Hizo story zimenniburudisha na mimi natupa moja yangu. Enzi hizo tulivuna maharage shamba tukawa na kazi ya kumenya na kuanika kilasiku, tukawa tunapimiwa kiasi cha kumenya kwa kila mmoja wetu ili tusitegeane, siku ya tukio mimi sikumaliza kumenya fungu langu nikachukua zile ambazo sijamenya nikazifukia kwenye shina la migomba, kumbe dingi mjanja hua jioni baada ya kazi anapita kukagua, akazikuta basi akauchuna mpaka usiku muda wa kula tumesha kaa wote mezani akauliza nani katupa yale maharage ambayo bado hayajamenywa, huku na kule baada ya kubanwa ikajulikana ni mimi, basi dingi akaniambia nikayachukue niliporudi ndani akaniambia niyaoshe na kuyaweka kwenye sahani yangu ya chakula na ndio yatakua chakula changu usiku ule, basi washkaji wanakula wali wa nazi na mchuzi wa nyama mimi namenya maharage na kuyala, huku nalia. Nilikoma kujitia mjanja