Mama kasema tukosoe na tushauri suluhu: "Bure Bure" ya NIDA inatuchelewesha

Mwanamaji

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
2,896
4,495
Kufuatia wito wa Mh. Rais kwamba vijana tutumie mitandao kukosoa lakini pia tupendekeze suluhisho la yale tunayoyakosoa, leo nina pendekezo juu ya suala zima la utoaji wa vitambulisho vya utaifa kupitia NIDA.

Utangulizi;
Ninafahamu hali ya kifedha ya baadhi ya watanzania wenzetu ni ngumu sana na hivyo nikiri wazi kuwa wazo la kutoa vitambulisho vya utaifa BILA MALIPO lilikua ni jema kabisa. Ukizingatia mahitaji ya kitambulisho hiki katika huduma mbalimbali, ni hakika kuwa kila Mtanzania stahiki anatakiwa kukipata bila makwazo yoyote ya kifedha
Hivyo basi,

Kwa kutoa vitambulisho bure kabisa, tumetengeneza "gharama" kubwa zaidi. (Time is Money):
1. Mtaani kuna malalamiko ya wananchi juu ya muda wanaotakiwa kusubiri ili kupata vitambulisho vyao mara baada ya kujisajili katika ofisi za mamlaka (NIDA). Wapo waliosubiri miaka miwili, miaka mitatu, mwaka mmoja, n.k

2. Ripoti ya CAG (iliyosomwa hivi karibuni) inaonyesha kwamba, kwa kasi ya utengenezaji vitambulisho wanayokwenda nayo NIDA, ni wazi zile materials zilizopo stoo zitafikia muda wa kuharibika kabla ya kutumiwa, hivyo kuipa serikali hasara ya mabilioni ya shilingi.

3. Ukipoteza kadi yako, ukataka nyingine yaani ku-Renew, mara baada ya kulipia Tshs 21,000/= na kukamilisha taratibu zote za kipolisi za kupotelewa mali, utatakiwa KUSUBIRI kadi hiyo kwa MIEZI MITATU (kama mtu anayejiandikisha upya).

Kutokana na hoja tatu tajwa hapo juu, ni wazi kwamba mamlaka ya vitambulisho vya taifa NIDA, inakosa ufanisi kwa maana ya uchache wa VIFAA na uhaba wa RASILIMALI WATU kuweza kuendana mahitaji utoaji wa vitambulisho KWA WAKATI.

Suluhu:
1. Tuijengee uwezo NIDA kibajeti, nilisikia wakati fulani waziri Simbachawene anasema wataiwezesha taasisi hii kwa kuiongezea mashine zaidi.

2. Wananchi tuchangie kupata vitambulisho hivi. Iwekwe gharama nafuu (Hata elfu 5 au elfu 10), mtu alipie na apate kitambulisho chake angalau ndani ya wiki MOJA.
Hizi fedha zitumike kuongeza mashine, kuajiri watumishi ili kuongeza ufanisi wa NIDA kama taasisi.

Je, tozo hii itakua ni mzigo kwa mwananchi?
Ndiyo, ukilinganisha na BURE, tozo yoyote ile ni mzigo.
Lakini ukilinganisha na adhabu ya kusubiri kwa mwaka mmoja au hata miaka miwili kuelekea mitatu (mzigo wa sasa), tozo ninayoipendekeza si lolote, si chochote.

Wasio na uwezo watafanyaje?
Wale wasio na uwezo wa kuilipa kama wazee vikongwe, hawa watatuomba hukuhuku kwenye jamii hiyo elfu 5 au elfu 10, kitambulisho sio suala la dharula, siku akipata hiyo pesa na akaenda NIDA basi alipe na apate kwa wakati.

Je, utaratibu wa kulipia huduma ni mgeni?
Hapana. Tunalipia vyeti vya kuzaliwa, tunalipia hati za kusafiria, tunalipia huduma kedekede ambazo ni haki zetu za msingi kuzipata.
Kama huduma inapatikana kwa wakati, hamna mtu anaweza kulalamikia malipo ya huduma hiyo.

