Ni wapi Serikali imefanikiwa kwa asilimia 100?

Ni wapi Serikali imefanikiwa kwa asilimia 100?

njeleson

Member
Joined
Apr 25, 2015
Posts
24
Reaction score
8
Nilikuwa najaribu Kufanya uchunguzi mdogo, kuona na eneo gani ambapo serikali yetu iliyo chini ya chama tawàla CCM. Kwa HAKIKA nimeshindwa kuona ni eneo gani ambapo serikali imemudu kufanya vizuri kabisa.

Hebu jaribu kuangalia maeneo yafuatayo( kama mifano tu)

1. Elimu: Shule za serikali ni matatizo makubwa.

2. Afya: Hospitali za serikali ni shida kubwa kuliko kawaida.

3.Usafirishaji: Barabara ni ajali kila kukicha. Bandarini ni malalamiko ya ubovu wa miundo mbinu, rushwa n.k. Usafiri wa ndege ( ATC) ni taabani, Uwanja wa ndege Dsm, mbovu, rushwa n.k.

4. Utumishi: Watumishi wa serikali kila siku ni malalamiko ya hali duni ya maisha, yanayosabàbisha utendaji mbovu ktk ofisi za serikali.

5. Kilimo: Hakuna miundombinu rafiki kwa wakulima. Wakulima wamekuwa yatima!

6. Posta na Simu: Chali !! Hakuna kinachoendelea huko!

Jamani, ivi ni sehemu gani ambapo serikali imefanya angalau kutufanya wananchi (wapigakura) tujivunie?? Au ni Intelligencia ya polisi PEKEE ndo iko vizuri? Inawezekana ...!!

Wana JF nisaidieni kunikumbusha basi. Kama sivyo nini kifanyike ili angalau tuwe na eneo moja la kujivunia??
 
fungu la mboga kuuzwa milioni 10 ni mafanikio makubwa mnooo bila kusahau nyoka wenye macho makengeza kuruhusiwa kuwa bungeni kwa kweli tujivunie mafanikio haya
 
Wewe mwenyewe umefanikiwa kimaisha kwa asilimia 100? Ungekuwa umefanikiwa kwa asilimia 100 usingekuja kulia lia hapa ungekuwa visiwa vya Bahamas unakula raha mwehu wewe.
 
njeleson

Mkuu huko ulikojikita kutafuta mafanikio ya serikali kwenye maendeleo ya wananchi siko. Ukitaka kutafuta mafanikio ya serikali yetu jikite kwenye Esrow, epa, richmond na maufisadi ya namna mbalimbali yanayofanywa na viongozi.

Na research yako wewe ni kuhudhuria mikutano yao. Kule utakuta wanajisifu mambo ya majoka yenye makengeza, hela za mboga nk.Ukitaka kutafuta serikali ilikoshindwa 100% ndo ujikite kwenye hizo mada zako 6.
 
Last edited by a moderator:
Imefanikiwa Kwenye AMANI, UTULIVU, MSHIKAMANO na MUUNGANO wetu wa kupigiwa mfano Afrika nzima.

Ivi ni kweli kuwa Tz tuna amani?? na hii hali tunayoendeleea nayo ni utulivu?? Je tubaki tukijivunia Muungano kwa wengine ilihali ndani ya nchi ni Kero mtupu?
 
njeleson

kuongeza deni la Taifa na umasikini kwa mtanzania,na kusema uongo mafanikio asilimia 200
 
Last edited by a moderator:
Wewe mwenyewe umefanikiwa kimaisha kwa asilimia 100? Ungekuwa umefanikiwa kwa asilimia 100 usingekuja kulia lia hapa ungekuwa visiwa vya Bahamas unakula raha mwehu wewe.
hii ndiyo sera ya ccm,Mimi kwanza wengine baadae-ufisadi ni matokeo ya sera hii,ndio maana si ajabu kuona wanaccm wakipiga bilioni 300 huku wakijua MSD imegoma kusambaza madawa kwa wadanganyika kwa deni la bilioni 90 tu maana wao wanatibiwa India,ujerumani,marekani na kwingineko.safi ccm ya leo
 
Mkuu huko ulikojikita kutafuta mafanikio ya serikali kwenye maendeleo ya wananchi siko. Ukitaka kutafuta mafanikio ya serikali yetu jikite kwenye Esrow, epa, richmond na maufisadi ya namna mbalimbali yanayofanywa na viongozi.

Na research yako wewe ni kuhudhuria mikutano yao. Kule utakuta wanajisifu mambo ya majoka yenye makengeza, hela za mboga nk.
Ukitaka kutafuta serikali ilikoshindwa 100% ndo ujikite kwenye hizo mada zako 6.

Mapya yaibuka sakata la Escrow.

http://www.globalnewztz.com/2015/05/mapya-yaibuka-sakata-la-escrow.html


Mbunge wa Ole (CUF), Rajab Mbarouk Mohamed.

Kashfa ya Escrow imeibuliwa upya bungeni baada ya wabunge kudai kuna kampuni ya Simba Trust inayomiliki asilimia 50 za kampuni ya Pan Africa Power (PAP), ambayo inadaiwa kuhusika katika ufisadi wa uchotwaji wa zaidi ya Sh.bilioni 300 katika akaunti ya Tegeta Escrow.

Hayo yaliibuliwa jana bungeni na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni wakati wa kuwasilisha hotuba yake ya kambi hiyo kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya mwaka 2015/2016 ya Wizara ya Viwanda na Biashara.

Msemaji wa kambi hiyo, Mbunge wa Ole (CUF), Rajab Mbarouk Mohamed, alisema wakati umma wa Watanzania unataka kuelewa wamiliki wa kampuni ya Simba Trust lakini katika hali ya kushangaza Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela), umegoma kutoa majina ya wamiliki wa kampuni hiyo.

"Kambi rasmi ya upinzani tunaitaka serikali ieleze kwanini taasisi hii ya Brela iliyo chini ya wizara hii bado inakataa kutoa majina ya wamiliki wa Simba Trust, imekuwa kama ilivyokuwa makampuni yaliyohusika na uchotaji mabilioni ya Epa na fedha za mradi wa Meremeta," alisema.

Mnyaa alisema hatua ya Brela kukataa kutoa majina ya wamiliki wa kampuni hiyo kuna unganisha na dhana kwamba wamiliki wa kampuni hiyo ni viongozi wandamizi wa serikali ya CCM.

Alisema matatizo ya kiutawala yaliyopo katika sekta ya umma nchini yamesababisha sekta ya viwanda kushindwa kujiendesha kiushindani.

Aliongeza kuwa Shirika la Umoja wa Mataifa la na Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco), limebainisha kuwa viwanda vingi vinaendeshwa kwa hasara kutokana na kuwapo kwa gharama kubwa za uzalishaji, tija ndogo, riba kubwa za kibenki,tatizo la umeme na urasimu.
 
Kwenye ufisadi na wizi wamefanikiwa zaidi ya asimilia 100.
 
Ivi ni kweli kuwa Tz tuna amani?? na hii hali tunayoendeleea nayo ni utulivu?? Je tubaki tukijivunia Muungano kwa wengine ilihali ndani ya nchi ni Kero mtupu?
Kama umeenda shule kidogo utaelewa kuwa AMANI na UTULIVU ni vitu viwili tofauti. Na kama kimojawapo hakipo Tanzania basi lazima kingine kipo. MSHIKAMANO upo kwa hakika japo tunaanza kuona mmomonyoko wa mshikamano. MUUNGANO upo na anayebisha ana matatizo. Kinacholeta mtafaruku kwa sasa ni muundo wa muungano.
 
Acheni unafiki nyie. Ukitaka kusema bwana hakuna wa kukuzuia kusema maana huko uliko unajua wewe mwenyewe unafanya nini na ni kwanini unafanya hivyo. Maisha yako yapo mikononi mwako na mafanikio yako yapo pia kwako. Tuambie ukweli wa mambo juu yako kabla ya kuwalaumu wengine. Wewe mwenyewe umefanikiwa kimaisha kwa asilimia 100?

Ungekuwa umefanikiwa kwa asilimia hizo usingekuja kulia lia hapa ungekuwa na mambo yako unakula raha zako mwenyewe. Acha unafiki wewe usiyo na maana. Kusema mnasema sana mkigeuka mnapongezana ila mkihujumiana wenyewe kwa wenyewe hizo hamtuambii. Unafiki huo.
 
unajua maana ya aman ww!
Najua sana tu. Penye AMANI pana UTULIVU unaokuja kama matokeo ya AMANI. Ila unaweza kuwa na UTULIVU bila ya kuwepo na AMANI. Ukienda gerezani mfano kuna UTULIVU wa hali ya juu na unauonekana dhahiri ila hakuna AMANI kwa sababu utulivu ule siyo matokeo ya AMANI. Iwe waitu umeeeeeeeelewa?
 
Back
Top Bottom