Nikalikuta 'vuvuzela' kanisani

Nikalikuta 'vuvuzela' kanisani

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Jumapili iliyopita nilihudhuria misa takatifu katika Kanisa katoliki la Mt.Anoarite,Makuburi Dar es Salaam. Ni misa ya kuanzia saa tano na robo asubuhi. Katika misa hiyo ya kuadhimisha sikukuu ya Watakatifu Petro na Paulo,wanakwaya wa Kwaya ya Mt.Kizito walitumia, pamoja na ngoma na kinanda, vuvuzela kunogesha uimbaji wao. Vuvuzela lilitumika mwanzo hadi mwisho wa misa katika uimbaji.


Kiukweli,sijawahi kushuhudia vuvuzela kanisani (kanisa katoliki) wakati wa misa. Nikiri kuwa vuvuzela lilichagiza vyema uimbaji na kuufanya ujae baraka zaidi. Hongereni wanakwaya ya Mt.Kizito kwa ubunifu huu. Nilibarikiwa sana kwa misa nzima na uimbaji wenu. Vuvuzela liko juu...
 
Kwaya za Dar hazijui kuimba kabisa, wanazidiwa na za Iringa. Ila kiboko yao MZA, shangwe mwanzo mwisho. Walau Makuburi wanajitahidi sana.
 
Jumapili iliyopita nilihudhuria misa takatifu katika Kanisa katoliki la Mt.Anoarite,Makuburi Dar es Salaam. Ni misa ya kuanzia saa tano na robo asubuhi. Katika misa hiyo ya kuadhimisha sikukuu ya Watakatifu Petro na Paulo,wanakwaya wa Kwaya ya Mt.Kizito walitumia, pamoja na ngoma na kinanda, vuvuzela kunogesha uimbaji wao. Vuvuzela lilitumika mwanzo hadi mwisho wa misa katika uimbaji.


Kiukweli,sijawahi kushuhudia vuvuzela kanisani (kanisa katoliki) wakati wa misa. Nikiri kuwa vuvuzela lilichagiza vyema uimbaji na kuufanya ujae baraka zaidi. Hongereni wanakwaya ya Mt.Kizito kwa ubunifu huu. Nilibarikiwa sana kwa misa nzima na uimbaji wenu. Vuvuzela liko juu...

Kwahiyo mulicheza kiduku??
 
.... hongera zao kwa ubunifu. Ilimradi tu ili noga watu wakafurahia Ibada ya kusifu bial kuvunja miiko ya kanisa
 
Jumapili iliyopita nilihudhuria misa takatifu katika Kanisa katoliki la Mt.Anoarite,Makuburi Dar es Salaam. Ni misa ya kuanzia saa tano na robo asubuhi. Katika misa hiyo ya kuadhimisha sikukuu ya Watakatifu Petro na Paulo,wanakwaya wa Kwaya ya Mt.Kizito walitumia, pamoja na ngoma na kinanda, vuvuzela kunogesha uimbaji wao. Vuvuzela lilitumika mwanzo hadi mwisho wa misa katika uimbaji.


Kiukweli,sijawahi kushuhudia vuvuzela kanisani (kanisa katoliki) wakati wa misa. Nikiri kuwa vuvuzela lilichagiza vyema uimbaji na kuufanya ujae baraka zaidi. Hongereni wanakwaya ya Mt.Kizito kwa ubunifu huu. Nilibarikiwa sana kwa misa nzima na uimbaji wenu. Vuvuzela liko juu...

Kwa hiyo vuvuzera yaani just a vuvuzera iliongeza baraka kwenye uimbaji,unless kama sijui maana ya baraka hapo sawa
 
Uliposema vuvuzela nikajua unamaanisha mtu fulani. Kumbe ni vuvuzela la ukwee kanisani.Ubarikiwe sana kama ulilifurahia kwenye kumsifu Mungu.
 
Waumini wa leo ni wavivu katika kumsifu Mungu kwa namna ya muziki ndio maana ndugu yangu uwepo wa 'vuvuzela' umekushangaza.

Nyakati za waumini wa kweli waliomuabudu Yehova walitumia kila kifaa cha muziki kiwezacho kutoa ala maridhawa katika ibada au maadhimisho yao kwa BWANA.

Mathalani:

1 Mambo ya Nyakati 13:8 Wakacheza Daudi na Israeli wote, mbele za Mungu, kwa nguvu zao zote; na kwa nyimbo na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa matoazi, na kwa tarumbeta.
 
Back
Top Bottom