Kwa sasa kitu pekee wanachoweza kijivunia watu wa NIDA, ni kutoa "namba za NIDA" yaani NIN.
Kimsingi hii ni "nusu huduma", tunataka mamlaka inayoweza kutupatia vitambulisho (physical ID) kwa wakati.

Burebure ya NIDA inatuchelewesha.

Asubuhi njema kwenu.
 
NIDA mbona inajiendesha kibiashara, tangu mwaka jana mwezi wa 10 walianza kutoza Tsh. 500 Kwa kila single request ya taarifa kwa mtoa huduma, Kwa mfano unapokwenda kusajili laini ya Simu pale unapoweka kidole kwenye kile kifaa ili taarifa zako zivutwe kutoka NIDA mtoa huduma(Mtandao husika wa simu) anatozwa Tsh. 500, hivyo hivyo ukiwa unataka kupata TIN Number TRA anatozwa Tsh 500 kwenda ku vuta taarifa zako kutoka NIDA, Hii ni kwa watoa huduma wote wanaotegemea kuthibitisha Utambulisho wa Mteja kupitia NIDA.

Nadhani hiyo inatosha.
 
Daaah mwaka unakatika sasa sijapata kitambulisho. Kila ukienda bado bado bado. Nilisikia mashine mpya imeletwa itakayokua inachapa vitambulish vingi kwa wakati mmoja. Sijui kazi yake ni ipi sasa. Tatizo letu kila kitu kinaingiziwa siasa aisee.

Mwaka 2017 waziri mkuu akasema ni lazma zoezi la kuandikisha watu liende kwa spidi matokeo yake watu kibao wamejiandikisha na hawana izo id mpaka leo.
 
Je, huu utarabu haufanyi upigaji wa fedha zinazopatikana uwe rahisi? Nikiri sijui hiyo system inavyofanya kazi, lakini nikitumia uzoefu wangu wa ''Bongoland'' nadhani ni rahisi sana ku-manipulate kumbukumbu za kila mtu anaye-request taarifa za kutoka NIDA.

Hivyo ku-manipulate mapato! Kwa nini tozo isiwekwe kwenye kitambulisho kama alivyopendekeza mtoa mada ili iwe rahisi zaidi ku-monitor mapato? Idadi ya vitambulisho vilivyotoka ikijulikana ni rahisi kujua zimeingia shilingi ngapi.....
 
Je, huu utarabu haufanyi upigaji wa fedha zinazopatikana uwe rahisi? Nikiri sijui hiyo system inavyofanya kazi, lakini nikitumia uzoefu wangu wa ''Bongoland'' nadhani ni rahisi sana ku-manipulate kumbukumbu za kila mtu anaye-request taarifa za kutoka NIDA...
Kila Request inakuwa logged (kuhifadhiwa) na NIDA pia na Mtoa huduma, na Kila request ina utambulisho wake wa kipekee (Transaction Id), mwisho wa mwezi NIDA anatuma invoice kwa mtoa huduma kulingana na idadi ya request za mtoa huduma.
 
NIDA mbona inajiendesha kibiashara, tangu mwaka jana mwezi wa 10 walianza kutoza Tsh. 500 Kwa kila single request ya taarifa kwa mtoa huduma, Kwa mfano unapokwenda kusajili laini ya Simu pale unapoweka kidole kwenye kile kifaa ili taarifa zako zivutwe kutoka NIDA mtoa huduma(Mtandao husika wa simu) anatozwa Tsh. 500, hivyo hivyo ukiwa unataka kupata TIN Number TRA anatozwa Tsh 500 kwenda ku vuta taarifa zako kutoka NIDA, Hii ni kwa watoa huduma wote wanaotegemea kuthibitisha Utambulisho wa Mteja kupitia NIDA.

