Ni ya nani hii hapa mjini?

Ni ya nani hii hapa mjini?

TODAYS

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
15,202
Reaction score
25,378
Katika hali ya kushangaza tulisimama kwenye foleni kwa takribani 30dkk, baadaye tulipokaribia ndipo nikagundua nini ilikuwa sababu ya ile foleni.

Sasa basi hawa jamaa (mbuzi) wana tabia ya ajabu sana wakiona chakula (nyasi) wanasimama wanakula, wakianza ku_move wanakuja katikatibya barabara na kusonga mbele, we piga honi zako au uwakwepe kwa nia ya kuwa_push aaah wapi, wanaendelea na mishe zao.

My take:
Hivi ni wanani hawa, na mbona ile sheria ya ufugaji mijini siioni ikifanya kazi kwa aina hii ya mifugo sumbufu mjini?
 

Attachments

  • 1428316989767.jpg
    1428316989767.jpg
    52.6 KB · Views: 1,020
Hua nasikia sio mbuzi hao ni majini.Hawana mwenyewe wanaishi kivyao vyao mjini hapa.Nani anayeweza kuwaachia mbuzi wake huru hivyo kwa dar hii? Hua nawaona sana magomeni na hiyo picha umepiga maeneo ya karibu na magomeni mikumi.
 
Ni kwamba hawa mbuzi walipotea, na mwenyewe akasoma albadili, kwa hiyo hata mwenyewe hawezi kuwachulua tena.
 
Hua nasikia sio mbuzi hao ni majini.Hawana mwenyewe wanaishi kivyao vyao mjini hapa.Nani anayeweza kuwaachia mbuzi wake huru hivyo kwa dar hii? Hua nawaona sana magomeni na hiyo picha umepiga maeneo ya karibu na magomeni mikumi.

Ya kuambiwa, changanya na yako!!!
 
Aisee Ni mbuzi wangu naombeni msiwabugudhi nitawatoa mabusha oooooh
 
Wasiliana na Kova mwambie kuna maandamano ya mbuzi wanaelekea Ikulu..
 
Hiyo ipo sana kwenye miji ya mwambao wa pwani. Amini usiamini hao mbuzi ni wa mtu(mzee) na anawaona kila mahali waendapo. Mwizi yeyote akitaka kuwaiba ile nia hutoweka na kubaki akiwaangalia tu. Hata waendesha gari sio rahisi kuwagonga zaidi ya kutawaliwa na hofu inayoambatana na huruma ya ajabu.
Kifupi wanakuwa attached na imani flani za kishirikina.
 
mura akuna cha mbuzi wa alubadili wala alkaida!tulikula wa mwanza mara 4. nimiaka sita sasa. wanalala wapi hao mnipe maelekezo. nawaitajisana.
 
Kun kitu cha kujiuliza, mifugo iliyo nje ya mji mara nyingi ukiikuta barabarani kwanza yenyewe uondoka au ukipiga honi kuondoka ila hii ya hapa sijui kama imezoea hizi fujo za mji, ukipiga honi AU kuisogelea karibu kwa gari wala haina habari, zaidi mbuzi ndo anasimama kabisa na kuanza kujikuna.

Ole wako liwepo beberu korofi ndo utaona sinema hapo ...!
 
Hao mbuzi wako maeneo tofauti maeneo ya Ilala bungoni pia wapo,Magomeni pia ni mbuzi wa wababe fulani wa maeneo hayo ni wababe wa mambo ya ulozi wanaogopeka mpaka na serkar
 
mmm kumbe haya yapo . . ? mbuz wa town hao haki sawa kwenye matumizi ya barabara. .
 
Huku Babati wako wengi sana, hawana mwenyewe, wanakunywa supu, awanakula. chipsi mayai, hawaogopi watu.ole wako umuibe,,,,,,,:rockon:
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom