Ni vigumu kuwa tajiri

Ni vigumu kuwa tajiri

Kiplayer

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2018
Posts
1,355
Reaction score
2,261
Sio rahisi kuupata utajiri kama una sifa hizi:
1. Kuguswa kwa dhati na matatizo ya wanaokuzunguka yaani ndugu, jamaa na marafiki maana wapo wengi mno kabla haujawasaidia wote tayari ushakuwa maskini.

2. Kuwa mtu wa haki, walio na utajiri kabla yako watakushusha kwa kutumia uwezo wao maana ni lazima utawakwaza katika mitikasi yao kwa kupenda kwako haki.

Kuna namna fulani lazima misingi ivunjwe ili utajiri unukie.
 
Haki uinua taifa
Kutoa ni bora kuliko kupokea
 
Nionavyo mie mtu hawezi kuwa tajiri kama hana elimu na maarifa kuhusu pesa.kusaidia wengine hakuzuii mtu kuwa tajiri.
 
Nionavyo mie mtu hawezi kuwa tajiri kama hana elimu na maarifa kuhusu pesa.kusaidia wengine hakuzuii mtu kuwa tajiri.
Mwambie SHABIBY aanze kutoa lift kwenye mabasi yake kwa wasio na uwezo wa kulipa nauli Kwani wapo ambao hukwama kusafiri kwa sababu hawana uwezo kabisa wa kulipa nauli na wanahitaji msaada.
 
Ni kwel unayoyasema.
Ukitaka kuwa tajiri:-
1.uwe mkatili
2.mnyonyaji
3.usiwe na mazoea na watu
4.usiende kwenye kila harusi au msiba
5.usidharau hela hata kama ni buku moja
 
Mwambie SHABIBY aanze kutoa lift kwenye mabasi yake kwa wasio na uwezo wa kulipa nauli Kwani wapo ambao hukwama kusafiri kwa sababu hawana uwezo kabisa wa kulipa nauli na wanahitaji msaada.
Hata akitoa.lakini bado ana vyanzo vingine vya mapato vitavyomsaidia asiporomoke kwenye utajiri.
Utajiri hauji kwa kuwa mchoyo,kujinyima na ubahili.,huja kwa kumultiply vyanzo vya kukuongezea fedha
Ongeza asset punguza liabilities huku una nidhamu ya fedha.
 
#1 inanihusu sana. Kipato changu kidogo lakini najikuta natatua matatizo ya watu kiuchumi kila leo.
Hizi 10, 20, 30 nazitoa sana.
Wewe ni tajiri kwa mtazamo wangu.
Tajiri huridhika maskini haridhiki
 
Back
Top Bottom