Nadhani hiyo inatosha.
Kama NIDA inatengeneza fedha za kutosha kama usemavyo basi wanunue mashine na waajiri watumishi wa kutosha ili watoe vitambulisho kwa wakati.

Kama umesoma na kuelewa uzi wangu nimelenga katika kuhakikisha kwamba huduma inatolewa kwa wakati.
Kusema tu kwamba kwa sasa hayo makusanyo ya 500 wanayokusanya yanatosha, bila kuboresha huduma ninayoizungumzia, nadhani si sawa.
 
Daaah mwaka unakatika sasa sijapata kitambulisho. Kila ukienda bado bado bado.
Nilisikia mashine mpya imeletwa itakayokua inachapa vitambulish vingi kwa wakati mmoja. Sijui kazi yake ni ipi sasa. Tatizo letu kila kitu kinaingiziwa siasa aisee.
Mwaka 2017 waziri mkuu akasema ni lazma zoezi la kuandikisha watu liende kwa spidi matokeo yake watu kibao wamejiandikisha na hawana izo id mpaka leo.
Ni bora ungelipia hata elfu 10 na ukapata kitambulisho ndani ya wiki moja na maisha mengine yakaendelea.
Sasa hii nenda rudi inakera sana na ni kupotezeana muda.

Waweke tozo, zinunue mashine nyingi, ziajiri watumishi wengi, watu wapate vitambulisho "chap kwa haraka".

Basi.
 
Ni bora ungelipia hata elfu 10 na ukapata kitambulisho ndani ya wiki moja na maisha mengine yakaendelea.
Sasa hii nenda rudi inakera sana na ni kupotezeana muda.

Waweke tozo, zinunue mashine nyingi, ziajiri watumishi wengi, watu wapate vitambulisho "chap kwa haraka".

Basi.
Ni kweli, bure aghali.
 
Kwa Tanzania yetu ninayoijua unaweza ukalipa na kitambulisho usipate. Mbona Tanesco unalipa na unakaa miezi sita kabla ya kufungiwa umeme.

Mimi huwa najiuliza mbona kitambulisho Cha mpiga kura vilitengenezwa ndani ya muda mfupi. Mkiendekeza kulipia kila kitu tumekwisha. Huduma gani tusiyolipia kwa mlango wa nyuma, huku tunalipa Kodi kibao. Kodi tunazolipa zinatosha kugharimia vitambulisho.
 
Kwa Tanzania yetu ninayoijua unaweza ukalipa na kitambulisho usipate. Mbona Tanesco unalipa na unakaa miezi sita kabla ya kufungiwa umeme.

Mimi huwa najiuliza mbona kitambulisho Cha mpiga kura vilitengenezwa ndani ya muda mfupi. Mkiendekeza kulipia kila kitu tumekwisha. Huduma gani tusiyolipia kwa mlango wa nyuma, huku tunalipa Kodi kibao. Kodi tunazolipa zinatosha kugharimia vitambulisho.
 
hivi mtoa mada kwa akili yako unafikiri Kila mtanzania ana uwezo wa Kutoa 5,000 kwa ajiri ya ID? hiyo pesa ni ndogo kwako lakini kwa watanzania walio wengi hicho no kiwango kikubwa mno, nashauri iendelee kuwa bure Ila wafanyakazi wa nida Kama wamechoka kazi waseme tuajiri damu changa ichape kazi.
 
Mimi nmejiandikisha toka Mwaka 2019 mwezi 11 ila mpk leo nna namba tu 🥲
Au pengine kungekua na huduma ya FAST TRACK, anayetaka cha bure asubirie miaka mitatu... sawa.
Anayetaka cha haraka basi alipie.
 
