Habari zenu wadau? Poleni na mihangaiko ya kimaisha!
Wadau, wiki jana nilikuja na mada hapa jamvini kuwa mchumba angu hataki kutoa kitu hadi siku nikimwoa.
Lakini nimegundua kuwa anaendelea kuchart na wanaume wengine. Nilivyomuuliza anadai kuwa hao ni wapenzi wake wa zamani hivyo bado hajawaambia kuwa anaolewa lakini nisijali atawapotezea taratibu! Kwani hawezi kuwatosa ghafla.
Nahisi nimevunjika moyo kabisa na nimeamua bora nimpotezee kabisa huyu binti.
Kabla sijachukua uamuzi tofauti naomba ushauri wenu!
Nawasilisha!!!