Ni sahihi kwa nguzo za eneo la vivuko kupakwa rangi ya bendera ya taifa?

Mnasihi

JF-Expert Member
Oct 9, 2013
7,659
6,910
Ni kuhusu hizi barabara maalum za mabasi ya mwendokasi.
Wiki iliyopita niliwaona vijana wakipaka rangi ya bendera ya Taifa la Tanzania kwenye nguzo zilizopo kwenye vivuko na zile za njia ya waenda kwa miguu yaani service road.
Wajenzi wa barabara hii ni sawa? Kwa uelewa wangu sehemu za barabara hasa vivuko hupakwa rangi ya pundamilia yaani nyeupe na nyeusi na hii ni dunia nzima.
Ni kwanini wajenzi hasa mainjinia wamelinyamazia hili? Au ni sawa kupaka rangi yoyote? Nisaidieni jibu.
 
Back
Top Bottom