Nikiwa Rais: Nitahakikisha nashawishi kila Chama halali cha Siasa nchini kiashiriki uchaguzi: Huo ndio uzalendo zaidi.

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,791
3,360
Wanajamvi, nimeshtushwa sana,kusikia ni mgombe mmoja tuu amepitishwa na NEC kuwania kiti kilichokuwa cha Mh. Lisu.
Awali ya yote bila kujali yuko chama gani, ninampongeza.
Pili, nimesikitika na kujiuliza kulikoni, na je, ndivyo walipenda iwe kwa Wananchi wa jimbo hilo? Na je, ndivyo tulivyozoea ktk chaguzi zetu za vyama vingi? Na je, ni nani wa kulaumu au kunungunikiwa endapo wananchi wa jimbo hilo hawakutaka iwe hivyo?
Juzi, Mh .Rais wetu akiwa Bahi,aliendesha mchango wa kujenga shule. Kwa mliokuwepo au mlioona ktk luninga,aliita watu mbalimbali kupita mbele wachangie. Hata Bodyguard wake alichangia.
Pia, pa kusikitisha ni pa alipoita viongozo wa Vyama vya upinzani waende mbele kuchangia. Hakuna aliyejitokeza licha ya kuwepo ndani ya mkutano ule!!
Kwa tafsiri ya karibu ni kuwa Mh, Raisi wetu anatambua kisheria uwepo wa vyama vya upinzani!
Pia, anatambua uwepo wa viongozi wa upinzani ndani ya ujenzi wa Taifa hili.
Swali la kujiuliza, viongozi hao hupatikanaje? Jibu ni kwa njia ya chaguzi zenye fursa sawa na utashi na upendo wa walioko madarakani.
Ni kweli, viongozi hawa wanachaguliwa na wananchi kwa taratibu za kikatiba kwa kuhusisha vyama vyote. Uzalendo ni pamoja na kujumuisha Taifa kuwa kitu kimoja siyo katika kutoa michango tuu ya ujenzi wa maendeleo, bali hata zile haki sawa za msingi za kuchagua na kuchaguliwa. Sasa basi,
Ni nani anapaswa kuweka mazingira ya ushindani sawa katika haya?
Kwa maoni yangu, ningekuwa Rais, nisingekubali haya yatokee machoni pangu kwa vile, umma utakuwa unanitegemea kama Mzalendo no 1 na baba wa wanafamilia wote.
 
... sema "ningekuwa" maana hizo ni wishes tu ambazo huenda zisitimie hadi utakapomrudia muumba wako.
 
Waliunda vyama vya nini Kama kushiriki tu uchaguzi wanatakiwa washawishiwe!!! Mleta mada unachekesha
 
Nitakuunga mkono katika kampeni zako za kutaka kua Rais kama ungeanza na kuhakikisha tume ya uchaguzi i akua huru kabisa
 
kwa mfano: wewe na wenzako ambao ni askari mpo vitani, katika mapambano mkaona kundi la maadui linakuja , ikawabidi mkimbie mmoja wenu akagoma kukimbia. Je, mtafanya nini?
 
Waliunda vyama vya nini Kama kushiriki tu uchaguzi wanatakiwa washawishiwe!!! Mleta mada unachekesha
Mkuu, Yehodaya, hata kukutana tu na wenzako mnaoshindania uongozi ni jambo jema na la kishawishi.
 
Waliunda vyama vya nini Kama kushiriki tu uchaguzi wanatakiwa washawishiwe!!! Mleta mada unachekesha
In short rais wako ni mnafiki tena mwandamizi ktk upande huo. Nje ya mikutano ya hadhara amewaelekezea mitutu, anataka kuona makaburi, .................
Mtu anaenguliwa kwa sababu za kiboya kabisa na hila za wazi kabisa.........
 
Jiwe anaogopa kura. Mtu ambaye hata kupitishwa kwake CCM kulikuwa na "namna" kamwe hawezi kuziamini kura za wananchi wake.

Anajua kura za halali 2015 hakushinda. Anajua hata uchaguzi ufanyike leo hatashinda.
 
Waliunda vyama vya nini Kama kushiriki tu uchaguzi wanatakiwa washawishiwe!!! Mleta mada unachekesha
Ndugu, bado ninachekesha kwa hili la Mh. Jaffo ambaye kisheria ni mwakilishi wa Raisi?
 
Back
Top Bottom