Nikaishi wapi Dar hii, nikimbie hizi foleni?

uwezo wako wa kufikiri nadhani umefikia hapo!we unaona hiyo ndo solution?????go back to hell
 
Sitanii bali namaanisha hicho nilichokiandika. Ni muhimu sana kuongeza bei ya mafuta kwa gari ambazo si za abiria na mizigo. Hayo uliyoyasema yatafuata baadaye kwani utekelezaji wake si wa leo au kesho. Pia si lazima tuanze na bei hiyo niliyopendekeza. Hata kiwango cha shilingi 5,000/= kwa LITA MOJA ya mafuta kwa gari zisizo za abiria au mizigo kinaweza kuwa kizuri kuanza nacho na kupima matokeo yake ndani ya miezi sita.

Ongeza juhudi katika kazi unazofanya na ufanye saving at least na wewe ununue gari kwani naona unasumbuliwa na tatizo la kisaikologia zaidi.
 
Hivi hapo si ndiyo unatengenezea ulaji hao wenye taxi? Mafuta watanunua sh 2000 kwa lita halafu watawauzia wenye magari kwa elfu 3 - faida ya bwerereeee!

Hii idea yako kwa kweli haiingii akilini hata kidogo samahani sana kwa hilo. Laiti usafiri wa umma ungekuwa mzuri na wa kuridhisha basi wengi wetu tungeziwacha gari nyumabani kwa hiari yetu.
 
Zumbukuku, wala sijakurupa. Ni lazima tukubali ukweli kuwa tumeelemewa kwa sasa kama taifa katika mambo mengi. Hapa sizungumzii kupandisha bei ya mafuta kwa ujumla wake. Kinachozungumziwa ni kupandisha bei ya mafuta kwa magari ambayo kazi yake si kubeba abiria wala mizigo. Hapa kuna tofauti kubwa sana. Na moja ya faida kuu ni watu kutumia muda mfupi zaidi kwenda sehemu zao mbalimbali za kuzalisha mali. Uamuzi huu utailazimisha serikali kuu na serikali za mitaa kufanya kazi ya ziada ili kuboresha usafiri wa umma.

Solar power umekurupuka..umeshajiuliza utawezaje kucontrol uuzaji wa hayo mafuta?? Teknolojia ya kutofautisha aina ya mafuta kati ya yale yanayotumika kwa magari ya abiria na private use haiko kwa sasa..labda kama Bongo mtaweza kubuni yale yaliyoshindwa na wale waliondelea. ..umeshajiuliza hao watu watanunuaje hayo mafuta??? Au utatenegneza aina ya magari tofauti ili kucontrol uuzaji wa mafuta..kubali yaishe umechemka na point yako..

 
Hayo magari ya abiria yenyewe yako wapi sijui wewe uko mikoa gani kati ya ulioitaja, ukiwa barabara ya uhuru utaona watu wengi wanatembea kwa miguu, nenda morogoro road hali ni hiyo hiyo, vituo vya buguruni na ubungo kwa barabara ya mandela hali ndo mbaya zaidi,nenda kilwa road pia nyerere road kuanzia tazara kuelekea gongo la mboto, sijataja barabara ndogo kama za tabata, shekilango, bagamoyo ya zamani,si kwamba watu hawana hela ya nauli ndo maana wanatembea kwa miguu ni ukosekanaji wa magari ya abiria ndo maana inakuwa.
Labda ungeeleza wakishanunua kwa bei ya juu halafu ndo inakuwaje hiyo hela inaenda wapi au lengo ni kuondoa magari ya binafsi barabarani?
 
Hivi nitakuwa na akili sawa sawa,ninunue mafuta TShs 12,000/= wakati jirani yangu ana taxi au dala dala ambalo anaweza akanunua yeye alafu akanifaulishia? Jaribu kubuni upya.
 
kinachopendekezwa hapa ni kupandisha bei ya mafuta hayo kwa gari zisizo za abiria. Hii maana yake ni kuwa bei ya mafuta haitabadilika ila kama unatumia gari ambalo kazi yake si kubeba abiria wala mizigo itabidi ulipe shilingi 12,000 tu kwa kila lita ya mafuta utakayo nunua na kwa daladala na taxi wao wataendelea kununua mafuta kwa bei ya sasa. Hii itasaidia kupunguza sana magari binafsi na ya serikali katika barabara zetu hivyo kumaliza tatizo la foleni hapa nchini. Pia itatoa fursa nzuri ya kuwa na usafiri bora na wa uhakika wa umma.

