuliza.

“Ndiyo mzee!”

“Utayaweza masharti?” aliniuliza.

“Nitayaweza tu..”

Mzee yule akasimama na kuanza kuimba nyimbo ambazo sikuwa nikizielewa kabisa. Hakuishia kuimba tu bali akaanza kucheza pia. Nilibaki nikimwangalia, sikutaka kuzungumza kitu chochote kile kwani hata nguvu ya kufanya hivyo sikuwa nayo.

Akanisogelea na kunipaka unga fulani machoni mwangu. Ulikuwa na rangi nyeusi, alipoyapaka macho yangu, nikaanza kuhisi hali ya tofauti moyoni mwangu, furaha kubwa ambayo sikuwahi kuipata maisha yangu yote.

“Unajisikiaje?” aliniuliza.

“Najisikia vizuri….”

“Unahitaji utajiri wa aina gani? Wa kuku na mahindi au wa milele?” aliniuliza swali ambalo sikuwa nikilijua kabisa.

“Sijajua upo vipi!”

Mzee Mudi ndiye akachukua nafasi hiyo na kuanza kuniambia tofauti ya utajiri hiyo aliyoniambia mzee huyo. Utajiri wa kuku ulikuwa ni kwamba kuku anatupiwa mahindi chini, anaanza kula, kama akila mahindi matano, basi utajiri wako utakuwa ni wa miaka mitano, kama akila mahindi ishirini, basi utajiri wako utakuwa wa miaka ishirini, baada ya hapo unafilisika na kufa.

“Hapana huo siupendi!” nilimwambia mzee Mudi.

“Kwa nini? Huo ndiyo mzuri!”

“Mimi nautaka huo mwingine.”

“Unaujua upo vipi?”

“Sijui, ila nautaka huohuo!” nilimwambia.

Utajiri niliosema kwamba niliutaka ulikuwa ni wa masharti makubwa. Niliambiwa hilo lakini nikasema kwamba nautaka huohuo na kama ni masharti nitayafanya yote lakini si kukubali ule wa mwanzo wa kuwa tajiri kwa kipindi fulani kisha kufa.

“Huu una masharti makubwa mawili,” aliniambia mganga.

“Yapi?”

“Moja, unatakiwa kuwaua wazazi wako wote wawili,” aliniambia huku akikishika kitunguli kidogo kilichokuwa pembeni yake.

“Kuwaua wazazi wangu?”

“Ndiyo!”

“Na sharti jingine?” niliuliza huku nikionekana kuchanganyikiwa.”

“Kufanya mapenzi na maiti ishirini..” aliniambia.

****

Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatilia kesho hapa kujua kitakachoendelea katika sehemu ya 10
 
Nilifanya Mapenzi na Maiti 20 Nitajirike – 8


ILIPOISHIA SEHEMU YA SABA


Wakati nikijiuliza hayo yote, mwanaume huyo, hata kabla ya kuzungumza nami, akatoa tabasamu pana usoni mwake, tabasamu lililoonyesha matumaini makubwa kwamba nisiwe na wasiwasi kwani tayari nilipata nilichokitaka.

“Naitwa bwana Hassani Mudi…” alijitambulisha huku akiniangalia kwa uso wenye tabasamu hilo pana.

“Naitwa Zakia…” nilimwambia, na mimi nikatoa tabasamu pana vilevile.

MWAGIKA NAYO HAPA…

Dickson akaanza kuniambia kwamba huyo ndiye alikuwa mtu aliyeniambia kwamba ningepata utajiri kupitia yeye, nilipomwangalia, bado nilikuwa na maswali mengi ambayo yote hayo hayakuwa na majibu yoyote yale.

Huyo mzee akaniambia niende naye pembeni kwani suala ambalo nililitaka halikuwa la kulizungumzia juujuu, ilitakiwa tutulie sehemu na aniambie kila kitu, nikakubaliana naye hivyo Dickson kutulia pembeni akitusubiri.

“Kweli unataka kuwa tajiri?” lilikuwa swali lake la kwanza kuniuliza.

