Ni nini tofauti kati ya Visa na Passport?

Ni nini tofauti kati ya Visa na Passport?

UNAOTA WEWE.
wazee wetu wangekuwa wanajielewa wangekuwa wanabeba malighafi na kupeleka ulaya na marekani?.na wao kubebwa UTUMWA?
Ukoloni pia una faida zake.
Umetuletea ELIMU,nguo ,mitambo n.k
Big noooooooo! Ulilishwa matango pori hayoo! mpaka umevembewa, na bado umevembewa!... ndo tatizo ya shule za kata!! Sisi tulikuwa wajanja tangia Misri ya kale ni mali yetu ile! tunaitaka irudi,

Na hapo MIsri siyo mbali na Shinyanga yaani unatirirIka na mto Nile tuu mpaka victoria ! unajaa Maganzo! asa iweje wao watufundishe matumizi ya haya makitu wakati ni yetu? na Pharaos wa misri walikuwa wanazitumia Miaka dahari?

Hapo bado sijasema Middle east!
 
Ni nini tofauti Kati ya VISA na PASSPORT?

Je, mtu mmoja anaweza kumiliki passport zaidi ya moja?

Je, mtu mmoja anaweza kumiliki Visa zaidi ya moja?

Je, inawezekana mtu mmoja akamiliki passport na visa?
Ushashiba ugali wa shemeji yako sio
 
[emoji120][emoji120]
Kwa kuongezea, passport inatolewa na nchi yako, visa inatolewa na nchi unayotaka kwenda.

Kwa mfano wewe ni mtanzania, basi unapaswa kuwa na passport ya tanzania.

Kama unataka kwenda Marekani, basi wakati unafuatilia utaratibu pale ubalozi wa US, wataibandika visa ya Marekani kwenye passport yako.
(Baadhi ya nchi wanagonga muhuri tu na kujaza idadi ya siku utakazo kaa kwenye passport yako)

Kwahiyo passport ni utambulisho wako kama mtanzania huko ugenini, wakati visa ni kibali cha wewe kuingia na kufanya shughuli iliyokupeleka huko ugenini.

NB. Passport inakua na kurasa nyinginyingi, hivyo kila anaposafiri viza huwekwa kwenye ukurasa tofauti, hadi pale passport yako itakapo jaa.
 
Back
Top Bottom