Consigliere
Platinum Member
- Sep 9, 2010
- 12,690
- 26,567
Hivi kuna uwezekano serikali ikaufungia mtandao wa 'X' (Twitter), lakini bado viongozi wake wakawa wanaendelea kuutumia kwa ku post na kufiatilia taarifa mbalimbali ikiwemo kuendelea kufanya online engagements?
Kabla ya kuufungia huo mtandao kuna taarifa yoyote rasmi serikali iliitoa kwa wananchi wake na watumishi wa umma kwamba serikali ime ban mtandao huo? Kwa muda gani? na sababu zipi? Au kuna watu tu wakajiamulia kuufunga?
Je viongozi na watu wengine wanaoendelea ku post kule, wenyewe wanatumia njia gani kuweza kuutumia mtandao huo? Kwanini? Kulikuwa na ulazima gani wa kuufunga?
Vipi kuhusu watu wafanyao biashara kupitia mtandao huo? ndiyo wahesabia kuwa maduka yao yamefungwa? Vipi hizo sababu zilizopelekea mtandao huo kufungwa hazipo kule TikTok , Instagram na facebook?
Kwa hali hii si ni rahisi sana Tanzania ikarudishwa gizani? Vipi kama vijana wa mataifa shindani wataitumia hiyo kama fursa ya kuwaondoa watanzania mitandaoni na kupunguza ushindani wa fursa za kimtandao?
Kabla ya kuufungia huo mtandao kuna taarifa yoyote rasmi serikali iliitoa kwa wananchi wake na watumishi wa umma kwamba serikali ime ban mtandao huo? Kwa muda gani? na sababu zipi? Au kuna watu tu wakajiamulia kuufunga?
Je viongozi na watu wengine wanaoendelea ku post kule, wenyewe wanatumia njia gani kuweza kuutumia mtandao huo? Kwanini? Kulikuwa na ulazima gani wa kuufunga?
Vipi kuhusu watu wafanyao biashara kupitia mtandao huo? ndiyo wahesabia kuwa maduka yao yamefungwa? Vipi hizo sababu zilizopelekea mtandao huo kufungwa hazipo kule TikTok , Instagram na facebook?
Kwa hali hii si ni rahisi sana Tanzania ikarudishwa gizani? Vipi kama vijana wa mataifa shindani wataitumia hiyo kama fursa ya kuwaondoa watanzania mitandaoni na kupunguza ushindani wa fursa za kimtandao?