Niko njia panda, niende UDSM au DIT?

Niko njia panda, niende UDSM au DIT?

co fm

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2016
Posts
1,569
Reaction score
2,584
Habarini wanajamiiforum,

Mimi ni mwanafunzi niliyemaliza kidato cha sita mchepuo wa PCM 2016,nimebahatika kuupata div 2 ya point kumi,sasa katika kuchagua vyuo mimi napenda kusoma engineering UDSM ila watu wananishauri kama unataka kuwa engineer mzuri niende DIT.

Sasa wadau nisaidieni kunipanua mawazo malengo yangu ni kuja kujiajiri so nataka chuo ambacho ninaweza kupata ujuzi wa kutosha katika kozi zifuatazo electrical,computer engineering au mechanical engineering.
 
Kama unataka usome engineering njoo UDSM kama ulitoka form six. Kama ulikua umepitia FTC nenda DIT. Kwa huo ufaulu wako kupata electrical UDSM itakua ni inshu mana inakuaga na competition pia inahitaj wanafunzi wachache.
Kwa upande wa mechanical unaweza kupata UDSM.
Karibu CoET.
 
Kama unataka usome engineering njoo UDSM kama ulitoka form six. Kama ulikua umepitia FTC nenda DIT. Kwa huo ufaulu wako kupata electrical UDSM itakua ni inshu mana inakuaga na competition pia inahitaj wanafunzi wachache.
Kwa upande wa mechanical unaweza kupata UDSM.
Karibu CoET.
Mkuu vipiii na mwenye division one ya 9yanii Math..C physic.C na chemistry C..na o lvl alkwa na one ya kumi na NNE anawza chagulwa udsm kusoma electrical
 
NENDA DIT, LAKINI JIANDAE KWA MSULI, MAANA PALE MWENDO MCHAKAMCHAKA.
 
Kwa mtazamo hasi na kma unapoint nzuri chagua udsm mana pale kunaushindani mkubwa hivyo itakujenga kuwa bora. Usidanganywe na dit ukazani kuna elimu kwa vitendo hilo sikuhizi halipo kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watu. Hivyo nenda udsm ili utanue wigo wako
 
Back
Top Bottom