Hivi watu wa Tanzania mbona hamna shukurani? CCM imekutoeni mbali, kumbukeni CCM imezaliwa na TANU na ASP, kwa hiyo Bila CCM watu wa bara na visiwani msingepata uhuru.
Mazuri yote mnayoyaona yanatokana na CCM, elimu uliyonayo ni CCM, maisha yako ya zamani na sasa ni CCM, uhuru wa kuongea, kuabudu na vyombo vya habari ni CCM, jamani mbona mnalaumu uongo?
Kumbukeni hata hivyo vyama vyenu vya siasa mnavyoviita upinzani bila CCM visingekuwepo. Loh! niachieni CCM yangu.
Watu gani nyie msio na shukurani, baba ni baba tu, hata siku moja bega halizidi kichwa hata kama linaonekana ni kubwa. TCCM tutashinda siku zote na miaka yote.
Nawasilisha.
Umesahau kuandika wizi EPA, Meremeta,Richmond,DOWANS, etc vyote ni CCM
Wizi wa madini na mikataba feki iliyosainiwa na watu ambao utafikiri wasoma shule ya ngumbaru vyote ni CCM
Kukaribisha wawekezaji feki na kuwagawia maeneo ya wananchi bure na kusababisha migogoro ya ardhi kila kona ya nchi vyote ni CCM etc........................................................