Kwa Tanzania yetu ninayoijua unaweza ukalipa na kitambulisho usipate. Mbona Tanesco unalipa na unakaa miezi sita kabla ya kufungiwa umeme.
Mimi huwa najiuliza mbona kitambulisho Cha mpiga kura vilitengenezwa ndani ya muda mfupi. Mkiendekeza kulipia kila kitu tumekwisha. Huduma gani tusiyolipia kwa mlango wa nyuma, huku tunalipa Kodi kibao. Kodi tunazolipa zinatosha kugharimia vitambulisho.
Wewe tayari unacho hiki kitambulisho mkuu ?
Ulikipata kwa muda gani tangu ujiandikishe ?
Maana inaonekana hujakutana na kadhia ninayoizungumzia.
 
hivi mtoa mada kwa akili yako unafikiri Kila mtanzania ana uwezo wa Kutoa 5,000 kwa ajiri ya ID? hiyo pesa ni ndogo kwako lakini kwa watanzania walio wengi hicho no kiwango kikubwa mno, nashauri iendelee kuwa bure Ila wafanyakazi wa nida Kama wamechoka kazi waseme tuajiri damu changa ichape kazi.
Maskini ya Mungu, umesoma uzi na kuelewa kweli wewe ?

Nimependekeza suluhisho la WATANZANIA WASIOWEZA KUMUDU ELFU 5, wanawezaje kupata huduma hii.
 
hivi mtoa mada kwa akili yako unafikiri Kila mtanzania ana uwezo wa Kutoa 5,000 kwa ajiri ya ID? hiyo pesa ni ndogo kwako lakini kwa watanzania walio wengi hicho no kiwango kikubwa mno, nashauri iendelee kuwa bure Ila wafanyakazi wa nida Kama wamechoka kazi waseme tuajiri damu changa ichape kazi.

Na kwa taarifa yako ni kwamba, ikitokea kitambulisho hicho kimepotea au kuharibika na ukahitaji kuki_Renew unatakiwa kulipia elfu 20. (Hata kama wewe ni mtanzania usiyemudu kupata elfu 5)

Ukishafanya hivyo, utakisubiri kwa muda mrefu (kama ambaye anaandikisha upya).

Lengo la uzi huu ni kutafuta namna ya kuiharakisha hii huduma muhimu kwa watu. Vitambulisho vipatikane kwa wakati.

Tukiamua kushindana kuwaonea huruma wasio na uwezo wa kumudu hiki na kile, nitapendekeza yafuatayo;-
1. Tufute ada na tozo zote katika shule za umma
2. Matibabu katika hospitali za umma yatolewe bure.
3. Vyeti vya kuzaliwa vitolewe bure.
4. Leseni mbalimbali zitolewe bure.
5. Tusafiri bure kwenye usafiri wa umma (UDART, TAZARA, TRC, Vivuko, n.k)
N.k n.k
Ukiniuliza kwanini tufanye hivyo, nitakuuliza HIVI UNAFIKIRI KILA MTANZANIA ANAWEZA KUPATA PESA YA KULIPIA HIZO HUDUMA ?

Nirudie tena lengo la huu uzi ni kutafuta suluhu ya ucheleweshwaji wa vitambulisho vya NIDA, wala sio kuongeza mapato ya serikali, kuwanyima "haki" wale wasionacho, au kuongeza gap kati ya walionacho na wasionacho.
 
Kwa Tanzania yetu ninayoijua unaweza ukalipa na kitambulisho usipate. Mbona Tanesco unalipa na unakaa miezi sita kabla ya kufungiwa umeme.
Mimi huwa najiuliza mbona kitambulisho Cha mpiga kura vilitengenezwa ndani ya muda mfupi. Mkiendekeza kulipia kila kitu tumekwisha. Huduma gani tusiyolipia kwa mlango wa nyuma, huku tunalipa Kodi kibao. Kodi tunazolipa zinatosha kugharimia vitambulisho.
Kweri kabisa nakuunga mkonoo
 
Back
Top Bottom