“Ndiyo!” nilimjibu huku nikionekana kumaanisha nilichomwambia.

“Kweli?” aliniuliza.

“Ndiyo!”
“Sidhani kama unataka utajiri…” aliniambia.

“Kweli tena, nataka kuwa tajiri…” nilimwambia kwa sauti yenye msisitizo kabisa.

“Zakia, huna moyo, huna moyo, unaonekana tu…”

“Moyo ninao, nipo tayari kwa lolote lile.”

Niliposema hivyo, yule mzee akaanza kucheka sana, sikujua alikuwa akicheka nini, sijui kama alifurahishwa na jibu langu au la. Nilibaki nikimwangalia kwa mshangao, yeye mwenye aligundua kwamba nilikuwa nikijiuliza mengi kuhusu kicheko kile.

“Eti una moyo! Moyo gani na wakati unaogopa hata mende?” aliniuliza.

“Siogopi mende…nimetoka Morogoro mpaka hapa kwa ajili ya kutafuta utajiri tu, jua kwamba nina kiu ya kuwa tajiri, nipo tayari kufanya lolote ili nipate huo utajiri,” nilimwambia.

“Hata kuua?” aliniuliza.

“Sidhani, ila nikiambiwa kwamba nikimuua huyu napata utajiri, nitaua tu, sitokuwa na budi,” nilimwambia.

Nilichokuwa nikikiongea, nilimaanisha kutoka moyoni mwangu, kwa wakati huo nilikuwa tayari kwa lolote lile, kiu kubwa ya kuwa tajiri ilikuwa imenikamata. Mzee Hassani akaniambia kwamba jioni ya siku hiyo angenifuata hivyo nijiandae kwani kuna sehemu nilitakiwa kwenda naye, hilo halikuwa tatizo, nikakubaliana naye, akazungumza kidogo na Dickson kisha kuondoka, ndiyo kwanza muda huo ilikuwa saa saba mchana.

Aliniacha na mawazo tele, kichwa changu kilivurugika kabisa, wakati mwingine nilikuwa namuamini huyo mzee kwamba angenifanya kuwa tajiri mkubwa lakini wakati mwingine nilikuwa na wasiwasi kwamba asingeweza kufanya hivyo.

Kama kweli yeye alikuwa akitoa utajiri, kwa nini yeye mwenyewe hakuwa tajiri? Kama alikuwa akitoa utajiri, kwa nini Dickson hakuwa tajiri na wakati alikuwa rafiki wake wa karibu? Kila nilichojiuliza, nikawa na uhakika kwamba inawezekana mzee huyo alikuwa muongo.

“Dickson…unamuamini kweli huyu mzee?” nilimuuliza Dickson.

“Ndiyo!”

“Kweli atanisaidia?”

“Sana tu…kuna marafiki zangu kama watano, kawasaidia na sasa hivi ni matajiri wakubwa hapa mjini,” aliniambia.

“Sasa kama yeye anatoa utajiri, kwa nini na wewe asikupe? Au hutaji kuwa tajiri?” nilimtupia swali.

“Nataka!”

“Sasa kwa nini hujamwambia akupe?”

“Basi tu, nataka utajiri ule wa kuutafuta kwa nguvu zangu ili baadaye niwe na ushuhuda jinsi nilivyosota,” aliniambia huku macho yake yakionekana kuwa na jambo lililojificha.

Sikutaka kujali sana, nilichokuwa nikikiangalia ni maisha yangu tu kwani kwenye ridhiki za kuwa na maisha mazuri, Mungu aliwapa wale waliokuwa na kiu kubwa kama niliyokuwa nayo kipindi hicho.

Basi baada ya saa kadhaa, mzee Hassani akarudi mahali hapo na kukutana naye. Akanichukua na kuanza kuondoka naye mahali hapo. Kumbuka kwamba kwa kipindi chote tangu nifike Dar es Salaam sikuwa nimetoka ndani ya kituo kile, hivyo kutoka humo ndipo nikaanza kuona mazingira halisi ya jiji hilo.

