Mhadzabe
JF-Expert Member
- May 20, 2009
- 3,226
- 4,730
Acha kabisa kula viporoNdugu zangu wa JF,
Naombeni namna ya kufanya nikiingia ofisini asubuhi saa 2 nikikaa kwenye kiti tu nasikia usingizi wa ajabu mpaka najiuliza ni kwanini.
Sijui nifanyeje?
Vaa nguo/funga mkanda pia Viatu visivyokubana
Unapokaa ofisini penda kuvua Viatu pia weka kitu kama mpira laini uwe unaukanyaga wakati wafanya kazi zako
Fungua mlango au madirisha ofisini kuruhusu hewa safi kuingia
Unapopata kifungua kinywa, kula kidogo tu, si lazima ushibe! Pendelea kula matunda zaidi na achana na vitafunio vya wanga kama chapati na vitumbua
Mwisho pata muda kuzungukia ofisi nyingine ndani ya jengo unalofanyia kazi hata kwa salam tu. Hii itakusaidia kuua usingizi unaoambatana na miayo mileeefu mpaka unatoa machozi.
Hapa Kazi Tu. Kidumu Chama Cha Mapinduzi