Sidhani kama unaupa ubongo wako muda wa kufikria vizuri! Una uhakika gani kwamba hayo magari unayosema ya abiria (daladala na taxi) hawatachakachua na kuwapelekea mafuta hao wenye magari ya starehe? Wazo lako halina tija!!
 
Unless uwe unatania au unataka kuongeza posts tu,hili wazo lako SolarPower ni la kichekechea zaidi. Inajulikana wazi kabisa kuwa tatizo la foleni Tz ni barabara zake kuwa ndogo au finyu,kiwango/ubora duni, chache na sababu nyingine kibao. Barabara ziboreshwe na zipitike kwa urahisi,channels ziongezwe na wadau wali-suggest uwepo wa flyovers inapobidi. Nway kwa vile umetoa wazo,basi ngoja tulichukulie kama wazo tu!!

MWANZO NILISHTUKA NIKAJARIBU KUFIKIRIA HUYU MTOA MADA ALIKUWA ANAFIKIRIA KUTUMIA NINI KUFIKIRIA LAKINI BAADAYE NIKAMUWEKA KATIKA KUNDI LA SWALI LA PRETA. Kwa ujumla na hiki kitu kimekuwa kila siku twasema dawa pekee ya kuondoa foleni si kupandasha mafuta kama huyo mtu alivyofikisha ujumbe wako nia ni kufufua barabara na kuzianzisha mpya katika lengo la kupunguza foleni
 
Hayo magari ya abiria yenyewe yako wapi sijui wewe uko mikoa gani kati ya ulioitaja, ukiwa barabara ya uhuru utaona watu wengi wanatembea kwa miguu, nenda morogoro road hali ni hiyo hiyo, vituo vya buguruni na ubungo kwa barabara ya mandela hali ndo mbaya zaidi,nenda kilwa road pia nyerere road kuanzia tazara kuelekea gongo la mboto, sijataja barabara ndogo kama za tabata, shekilango, bagamoyo ya zamani,si kwamba watu hawana hela ya nauli ndo maana wanatembea kwa miguu ni ukosekanaji wa magari ya abiria ndo maana inakuwa.
Labda ungeeleza wakishanunua kwa bei ya juu halafu ndo inakuwaje hiyo hela inaenda wapi au lengo ni kuondoa magari ya binafsi barabarani?

Naomba niwaambie wote kuwa bila kutumia mkakati wa kupunguza gari binafsi katika barabara zetu na kuongeza gari za abiria na kuboresha usafiri wa umma tusahau kabisa kutatua tatizo la foleni katika miji yetu mikubwa. Barabara za Kawawa, Mandela , Nyerere, Kilwa, Shekilango na nyingine zimepanuliwa lakini angalieni hali ya foleni ilivyo katika barabara hizo???. Nakubaliana na wale wanaozungumzia uboreshaji wa barabara zote zilizoko katika miji yetu mikubwa. Ila tutambue kuwa ni muhimu sana tukawa na wiano mzuri kati ya idadi ya watu katika miji yetu na idadi ya gari za abiria na zile za binafsi.
 
Sidhani kama unaupa ubongo wako muda wa kufikria vizuri! Una uhakika gani kwamba hayo magari unayosema ya abiria (daladala na taxi) hawatachakachua na kuwapelekea mafuta hao wenye magari ya starehe? Wazo lako halina tija!!

Hawataweza kuchakachua kama tukitunga sheria zenye adhabu kali na kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sheria hizo. Kwa mfano ukipatikana na hatia yoyote katika mpango huu adhabu inakuwa ni kifungo kisichopungua miaka 12 pamoja na faini ya shilingi milioni 15 na viboko 36 .
 
MWANZO NILISHTUKA NIKAJARIBU KUFIKIRIA HUYU MTOA MADA ALIKUWA ANAFIKIRIA KUTUMIA NINI KUFIKIRIA LAKINI BAADAYE NIKAMUWEKA KATIKA KUNDI LA SWALI LA PRETA. Kwa ujumla na hiki kitu kimekuwa kila siku twasema dawa pekee ya kuondoa foleni si kupandasha mafuta kama huyo mtu alivyofikisha ujumbe wako nia ni kufufua barabara na kuzianzisha mpya katika lengo la kupunguza foleni

