Niende au nisiende?

Niende au nisiende?

Mwanzo sikuamini kabisa katika mambo haya. Lakini si unajua ukiwa na shida unatafuta sehemu yoyote ya kuponea. Lakini huyu sio wale wa tunguli na wapiga ramli. Ni ustadh anatumia quran lakini alichosema ni kwamba napaswa nisomewe na nisafishwe mwili na niweke ubani kwa mkono wangu. Nasubiri unishauri zaidi hapo mkuu
Njoo pm
 
Mmmmh! Mpaka karne hii watu bado mnaamini ushirikina? Haya huyo bado ni mchumba tu anakushauri muende kwa mganga kwa tatizo mlilonalo, kwa nini msimuamini Mungu? Yaani kama mchumba wako ni mtu wa kwenda kwa waganga, kaa mkao wa kufanyiwa ndumba hadi utasahau watu wa kwenu!!! Mtu ambaye anaamini kwenda kwa waganga ni wa kukaa nae mbali, ni wa kuogopa kuliko EBOLA😵
 
sitaki kuamini kama umeshindwa kufikiria jambo dogo kam hilo.....mm sikushauri naamini ww mwenyewe unamajibu mazuri kuliko nitakayo kupa mm
 
Muamini Mungu muweza wa yote. Hao waganga wenyewe wana yao yanawashinda. Na ukiendekeza ushirikina hautoendlea
 
Nilikuwa na ngoja jibu kwa umakini sana
 
Mmmmh! Mpaka karne hii watu bado mnaamini ushirikina? Haya huyo bado ni mchumba tu anakushauri muende kwa mganga kwa tatizo mlilonalo, kwa nini msimuamini Mungu? Yaani kama mchumba wako ni mtu wa kwenda kwa waganga, kaa mkao wa kufanyiwa ndumba hadi utasahau watu wa kwenu!!! Mtu ambaye anaamini kwenda kwa waganga ni wa kukaa nae mbali, ni wa kuogopa kuliko EBOLA😵
Asante Pendaneni
 
"Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye Mwanadamu na kumfanya kinga yake"

Ushauri: USIENDE.
 
Ni hivi: Nimekuwa na matatizo binafsi yanayonisumbua. Sasa mchumba wangu kanishawishi anipeleke kwa mganga (ustaadh) kwamba ana uhakika pale ndo utakuwa mwisho wa matatizo yangu. Huyo mganga wanafahamiana sababu alishawahi kumtibu.
Sasa najiuliza, niende huko kweli?? Au ndo naenda kutengenezwa nipende milele na kukalishwa sijui wanaita.

NB: Nilishaenda nikatanguliza kiasi flani cha pesa lakini hakuna kazi iliyofanyika kutokana na ubize uliokuwepo, hivyo alituahidi turudi siku mbili baadae. Na nilipofika nyumbani ndo nikaijiwa na hili swali la niende au nisiende? Na je nisipoenda nimkwepe vipi huyu mchumba wangu ili asijue kama nimekwepa na tuendelee vizuri.
Niko njia panda wadau.
Wamasai na ninyi MNA Imani za kishirikina? Kushiriki ni Imani, kukushauri kwenda au kutokwenda MTU kama Mimi siwezi kukushauri sababu umeishasema awali una matatizo yako binafsi bila kujua hayo matatizo kila akushaurie akudangana. Kuna matatizo mengine ni psychological unaweza tu kupata counselling na ukapona! Nitafute ntakupa solution.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom