Ni nani mtunzi wa wimbo, "Mabepari Walia" na yuko wapi?

Njaare

JF-Expert Member
Sep 26, 2010
1,081
275
Wanajamvi,
Kwa wale wanaokumbuka vizuri miaka ya sabini na themanini kulikuwa na huu wimbo, Mabepari walia, mabepari walia wakatiwa mirija. Walipotangaziwa, walipotangaziwa azimio la Arusha.
Wengi walisikitika, wengi walisikitika wakarukwa na akili ....................."

Naomba kuuliza ni nani mtunzi wa huu wimbo na yuko wapi kwa sasa?

Je, bado anashangilia kuona mabepari wakilia?

Je, ipo siku utaimbika tena hadharani?

Je, Kuna tofauti gani katu ya ubepari na uwekezaji?
 
dah, enzi hizo, vijana tunaitumikia nchi kwa imani na ushupavu kabisa.
 
Good question .. I would say!!!Mkuu wewe umeguswa na nini haswa mpaka kurusha uzi huu!!?
 
Good question .. I would say!!!Mkuu wewe umeguswa na nini haswa mpaka kurusha uzi huu!!?

Nilikuwa natafakari jinsi binadamu wanavyogeuka. Huu wimbo uliimbwa sana kwenye mikutano ya CCM. Sasa CCM hao hao ndo wamekuwa mawakala wa ubinafsishaji. Nikawa najiuliza hivi mtunzi haswa wa huu wimbo bado yuko CCM au naye kabadilika?
 
Wanajamvi,
Kwa wale wanaokumbuka vizuri miaka ya sabini na themanini kulikuwa na huu wimbo, Mabepari walia, mabepari walia wakatiwa mirija. Walipotangaziwa, walipotangaziwa azimio la Arusha.
Wengi walisikitika, wengi walisikitika wakarukwa na akili ....................."

Naomba kuuliza ni nani mtunzi wa huu wimbo na yuko wapi kwa sasa?

Je, bado anashangilia kuona mabepari wakilia?

Je, ipo siku utaimbika tena hadharani?

Je, Kuna tofauti gani katu ya ubepari na uwekezaji?

Mkuu umenikumbusha mbaaaaali! Umenikumbusha mirija, mabepari, makabaila.

Wawekezaji = Mabepari tena si mabepari tu bali Mabeberu (NB Ubeberu ni ubepari uliokomaa)
Makabaila = Kilimo kwanza
 
Huu mwimbo ulisaidia sana kuengeneza group la watu waitwao proletariants(walala hoi). Maana ubepari baada ya kufa watu wengi sana walipoteza kazi baada ya viwanda na mashamba ya bepari kuendeshwa na watu wasiokuwa na hekima ya kazi. Ubepari ndio uwekelezaji, hivyo tunapofatafuta wawekelezaji ina maana tunalilia ubepari urudishiwe heshima yake.

Kenya hawakumnyang'anya Lonho mali zake na hivyo huyu jamaa kaitangaza chai ya kenya duniani kote na inauzwa mpaka marekani katika maduka ya uthnic store. kweli kufanywa wajinga ni kosa baya sana . tulipokuwa tunaimba wimbo huu pale uwanja wa taifa hatukujua kuwa tunatanga kifo cha soko la ajira ambalo vijana wengi hivi sasa wanhaha kusaka kazi za viwanda na ujanzi.

Shilika la mwananchi engineerin Company(MECCO) lilikuwa na Bepari. Ona sasa walipokabidhiwa wazarendo, limeishia kutendeneza majeneza tuu na wala kazi za ujenzi haziaminiki tena,. halitoi ajira akabisaaa!
 
Huu mwimbo ulisaidia sana kuengeneza group la watu waitwao proletariants(walala hoi). Maana ubepari baada ya kufa watu wengi sana walipoteza kazi baada ya viwanda na mashamba ya bepari kuendeshwa na watu wasiokuwa na hekima ya kazi. Ubepari ndio uwekelezaji, hivyo tunapofatafuta wawekelezaji ina maana tunalilia ubepari urudishiwe heshima yake.

Kenya hawakumnyang'anya Lonho mali zake na hivyo huyu jamaa kaitangaza chai ya kenya duniani kote na inauzwa mpaka marekani katika maduka ya uthnic store. kweli kufanywa wajinga ni kosa baya sana . tulipokuwa tunaimba wimbo huu pale uwanja wa taifa hatukujua kuwa tunatanga kifo cha soko la ajira ambalo vijana wengi hivi sasa wanhaha kusaka kazi za viwanda na ujanzi.

Shilika la mwananchi engineerin Company(MECCO) lilikuwa na Bepari. Ona sasa walipokabidhiwa wazarendo, limeishia kutendeneza majeneza tuu na wala kazi za ujenzi haziaminiki tena,. halitoi ajira akabisaaa!

Wewe ni muongo wa kutupa. Mimi naishi Marekani, sijawahi kuona chai ya Kenya hapa. Huwa nanunua paketi nikienda Nairobi. Kamwe ubepari hautajenga Tanzania. Utajenge matabaka ya wamiliki na watwana. Ndiko huko tunakoelekea sasa kwa sera za CCM. Huwezi kutengeneza ajira bila viwanda. CCM imeua viwanda vyetu na kuwakabidhi wageni ambao wamevibadilisha kuwa go downs za kuagizia bidhaa za nje ambazo tungeweza kuzalisha wenyewe nchini. Aliyekuita muongo hajakosea kabisa.
 
Wewe ni muongo wa kutupa. Mimi naishi Marekani, sijawahi kuona chai ya Kenya hapa. Huwa nanunua paketi nikienda Nairobi. Kamwe ubepari hautajenga Tanzania. Utajenge matabaka ya wamiliki na watwana. Ndiko huko tunakoelekea sasa kwa sera za CCM. Huwezi kutengeneza ajira bila viwanda. CCM imeua viwanda vyetu na kuwakabidhi wageni ambao wamevibadilisha kuwa go downs za kuagizia bidhaa za nje ambazo tungeweza kuzalisha wenyewe nchini. Aliyekuita muongo hajakosea kabisa.

Kuna ubaya gani kukiwa na matabaka. Niko Marekani na tabaka langu ni la working class but I have everything I need.
 
Ameuliza mtunzi wa wimbo na je yupo wapi maana tungejua kuwa kama yupo tuweze kuwasiliana nae na kujua ana hali gani ya maisha je na bado ana msimamo wake uleule aliokuwa nao alipokuwa anaimba wimbo huo
 
Kuna ubaya gani kukiwa na matabaka. Niko Marekani na tabaka langu ni la working class but I have everything I need.

Naona Wamarekani mnatupa uzoefu wenu. Wewe uko working class ya huko Marekani na unapata kila kitu; je unaijua working class ya Tanzania? Unajua kuwa haipati mshahara bali inapata maskhara?
 
Kuna ubaya gani kukiwa na matabaka. Niko Marekani na tabaka langu ni la working class but I have everything I need.
Zakumi,
In a developed country tabaka si kitu kibaya sana kwa sababu working class ni kama middle class. Halafu hapa unakuta tabaka la wakulima wanatengeneza pesa kuliko working class. Lakini katika nchi zetu wakulima bado ni mafukara wa kutupwa. Tukifikia hali ambapo wakulima wetu wanaweza kumudu maisha, kusomesha watoto wao katika shule nzuri, kupata matibabu yanayokidhi, hapo tunaweza kusema hakuna ubaya na matabaka. Let Mitt Romney build his elevator for his cars, I do not care because I am living well on my salary.
 
Naona Wamarekani mnatupa uzoefu wenu. Wewe uko working class ya huko Marekani na unapata kila kitu; je unaijua working class ya Tanzania? Unajua kuwa haipati mshahara bali inapata maskhara?

Kimbunga,

Baba yangu alianza kazi na mshahara wa shiling 270 akiwa kama working class na alipata mahitaji yake. Na alistaafu akiwa afisa wa ngazi ya kati serikalini mwenye kupokea malaki lakini hakumudu maisha yake. Je ni kitu gani kilichofanya kupungua kwa thamani ya mishahara ya wafanyakazi? Jibu ni poor government policies. Policies zilizotaka kusawazisha, hizo hizo zikapunguza thamani ya mishahara.
 
Zakumi,
In a developed country tabaka si kitu kibaya sana kwa sababu working class ni kama middle class. Halafu hapa unakuta tabaka la wakulima wanatengeneza pesa kuliko working class. Lakini katika nchi zetu wakulima bado ni mafukara wa kutupwa. Tukifikia hali ambapo wakulima wetu wanaweza kumudu maisha, kusomesha watoto wao katika shule nzuri, kupata matibabu yanayokidhi, hapo tunaweza kusema hakuna ubaya na matabaka. Let Mitt Romney build his elevator for his cars, I do not care because I am living well on my salary.

Ukitaka kumjengea kila mkulima shule nzuri, zahanati nzuri na huduma zingine nzuri ni lazima uongeze ukubwa wa serikali. Ukubwa huo utaongeza matumizi ya serikali na kufanya serikali kushindwa kutoa huduma nzuri au kulipa mishahara mizuri. Matokeo yake unakuwa na wafanyakazi na wakulima mafukara.

Hivyo kutokujenga matabaka katika nchi kama Tanzania ni suala gumu. Na kutatuliwa kwake kunahitaji resources za mali na vichwa.
 
Ameuliza mtunzi wa wimbo na je yupo wapi maana tungejua
kuwa kama yupo tuweze kuwasiliana nae na kujua ana hali gani ya maisha
je na bado ana msimamo wake uleule aliokuwa nao alipokuwa anaimba wimbo
huo

siyo moses nnauye?
 
Huu mwimbo ulisaidia sana kuengeneza group la watu waitwao proletariants(walala hoi). Maana ubepari baada ya kufa watu wengi sana walipoteza kazi baada ya viwanda na mashamba ya bepari kuendeshwa na watu wasiokuwa na hekima ya kazi. Ubepari ndio uwekelezaji, hivyo tunapofatafuta wawekelezaji ina maana tunalilia ubepari urudishiwe heshima yake.

Kenya hawakumnyang'anya Lonho mali zake na hivyo huyu jamaa kaitangaza chai ya kenya duniani kote na inauzwa mpaka marekani katika maduka ya uthnic store. kweli kufanywa wajinga ni kosa baya sana . tulipokuwa tunaimba wimbo huu pale uwanja wa taifa hatukujua kuwa tunatanga kifo cha soko la ajira ambalo vijana wengi hivi sasa wanhaha kusaka kazi za viwanda na ujanzi.

Shilika la mwananchi engineerin Company(MECCO) lilikuwa na Bepari. Ona sasa walipokabidhiwa wazarendo, limeishia kutendeneza majeneza tuu na wala kazi za ujenzi haziaminiki tena,. halitoi ajira akabisaaa!

mkuu una maana kenya kuna ajira za kumwaga eeh! shituka wewe! huwezi kupata eneo la duara bila kuishirikisha pai, shirikisha ubongo wako.
 
Ukitaka kumjengea kila mkulima shule nzuri, zahanati nzuri na huduma zingine nzuri ni lazima uongeze ukubwa wa serikali. Ukubwa huo utaongeza matumizi ya serikali na kufanya serikali kushindwa kutoa huduma nzuri au kulipa mishahara mizuri. Matokeo yake unakuwa na wafanyakazi na wakulima mafukara.

Hivyo kutokujenga matabaka katika nchi kama Tanzania ni suala gumu. Na kutatuliwa kwake kunahitaji resources za mali na vichwa.
Zakumi,
I would do it without increasing the size of government. Ningepunguza marupurupu wanayojilipa viongozi, kuongeza kodi na kufuta misamaha ya kodi. Can you imagine kampuni kama Vodacom mpaka sasa hawalipi kodi? What the hell is this?
 
Wanajamvi,
Kwa wale wanaokumbuka vizuri miaka ya sabini na themanini kulikuwa na huu wimbo, Mabepari walia, mabepari walia wakatiwa mirija. Walipotangaziwa, walipotangaziwa azimio la Arusha.
Wengi walisikitika, wengi walisikitika wakarukwa na akili ....................."

Naomba kuuliza ni nani mtunzi wa huu wimbo na yuko wapi kwa sasa?

Je, bado anashangilia kuona mabepari wakilia?

Je, ipo siku utaimbika tena hadharani?

Je, Kuna tofauti gani katu ya ubepari na uwekezaji?

Mmh! Mkuu una kumbukumbu nzuri, ubarikiwe. Mtunzi wa wimbo huo hata mie simjuhi japo nimeimba wimbo huo sana nikiwa primary kwenye miaka ya70s. Kuna mwingine: 'Kaburu matata huyo...
 
Back
Top Bottom