Mkuu, bila kupunguza idadi ya magari binafsi katika barabara zetu tusahau kutatua tatizo la foleni hapa nchini. Unachopendekeza ni sawa lakini ni suluhisho la muda tu hilo. Dawa ni kupunguza idadi ya magari binafsi katika barabara zetu pamoja na kuhakikisha kuwa barabara zetu zote zinapitika muda wote na zina ubora unaotakiwa. Mbali na kupandisha bei ya mafuta kwa magari ambayo si ya abiria, njia mbadala inayoweza kutumika katika kutatua tatizo la foleni ni kuanzisha KODI MPYA KWA KILA GARI LISILO LA ABIRIA LINALOPITA KATIKA BARABARA ZETU ZA LAMI KATIKA MIJI YA MWANZA, DAR ES SALAAM NA ARUSHA. KODI HII INAPENDEKEZWA IWE SHILINGI 25,000 KWA SIKU KWA KILA GARI LA AINA HIYO. Kodi hii italipwa katika vituo maalumu pale tu ambapo gari husika litakuwa nimeingia katika barabara zetu za lami katika miji ya Arusha Mwanza na Dar es Salaam. Kupitia kodi hii Serikali itakuwa na uhakika wa kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 250 kila mwezi. Na fedha hizi zote itabidi zitumike katika kuboresha Elimu yetu katika ngazi ya Msingi na Sekondari.
 
Hivi nitakuwa na akili sawa sawa,ninunue mafuta TShs 12,000/= wakati jirani yangu ana taxi au dala dala ambalo anaweza akanunua yeye alafu akanifaulishia? Jaribu kubuni upya.
:tonguez:

Itabidi kila unaponunua mafuta unatembea na Stakabadhi uliyonunulia hayo mafuta na kwa bei iliyopangwa. Vinginevyo somo POST NAMBA 40.
 
Hivi hapo si ndiyo unatengenezea ulaji hao wenye taxi? Mafuta watanunua sh 2000 kwa lita halafu watawauzia wenye magari kwa elfu 3 - faida ya bwerereeee!

Hii idea yako kwa kweli haiingii akilini hata kidogo samahani sana kwa hilo. Laiti usafiri wa umma ungekuwa mzuri na wa kuridhisha basi wengi wetu tungeziwacha gari nyumabani kwa hiari yetu.

Naomba usome POST NAMBA 40.
 
ukishangaa ya musa utayaona .....
kwa sababu hivi vituo vya mafuta ni charity na si biashara? hawa wanaomiliki vituo vya mafuta ni wafanya biashara, wanahitaji biashara ikue na wanaajiri watumishi wanaohudumia, unapotaka kupunguza idadi ya magari kwa kuweka bei hiyo ujiandae kupunguza na waajiriwa wa vituo hivi na (inawezekana) ujiandae wimbi la uhalifu mtaani kwa kukosa ajira nk.

dawa ya kupunguza foleni ni kujenga miundombinu ya uhakika yenye kiwango bora na kukidhi mahitaji husika, upanuzi wa barabara ni muhimu, alkadhalika kuwe na njia mbadala za kutoha na si "ku-relay" na barabara moja!!

bila kusahau barabara za juu n.k

hata usafiri wa treni ambao kwetu bado ni ndoto ya mchana....

vilevile kwa barabara za ndani mijini(mfano jamhuri, samora, uhindini, mosque n.k) kuacha kupaki magari kando kando ya barabara na kusababisha ufinyu wa barabara unaoleta msongamano usio na sababu.....

nyingine unaweza kuongezea, ila hiyo solution yako mmmmh umetokota mjomba.....:A S tongue:
 
ukishangaa ya musa utayaona .....
kwa sababu hivi vituo vya mafuta ni charity na si biashara? hawa wanaomiliki vituo vya mafuta ni wafanya biashara, wanahitaji biashara ikue na wanaajiri watumishi wanaohudumia, unapotaka kupunguza idadi ya magari kwa kuweka bei hiyo ujiandae kupunguza na waajiriwa wa vituo hivi na (inawezekana) ujiandae wimbi la uhalifu mtaani kwa kukosa ajira nk.

dawa ya kupunguza foleni ni kujenga miundombinu ya uhakika yenye kiwango bora na kukidhi mahitaji husika, upanuzi wa barabara ni muhimu, alkadhalika kuwe na njia mbadala za kutoha na si "ku-relay" na barabara moja!!

bila kusahau barabara za juu n.k

hata usafiri wa treni ambao kwetu bado ni ndoto ya mchana....

