Nile nini ili kuongeza wingi wa damu

Nile nini ili kuongeza wingi wa damu

Kanjunju

Member
Joined
Oct 8, 2010
Posts
92
Reaction score
6
wadau naomba mnisaidie nile nini ili niweze kuongeza wingi wa damu mwilini?
 
Sina hakika kama umeeleweka vizuri,ila ni vema ungesema kama umepimwa ukakutwa una upungufu wa damu au ni wewe mwenyewe tu umeamua ule kitu fulani ili uongeze damu mwilini.

Unajua kuna sababu nyingi zinazosababisha upungufu wa damu mwilini,na kwa bahati mbaya,kuna sababu kadhaa ambazo hazitegemei chakula kabisa,kwa hiyo hata ule chakula gani hakitazuia damu kupungua.Kwa hiyo kama ungesema kwanini umeamua kuuliza hivi ingesaidia kupewa majibu ya kuridhisha.
 
nadhani ungeanza kujibu swali la mdau hapo juu pengine ungepata ushauri mwingi. Ila kama ni mjamzito jaribu kula mboga za majani kwa wingi au kunywa aloevera
 
Kwa ajili hipi mbona haujaweka swali wazi? Ilikuwa yakawaida ikaanza kupungua tu au uliugua ndio ikaanza kupungua? au unatakujua tu!
 
Mdau naona unatoa thanks nyingi unapoambiwa kula mchicha na rozella,lakini laiti kama ungejua upungufu wa damu na sababu zake ungejibu hoja yangu hapo juu.Kwa uzoefu wangu mdogo humu JF Doctor mpaka sasa sijaona madaktari ninaowafahamu humu wakichangia hii mada yako.Pengine hawajaiona au wameiona ila kila mtu ana sababu zake za kuacha kuchangia.

Anyway,kila la heri katika kula mchicha na majani ya rosella mkuu.
 
Unapoendelea kupokea majibu tambuwa hili;''Asilimia 94 ya damu ni maji'', ni kama kusema kwa kila lita 10 za damu uliyonayo lita 9 kati ya hizo 10 ni maji. Hata ukijikata na ukaona majimaji mekundu yanatiririka ujuwe hiyo si damu, hayo ni maji ambayo ndani yake kuna damu!.

Jieleze vizuri usaidiwe.
 
Unapoendelea kupokea majibu tambuwa hili;''Asilimia 94 ya damu ni maji'', ni kama kusema kwa kila lita 10 za damu uliyonayo lita 9 kati ya hizo 10 ni maji. Hata ukijikata na ukaona majimaji mekundu yanatiririka ujuwe hiyo si damu, hayo ni maji ambayo ndani yake kuna damu!.

Jieleze vizuri usaidiwe.

Jamaa hataki kujieleza.Anataka majibu tu!
 
Ungeenda hospitali ndugu. Unaweza kuwa una kansa inakutafuna taratibu. Lakini kwa sababu yoyote ile pamoja na kuishughulikia, kula matunda na mboga za majani ambazo hazijapikwa sana.
 
nadhani ungeanza kujibu swali la mdau hapo juu pengine ungepata ushauri mwingi. Ila kama ni mjamzito jaribu kula mboga za majani kwa wingi au kunywa aloevera

Alovera kwa mjamzito? au unamaanisha rozela nitonye
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom