Nida ni jipu

Greg50

JF-Expert Member
Feb 11, 2014
1,953
2,431
Habari wakuu,

Hawa Nida nadhani kazi waliyopewa ya kuwapa wananchi vitambulisho hawaiwezi. Sasa hivi kila huduma serikalini wanadai uwe na kitambulisho cha Taifa, kuanzia uhamiaji, TRA mpaka TCRA.

Lakini tatizo linakuja kukipata hiko kitambulisho Nida utazungushwa bila mafanikio na huku mambo yako yakichelewa. Kwanza namba zao walizoweka mitandaoni kila muda zinatumika au hazipatikani, ile huduma yao ya *152*00# inakula tuu pesa yako majibu hupati, ukienda ofisini kwao utakutana na foleni kubwa utakaa, utafika pale mbele kwa mhudumu anakwambia wewe chako bado wanakiprocess huko kibaha, rudi wiki ijayo wiki ijayo, ukienda hiyo wiki ijayo ni kalenda tena, unachoma nauli mpaka unachoka.

Tatizo hili naamini si la kwangu peke yangu bali ni watu wengi, Niwaombe serikali wampatie investor yeyote yule tenda ya kutengeneza vitambulisho, hawa Nida wabaki kukusanya documents na taarifa za wananchi tuu ila vitambulisho wasitengeneze wao.
 
Niwaombe serikali wampatie investor yeyote yule tenda ya kutengeneza vitambulisho, hawa Nida wabaki kukusanya documents na taarifa za wananchi tuu ila vitambulisho asitengeneze wao.
Usalama wa nchi yako unauweka rehani!
 
Ukali wote anaojisifu nao mkuu wa kaya. Sielewi kwanini anashindwa kuwakamua NIDA.
Juzi nilishangaa sana.. Nilikwenda Uhamiaji kuchukua pasport ya mke wangu. Nilikataliwa kuichukua kwavile sina kitambulisho cha Taifa.. Nilionyesha cha kupigia kura, leseni ya udereva. Zote zilikataliwa. Hadi mke aende mwenyewe. Hapo ndipo tulipo fika. Halafu NIDA hawatoi vitambulisho..
 
Juzi nilishangaa sana.. Nilikwenda Uhamiaji kuchukua pasport ya mke wangu. Nilikataliwa kuichukua kwavile sina kitambulisho cha Taifa.. Nilionyesha cha kupigia kura, leseni ya udereva. Zote zilikataliwa. Hadi mke aende mwenyewe. Hapo ndipo tulipo fika. Halafu NIDA hawatoi vitambulisho..
Kwa hili la kunyimwa Pass ya Mke wako
Wapo sawa,wala hakuna tatizo

Mke wako,aende mwenyewe kuchukua,na si kuchukuliwa na Mtu yeyote yule,awe Baba au Mama hata ww Mume
Hufai kumchukulia

Shukran Chief
 
Habari wakuu,

Hawa Nida nadhani kazi waliyopewa ya kuwapa wananchi vitambulisho hawaiwezi. Sasa hivi kila huduma serikalini wanadai uwe na kitambulisho cha Taifa, kuanzia uhamiaji, TRA mpaka TCRA.

Lakini tatizo linakuja kukipata hiko kitambulisho Nida utazungushwa bila mafanikio na huku mambo yako yakichelewa. Kwanza namba zao walizoweka mitandaoni kila muda zinatumika au hazipatikani, ile huduma yao ya *152*00# inakula tuu pesa yako majibu hupati, ukienda ofisini kwao utakutana na foleni kubwa utakaa, utafika pale mbele kwa mhudumu anakwambia wewe chako bado wanakiprocess huko kibaha, rudi wiki ijayo wiki ijayo, ukienda hiyo wiki ijayo ni kalenda tena, unachoma nauli mpaka unachoka.

Tatizo hili naamini si la kwangu peke yangu bali ni watu wengi, Niwaombe serikali wampatie investor yeyote yule tenda ya kutengeneza vitambulisho, hawa Nida wabaki kukusanya documents na taarifa za wananchi tuu ila vitambulisho wasitengeneze wao.
Pole sana. Mimi nadhani wala siyo hao NIDA tu ila ni utamaduni wetu watanzania kwenye utendaji. Kila sehemu watu ni wazembe na wanajivuta. Na mbaya zaidi hakuna anayeona kama hili ni kero. Hawajifunzi kutoka nchi nyingine. Hivi vitambulisho wametoa kwa kukurupuka bila maandalizi (ni kila jambo tuna tabia hii). Utoaji wa vitambulisho huanza kwanza na usajili wa wananchi wote ili kuwa na database. Ikishapatikana database hapo ndiyo mtu mmoja mmoja anapeleka maombi ya kupatiwa kitambulisho. Hii inarahisisha sana kwani data nyingi za mhusika zinakuwa tayari zipo kwenye database. Wanachofanya wao sasa ni mkorogano usio na mpangilio. Halafu huduma ya mawasiliano ilivyokua wangekuwa wanatumia msg kujulisha watu vitambulisho vinapokuwa tayari. Wanatakiwa wa-set maximum time eg wiki mbili kila kwa mtu kupata kitambulisho.
 
nasikia kuna uhaba mkubwa wa karatasi na wino wa kuchapia,mpaka tuagize toka china
 
Kwa hili la kunyimwa Pass ya Mke wako
Wapo sawa,wala hakuna tatizo

Mke wako,aende mwenyewe kuchukua,na si kuchukuliwa na Mtu yeyote yule,awe Baba au Mama hata ww Mume
Hufai kumchukulia

Shukran Chief
Kwa hiyo wewe unajua zaidi ya Ujamiaji waliotaka kitambulisho cha taifa ili aweze kumchukulia mkewe passport?
 
Back
Top Bottom