BLACK MOVEMENT
JF-Expert Member
- Mar 11, 2020
- 5,487
- 14,064
Kwenye picha hapo ni Viongozi wa Serikali eti wanakagua maandalizi ya uwanja kwa ajili ya mei mosi. Hizi kwa mchi zote Duniani hata kule Somalia ni sherehe za wafanya kazi tu.
Bado unakuta wafanya kazi wana taguta mchawi wa masilahi yao?
Hakuna Taifa isipo kuwa Tanzania ambako Sherehe za wafanya kazi zinaandaliwa na Serikali. Mataifa yote isipo kuwa Tanzania sherehe huratibiwa na kuandaliwa na vyama vya wafanya kazi na sio lazima wamualike mkuu wa nchi wanaweza wasimualike kabisa na hakuna tatizo.
Sasa Tanzanua ni lazima Raisi wa nchi awepo kwenye sherehe, na sherehe zenyewe zimendaliwa na Seerikali yaani hata vyama vya wafanya kazi vinafanywa kualikwa na kupangiwa cha kuzungumza.
Nenda hapo Burundi nchi masikini kabisa sherehe za Mei mosi husimamiwa na vyama vya wafanyakazi wa Burundi na sio Serikali. Nenda Uganda, nend Kenya huko.
Halafu sherehe unakuta zimejaa wasanii wa kwenda kupoteza muda ikibakia lisaa ndio hotuba zinaanza za kusifu na kuabudu.
Huwezi ukawa mwajiri na hapo hapo ukawa unaandaa sherehe za waajiriwa wako ili wakutane wazungumzie matatizo yao.
Wafanya kazi sana watapewa chakula cha bure kesho sana itakuwa wali kuku na soda na watasahau matatizo yote na watashukuru kwa wali na soda kutoka Serikalini.