Tukielekea katika siku maalum ya kilele Cha sherehe ya kuadhimisha mwaka mmoja wa utawala wa raisi wa awamu ya sita nchini Tanzania,Nina maswali kadhaa kwa wadau wa siasa nchini.
Je ni raisi gani wa TANZANIA aliyewahi kufanya sherehe ya kuadhimisha mwaka mmoja tu wa madaraka yake?
Je Kuna kipi kipya ambacho kimefanyika katika mwaka mmoja huu ambacho hakikuanzishwa na mwenda zake?
Tatu je mwaka mmoja unatosha kweli kujipima kwa utendaji wa nchi kubwa Kama Tanzania yenye wakazi zaidi ya milioni 60.
Je, wananchi wanaichukuliaje hii sherehe na inamaslahi gani kwa wananchi wanyonge Kama Mimi?
Je, kutapatikana fursa ya kufanya tathmini ya kina ya kujikosoa ili kufanya maboresho katika nyanja mbalimbali za kiutendaji Kama serikali au shughuli itakuwa imemezwa na Sera za kusifu kila kitu?
Naombeni majibu wadau ili tusaidie kupeleka mbele gurudumu la Taifa tujadili kistaarabu tukitanguliza maslah mapana ya Taifa na uzalendo