Lilikuwa zuri, lililopendeza machoni mwangu.

Mzee Hassani alifika na gari lake na kulipaki nje. Tulipotoka, tukapanda na kisha kuondoka, tulipoelekea kwa kipindi hicho sikuwa nikipafahamu ila kwa sasa, ninapajua mno, palikuwa ni Bunju.

Njiani tulikuwa tukizungumza mambo mengi, katika kila sentensi aliyoongea ilionyesha alikuwa miongoni mwa watu waliojiamini kwa kila walichokuwa wakikifanya. Sikutakiwa kuwa na hofu hata kidogo.

Tulikwenda mpaka tulipofika sehemu iliyokuwa imeunganishwa na barabara moja ya vumbi, tukaingia nayo, tulikwenda zaidi mpaka tukaanza kuingia sehemu iliyokuwa na miti mingi.

Sikuwa na uhakika kama huko kulikuwa na watu walikuwa wakiishi, kulikuwa kimya sana, hatukusimama, tuliendelea kuifuata barabara hiyo ya vumbi mpaka kufika sehemu ambayo barabara ilifika mwisho, sasa tukaanza kuelekea katika njia ambayo hakukuwa na njia rasmi, nikaanza kushikwa na hofu, nikahisi kuna hatari mbele yangu! Mzee Hassani hakutaka kuzungumza tena, naye alikuwa kimya, macho yake yalikuwa mbele, hakuonekana kuwa na hofu hata kidogo, ila kwangu, nilitamani nirudi. Eti huko ndipo kulipokuwa na utajiri! Nikasubiri nione nini kingetokea.

****

Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatilia kesho hapa kujua kitakachoendelea katika sehemu ya TISA.
I'm waiting... for the next
 
Nilifanya Mapenzi na Maiti 20 Nitajirike – 9


ILIPOISHIA SEHEMU YA NANE


Tulikwenda mpaka tulipofika sehemu iliyokuwa imeunganishwa na barabara moja ya vumbi, tukaingia nayo, tulikwenda zaidi mpaka tukaanza kuingia sehemu iliyokuwa na miti mingi.

Sikuwa na uhakika kama huko kulikuwa na watu walikuwa wakiishi, kulikuwa kimya sana, hatukusimama, tuliendelea kuifuata barabara hiyo ya vumbi mpaka kufika sehemu ambayo barabara ilifika mwisho, sasa tukaanza kuelekea katika njia ambayo hakukuwa na njia rasmi, nikaanza kushikwa na hofu, nikahisi kuna hatari mbele yangu! Mzee Hassani hakutaka kuzungumza tena, naye alikuwa kimya, macho yake yalikuwa mbele, hakuonekana kuwa na hofu hata kidogo, ila kwangu, nilitamani nirudi. Eti huko ndipo kulipokuwa na utajiri! Nikasubiri nione nini kingetokea.

MWAGIKA NAYO HAPA…

Tuliendelea na safari mpaka tulipofika sehemu fulani ambayo ilikuwa na miti mingi na kwa mbali kulikuwa na nyumba ndogo ya udongo. Nilibaki na mshangao, sikuamini sehemu kama hiyo kungekuwa na mtu anaishi, niliogopa, wakati mwingine nilihisi kama nilikuwa kwenye sehemu mbaya, yenye kutisha ambayo ingenifanya nitekwe na watu wenye roho mbaya.

“Ila si natafuta utajiri, haina jinsi..” nilijisemea.

Mzee Mudi akaniambia niteremke na tuanze kwenda kule kwenye kile kijumba, wakati natembea, mwili wangu ulikuwa unatetemeka mno na wakati mwingine nilihisi ningeweza hata kuanguka.

“Mbona unatetemeka?” aliniuliza.

“Hakuna kitu.”

“Kweli?”

“Ndiyo!”

Japokuwa nilimficha lakini nilikuwa na uhakika kwamba alinigundua. Tuliendelea kusogea mbele mpaka tulipokifikia kijumba kile ambapo akaniambia kwamba hatukutakiwa kuingia moja kwa moja bali tulitakiwa kusubiri nje, tukafanya hivyo.