vilevile kwa barabara za ndani mijini(mfano jamhuri, samora, uhindini, mosque n.k) kuacha kupaki magari kando kando ya barabara na kusababisha ufinyu wa barabara unaoleta msongamano usio na sababu.....

nyingine unaweza kuongezea, ila hiyo solution yako mmmmh umetokota mjomba.....:A S tongue:

Naomba usome POST YANGU NAMBA 41 HApo juu.
 
sijasema mafuta yapande bali ni kwa gari zisizo za abiria tu. Hivyo kama una taxi au daladala bado utaendelea kununua mafuta kwa bei ya sasa.

fanya juhudi na wewe ununue gari lako sio kuleta mawazo ya wivu kwa waliojinyima na kununua.ninahakika ungekua umejibana na umenunua usafiri wako usingeandika huu upupu
 
Hawataweza kuchakachua kama tukitunga sheria zenye adhabu kali na kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sheria hizo. Kwa mfano ukipatikana na hatia yoyote katika mpango huu adhabu inakuwa ni kifungo kisichopungua miaka 12 pamoja na faini ya shilingi milioni 15 na viboko 36 .

Hii itatulazimu pia kuunda chombo madhubuti ambacho kazi yake itakuwa kuhakikisha chombo cha kusimamia utekelezaji wa sheria hiyo kinatekeleza majukumu yake. Hii itatugharimu sana.
 
Naomba usome POST YANGU NAMBA 41 HApo juu.

mkuu una roho ngumu bado unaendelea kutetea hoja yako, ukimaliza foleni ya barabarani kwa mpango huo unapandisha gharama za matibabu maana hospitalini na penyewe kuna foleni za kufa mtu, halafu ukitoka hapo unapandisha gharama za kuchukua na kuweka hela benki maana nako ni balaa, kisha unapandisha gharama za kuwaona tra maana nako ni foleni kwa kwenda mbele, kisha unapandisha ada mashuleni na vyuoni maana madarasa na mabweni hayatoshi watu wanalala hadi wanane chumba kimoja, halafu hakuna kukamata wahalifu maana nafasi magerezani hazitoshi na mahakama za kusikiliza kesi na kutoa hukumu ni chache na mahakimu na majaji ni wachache.

Kazi kweli kweli nchi hii kila mahali foleni hadi dukani kwa mangi na kwenyewe upandishe bei ya vitu.
 
Mkuu, bila kupunguza idadi ya magari binafsi katika barabara zetu tusahau kutatua tatizo la foleni hapa nchini. Unachopendekeza ni sawa lakini ni suluhisho la muda tu hilo. Dawa ni kupunguza idadi ya magari binafsi katika barabara zetu pamoja na kuhakikisha kuwa barabara zetu zote zinapitika muda wote na zina ubora unaotakiwa. Mbali na kupandisha bei ya mafuta kwa magari ambayo si ya abiria, njia mbadala inayoweza kutumika katika kutatua tatizo la foleni ni kuanzisha KODI MPYA KWA KILA GARI LISILO LA ABIRIA LINALOPITA KATIKA BARABARA ZETU ZA LAMI KATIKA MIJI YA MWANZA, DAR ES SALAAM NA ARUSHA. KODI HII INAPENDEKEZWA IWE SHILINGI 25,000 KWA SIKU KWA KILA GARI LA AINA HIYO. Kodi hii italipwa katika vituo maalumu pale tu ambapo gari husika litakuwa nimeingia katika barabara zetu za lami katika miji ya Arusha Mwanza na Dar es Salaam. Kupitia kodi hii Serikali itakuwa na uhakika wa kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 250 kila mwezi. Na fedha hizi zote itabidi zitumike katika kuboresha Elimu yetu katika ngazi ya Msingi na Sekondari.

Tanzania hakuna magari mengi isipokua tu ni miundombinu haitoshi. Kuna nchi zina mara 3 ya idadi ya magari ya Tanzania lakini mambo safi.

Hapa cha msingi kemea ufisadi ili hela zitumike kutengeneza miundombinu na sio kukomoa raia wanaojibana ktk matumizi yao. Pia serikali itoke Dar iende inakotakiwa kua, wakihama vigogo wa serikali na magari yao foleni hakuna.

Kumbuka kigogo mmoja akihama familia zaidi ya 3 zitahama i.e familia ya shamba boy, fundi magari,e.t.c na zaidi ya magari matatu yatahama i.e la mke, la watoto, la mshua mwenyewe e.t.c
 
Back
Top Bottom