Richard
Platinum Member
- Oct 23, 2006
- 16,630
- 25,586
Nimeeleza kwenye moja ya mada za Britannica namna vyombo vya usalama vinavyofuatilia na kuteka watu wasipatikane kwa muda au hadi uchaguzi utakapokamilika. Mimi soma profile yangu nipo kama mchambuzi fulani hivi lakini baada ya kuona mambo fulani hivi imebidi niingie in details kuongea na Gen Z ili niwape moja mbili za kuwa uanaharakati wa kidijitali.
Kuna sehemu ntaingia more technical lakini mtanielewa naomba mnivumulie ndo mambo yalivyo wakutana na "somehow expert opinion".
Gen Z wamekuwa nyuma ya muda katika kufanya matayarisho na wamekosa stratejia ya namna ya kuandaa maandamano kama vile ilivyokuwa hivi karibuni katika nchi za Nepal na Madagascar, kwani maofisa usalama wa Tanzania walikwenda hatua tatu mbele kwa kuwahi kudhibiti njia za mawasiliano.
Hivyo inakuwa vigumu kutumia Tik-Tok, Facebook na X ambazo sasa zipo chini ya uangalizi maalum wa TCRA na hata huyu msichana aliekamatwa juzi aitwae Frida alitumia Tik-Tok ambayo imefanyiwa "phone tracking" hadi alipokamatwa.
Tokea mwanzo kulitakiwa kuwe na stratejia kwamba zipo njia tatu za mafanikio katika mitandao hii mitatu ambayo imetumika kifasaha kule Nepal na Madagascar. Njia ya kwanza ni majadiliano (Discussion) kupitia Discord ambapo katika majadiliano hayo huja mpango au "planning" ambapo coordinator anaanda vijana ambao tiyari kitambo walitakiwa wawe wamejiandaa kwa ajili ya siku hiyo au "D Day".
Discord yasisitiza kwenye kupanga au planning, kujadili au "debate" na kuandaa au organise katika muda huo yaani Real -Time and Live Stream Events", njia ya kukwepa udhibiti au bypass censorship ili kuweza kuingia barabarani kwa wakati mmoja.
Pia maandamano kukosa "Context" au sababu za msingi za kuandamana na kuleta vurugu, hii ni muhimu kwani Context ni tofauti katika kila nchi na kwa kwetu itawawia ugumu waandamanaji kwani tiyari raisi kasema yeye ni Amiri Jeshi Mkuu akimaanisha kuwa vyombo vyote vya usalama vimepewa nyenzo zote na zana kwa ajili ya kukabiliana na yeyote ataekwenda kuandamana na si kupiga kura.
Naomba nieleweke nikisema kukosa "Context" yaani mazingira yote, mawazo na mipango inopelekea kuwepo maandamano na hayo mazingira yakaeleweka yote kwa umakini. Hii ya kukosa "Context" imepelekea maandalizi ya maandamano haya kukosa support hata ya jumuiya ya kimataifa ambayo hadi sasa haijatoa kauli yoyote ile ya kuuliza au kuhoji hali ya utekaji na ukandamizaji inofanywa na vyombo vya usalama nchini.
Gen Z kukosa uwezo wa fedha na kutegemea VNP na bure nalo ni tatizo kwani VPN za bure hazina usalama wa uhakika na zipo wazi kwa ajili ya kuingiliwa na wataalam ambao wapo TCRA wanoweza kufanya "hacking" na "penetration" ili kuweza kuingilia mawasiliano na mitandao ya kijamii.
Kuzimwa kwa mitandao siku ya uchaguzi au kuwa limited kwa watu wachache tu itakuwa ni vigumu ka Gen Z kufanya matayarisho yoyote na mawasiliano baina yao. Mitandao ya Tik-Tok, Facebook na X yote ipo chini ya TCRA kwa ajili ya ufuatiliaji au "surveillance".
Watu/Jamii na vyombo vya habari.
Watanzania wengi wamekuwa katika hali ya kuamini kuwa amani iliyopo ndo hiyohiyo inowapa kula. Halikadhalika vyombo vya habari vimeacha majukumu yake mawili katika majukumu matatu yaani kuelmisha na kuhabarisha jamii na kubakia kufanya jukumu moja tu la kuhabarisha tena habari za upande mmoja tu.
Kwa mfano vyombo vya habari vikieleza tu kwamba fulani kakamatwa na polisi au leo Tundu Lissu kafikishwa mahakamani na kujaza mapicha, lakini vyashindwa kuleta vichwa vya habari za watu kutekwa. Kwahiyo habari zikiwa ni fulani kakamatwa au Tundu Lissu leo Kisutu habari zile zaogofya kwa umma au jamii itakayosoma na hovyo kuingiwa tiyari na hofu.
Kutokana na hayo ujumbe wa "October Tunatiki" umeingia kwenye jamii na pia miji mingi sasa hivi nchini ina ina mapicha kila kona ya mgombea mmoja tu ambae ndiye atarajiwa kushinda uchaguzi wa October na hivyo ndo jamii inavyoaminishwa.
Sasa ni nyenzo zipi ni muhimu kuzitumia katika kuandaa kufanya maandamano?
Katika mazingira magumu yalowekwa na vyombo vya ulinzi na usalama katika kudhibiti mitandao ya kijamii nyenzo pekee ambao zitatoa ulinzi na kufanya mawasiliano yawe salama ni zile ziitwazo Advance Cryptographic technology. Ingawa wamechelewa sana, Gen Z waweza kutumia njia za Signal na Tor ambazo zasaidia kuweza kutumia internet kufanya browsing na pia kuandaa shughuli za maandamano kwa usalama zaidi. Hii itafaa zaidi kwa baadae ikiwa hali ya October 29 itakuwa kama inavyokusudiwa.
Sina uhakika kama ntaeleweka lakini hali ndivyo ilivyo na nipo hapa Dodoma mjini naona mitandao imeanza kusumbua na hapa Dodoma Hoteli pana watu wengi sana wapitapita tu lakini hawanunui hata kahawa wala kashata wang'aang'aa macho tu.
Vijana wa GenZ wale "tech savvy" kazi kwenu wekeni mambo sawa nimewapa dondoo muhimu.
Kuna sehemu ntaingia more technical lakini mtanielewa naomba mnivumulie ndo mambo yalivyo wakutana na "somehow expert opinion".
Gen Z wamekuwa nyuma ya muda katika kufanya matayarisho na wamekosa stratejia ya namna ya kuandaa maandamano kama vile ilivyokuwa hivi karibuni katika nchi za Nepal na Madagascar, kwani maofisa usalama wa Tanzania walikwenda hatua tatu mbele kwa kuwahi kudhibiti njia za mawasiliano.
Hivyo inakuwa vigumu kutumia Tik-Tok, Facebook na X ambazo sasa zipo chini ya uangalizi maalum wa TCRA na hata huyu msichana aliekamatwa juzi aitwae Frida alitumia Tik-Tok ambayo imefanyiwa "phone tracking" hadi alipokamatwa.
Tokea mwanzo kulitakiwa kuwe na stratejia kwamba zipo njia tatu za mafanikio katika mitandao hii mitatu ambayo imetumika kifasaha kule Nepal na Madagascar. Njia ya kwanza ni majadiliano (Discussion) kupitia Discord ambapo katika majadiliano hayo huja mpango au "planning" ambapo coordinator anaanda vijana ambao tiyari kitambo walitakiwa wawe wamejiandaa kwa ajili ya siku hiyo au "D Day".
Discord yasisitiza kwenye kupanga au planning, kujadili au "debate" na kuandaa au organise katika muda huo yaani Real -Time and Live Stream Events", njia ya kukwepa udhibiti au bypass censorship ili kuweza kuingia barabarani kwa wakati mmoja.
Pia maandamano kukosa "Context" au sababu za msingi za kuandamana na kuleta vurugu, hii ni muhimu kwani Context ni tofauti katika kila nchi na kwa kwetu itawawia ugumu waandamanaji kwani tiyari raisi kasema yeye ni Amiri Jeshi Mkuu akimaanisha kuwa vyombo vyote vya usalama vimepewa nyenzo zote na zana kwa ajili ya kukabiliana na yeyote ataekwenda kuandamana na si kupiga kura.
Naomba nieleweke nikisema kukosa "Context" yaani mazingira yote, mawazo na mipango inopelekea kuwepo maandamano na hayo mazingira yakaeleweka yote kwa umakini. Hii ya kukosa "Context" imepelekea maandalizi ya maandamano haya kukosa support hata ya jumuiya ya kimataifa ambayo hadi sasa haijatoa kauli yoyote ile ya kuuliza au kuhoji hali ya utekaji na ukandamizaji inofanywa na vyombo vya usalama nchini.
Gen Z kukosa uwezo wa fedha na kutegemea VNP na bure nalo ni tatizo kwani VPN za bure hazina usalama wa uhakika na zipo wazi kwa ajili ya kuingiliwa na wataalam ambao wapo TCRA wanoweza kufanya "hacking" na "penetration" ili kuweza kuingilia mawasiliano na mitandao ya kijamii.
Kuzimwa kwa mitandao siku ya uchaguzi au kuwa limited kwa watu wachache tu itakuwa ni vigumu ka Gen Z kufanya matayarisho yoyote na mawasiliano baina yao. Mitandao ya Tik-Tok, Facebook na X yote ipo chini ya TCRA kwa ajili ya ufuatiliaji au "surveillance".
Watu/Jamii na vyombo vya habari.
Watanzania wengi wamekuwa katika hali ya kuamini kuwa amani iliyopo ndo hiyohiyo inowapa kula. Halikadhalika vyombo vya habari vimeacha majukumu yake mawili katika majukumu matatu yaani kuelmisha na kuhabarisha jamii na kubakia kufanya jukumu moja tu la kuhabarisha tena habari za upande mmoja tu.
Kwa mfano vyombo vya habari vikieleza tu kwamba fulani kakamatwa na polisi au leo Tundu Lissu kafikishwa mahakamani na kujaza mapicha, lakini vyashindwa kuleta vichwa vya habari za watu kutekwa. Kwahiyo habari zikiwa ni fulani kakamatwa au Tundu Lissu leo Kisutu habari zile zaogofya kwa umma au jamii itakayosoma na hovyo kuingiwa tiyari na hofu.
Kutokana na hayo ujumbe wa "October Tunatiki" umeingia kwenye jamii na pia miji mingi sasa hivi nchini ina ina mapicha kila kona ya mgombea mmoja tu ambae ndiye atarajiwa kushinda uchaguzi wa October na hivyo ndo jamii inavyoaminishwa.
Sasa ni nyenzo zipi ni muhimu kuzitumia katika kuandaa kufanya maandamano?
Katika mazingira magumu yalowekwa na vyombo vya ulinzi na usalama katika kudhibiti mitandao ya kijamii nyenzo pekee ambao zitatoa ulinzi na kufanya mawasiliano yawe salama ni zile ziitwazo Advance Cryptographic technology. Ingawa wamechelewa sana, Gen Z waweza kutumia njia za Signal na Tor ambazo zasaidia kuweza kutumia internet kufanya browsing na pia kuandaa shughuli za maandamano kwa usalama zaidi. Hii itafaa zaidi kwa baadae ikiwa hali ya October 29 itakuwa kama inavyokusudiwa.
Sina uhakika kama ntaeleweka lakini hali ndivyo ilivyo na nipo hapa Dodoma mjini naona mitandao imeanza kusumbua na hapa Dodoma Hoteli pana watu wengi sana wapitapita tu lakini hawanunui hata kahawa wala kashata wang'aang'aa macho tu.
Vijana wa GenZ wale "tech savvy" kazi kwenu wekeni mambo sawa nimewapa dondoo muhimu.