Baada ya dakika kama mbili, tukasikia sauti ndani ikitukaribisha, tukasimama na kuanza kuingia ndani. Huko, tulimkuta mzee mmoja, kwa kumwangalia harakaharaka, alikuwa na miaka kama sabini ila alikuwa amechoka sana kimaisha.

Kichwa changu kikaanza kujiuliza, je, mzee yule angeweza kunifanya niwe tajiri kama nilivyotaka? Wakati najiuliza hayo, nikashangaa mzee yule akisimama na kunishika kichwa changu.

“Usijiulize swali hilo, nitakufanya kuwa tajiri mkubwa sana,” aliniambia huku akiwa amenikazia macho.

Kwanza nikashtuka, ilikuwaje ajue kile nilichokuwa nikijiuliza, mpaka hapo, nikajua kwamba huyo mzee alikuwa na nguvu za ziada. Nikatulia na kumwangalia usoni. Kwa jinsi chumba kile kilivyokuwa, kiliniogopesha mno, kulikuwa na tunguli kila kona, harufu mbaya ambayo ilinifanya kutamani kuziba pua zangu.

“Unataka kuwa tajiri?” aliniuliza mzee huyo.

“Ndiyo!”

“Una uhakika?” aliniuliza.

“Ndiyo mzee!”

“Utayaweza masharti?” aliniuliza.

“Nitayaweza tu..”

Mzee yule akasimama na kuanza kuimba nyimbo ambazo sikuwa nikizielewa kabisa. Hakuishia kuimba tu bali akaanza kucheza pia. Nilibaki nikimwangalia, sikutaka kuzungumza kitu chochote kile kwani hata nguvu ya kufanya hivyo sikuwa nayo.

Akanisogelea na kunipaka unga fulani machoni mwangu. Ulikuwa na rangi nyeusi, alipoyapaka macho yangu, nikaanza kuhisi hali ya tofauti moyoni mwangu, furaha kubwa ambayo sikuwahi kuipata maisha yangu yote.

“Unajisikiaje?” aliniuliza.

“Najisikia vizuri….”

“Unahitaji utajiri wa aina gani? Wa kuku na mahindi au wa milele?” aliniuliza swali ambalo sikuwa nikilijua kabisa.

“Sijajua upo vipi!”

Mzee Mudi ndiye akachukua nafasi hiyo na kuanza kuniambia tofauti ya utajiri hiyo aliyoniambia mzee huyo. Utajiri wa kuku ulikuwa ni kwamba kuku anatupiwa mahindi chini, anaanza kula, kama akila mahindi matano, basi utajiri wako utakuwa ni wa miaka mitano, kama akila mahindi ishirini, basi utajiri wako utakuwa wa miaka ishirini, baada ya hapo unafilisika na kufa.

“Hapana huo siupendi!” nilimwambia mzee Mudi.

“Kwa nini? Huo ndiyo mzuri!”

“Mimi nautaka huo mwingine.”

“Unaujua upo vipi?”

“Sijui, ila nautaka huohuo!” nilimwambia.

Utajiri niliosema kwamba niliutaka ulikuwa ni wa masharti makubwa. Niliambiwa hilo lakini nikasema kwamba nautaka huohuo na kama ni masharti nitayafanya yote lakini si kukubali ule wa mwanzo wa kuwa tajiri kwa kipindi fulani kisha kufa.

“Huu una masharti makubwa mawili,” aliniambia mganga.

“Yapi?”

“Moja, unatakiwa kuwaua wazazi wako wote wawili,” aliniambia huku akikishika kitunguli kidogo kilichokuwa pembeni yake.

“Kuwaua wazazi wangu?”

“Ndiyo!”

“Na sharti jingine?” niliuliza huku nikionekana kuchanganyikiwa.”

“Kufanya mapenzi na maiti ishirini..” aliniambia.

****

Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatilia kesho hapa kujua kitakachoendelea katika sehemu ya 10

Duh story Nzuri sana
 
Back
Top Bottom