naweza kusema kuwa miongoni mwa watu waliochaguliwa tra kwa nafasi ya custom officer ii is like dreams come true kwa sababu toka nikiwa mdogo mawazo yangu yalikua ni kufanya kazi sehemu tano tu ambazo ni tra,bot,Tic,wizarani na kuwa mwanajeshi,lakini kutokana na kwamba ukizaliwa africa ndoto zinaweza zisitimie basi nilijikuta naingia kufanya kazi ambazo sikuwahi kuzisomea au kuziwazia hata siku moja ingawa kwa naweza kusema zimenijenga na kunipa exposure ya kuelewa ulimwengu wa biashara na pia connection nazo nimekua nazo nyingi sana kwa kipindi hiki kifupi nilichojiingiza kwenye hii kazi,mtoto wa mkulima mimi sikutegemea kama kuna siku ningeweza kufanya biashara na maofisa kutoka ikulu ya Tanzania but kwa sasa ni kitu cha kawaida kwa mimi kuwa na appointment na maofisa wa ikulu kwa ajili ya kufanya biashara,kwa kifupi mimi kwa sasa nafanya kazi za sales katika lampuni moja ya wachina inayojishughulisha na importation ya vifaa vya magari hivyo nimejijengea urafiki na watu wa kila aina hapa nchini.
anway.imetokea issue ambayo inanifanya niwe dilemma katika maamuzi yangu,nami ni miongoni mwa vijana tulioitwa kazini tra lakini mpaka sasa nimeshindwa kuamua,ndugu zangu huko bush wananipigia kelele kwamba niende tra lakini hawa hawana exposure ya nini kinaendelea ulimwengun,wao wanajua nikiingia tra nitakua tajiri siku hiyo hiyo, kumbe kuna mengi ya kufanya huko.kwa sasa kampuni ninayoifanyia kazi wamenipa permanent contract toka mwanzoni mwa mwezi huu,mwanzo mshahara ulikua ni 0.75 gross lakini kwa sasa wameniongezea to 950000 gross,kila week napewa elfu 30 ya transport,elfu 15 ya muda wa maongezi,medical coverage wamenipa,house allowance ya 100000 kila mwezi na pia tunasafiri sana kwenda mikoani na nchi jirani.kwa kifupi maisha sio haba sana na ukizingatia sina majukumu makubwa yanayonikabili,malengo yangu yalikua ni kufanya kazi miaka mitatu na hawa jamaa ili baadae nami nije kufungua duka langu la spea za magari lakini sasa imejitokeza hii issue ya tra na huko kijijini watu naskia wmefanya mpaka sherehe eti kisa mtoto wao nimepata kazi tra,maslahi ya tra mimi siyajui yakoje na wala utendaji kazi wao siulewi ukoje ni kama naenda kuanza upya,halafu mbaya zaidi kuna madeni ya kampuni mengi tu yako nje ambayo natakiwa kuyakusanya hivo inaniwia ngumu kuondoka haraka haraka
kwa hiyo ningependa tushauriane kiundugu wakuu,nibaki na hawa jamaa zangu wachina au nitimkie tra maana wasiwasi wangu wa kwenda huko tra ni kwamba naamini ntapelekwa huko mikoani na mimi nimeshaanza kuset baadhi ya mambo yangu hapa mjini hivo nahofia yatakwama,