๐—ก๐—ถ ๐—บ๐—ฎ๐—ธ๐—ผ๐˜€๐—ฎ ๐—ฅ๐—ฎ๐—ถ๐˜€ ๐—ธ๐˜‚๐—ถ๐—ป๐—ด๐—ถ๐—ฎ ๐—ป๐—ฎ ๐—บ๐—ฎ๐—บ๐—น๐—ฎ๐—ธ๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ๐—ธ๐—ฒ ๐˜†๐—ฎ ๐—จ๐—ฟ๐—ฎ๐—ถ๐˜€ ๐—ธ๐—ฎ๐—ป๐—ถ๐˜€๐—ฎ๐—ป๐—ถ

Mdude_Nyagali

Member
Dec 11, 2022
60
1,237
Jana wakati wa ibada ya kumuingiza kazini Askofu Malasusa nilishangaa kuona tena Rais Samia akiingia na jukwaa lake la kimamlaka pamoja na kiti chake cha kimamlaka licha ya kwamba tulishawahi kuonya huko nyuma kuwa ni makosa. Kanisani au msikiti ni sehemu za ibada takatifu na wala hatupaswi kuingia na vyeo hata kama tumealikwa maana pale mkuu ni mmoja tu Mungu Mwenyezi.

Kwa bahati mbaya sasa madhabahu ya kanisa yamegeuzwa majukwaa ya kimamlaka ya serikali kiasi kwamba Rais anafika hapo na kutoa tamko au amri za kiserikali kinyume kabisa na kanuni za kikristo.

Mfalme Suleiman pamoja na kwamba yeye ndiye aliyejenga hekalu la Mungu pale Jerusalem lakini hakuwahi kuingia na ufalme wake hekaluni. Mfalme Suleiman aliingia hekaluni na kusali kama muumini wa kawaida.

Mwaka 734 - KK mfalme Uzia alipigwa ukoma na Mungu baada ya kulazimisha kupanda madhabahuni wakati anajua hakuwa na hiyo mamlaka ya kimungu isipokuwa wana wa haruni na walawi wengine. Pamoja na kwamba mfalme Uzia alionywa kwamba alikuwa anafanya makosa alipuuza maonyo hayo kisha kupanda madhabahuni. Mfalme Uzia alipigwa ukoma mpaka kifo chake huku akikaa peke yake katika nyumba ya kutengwa kama ilivyokuwa desturi zamani za kale mtu mwenye ukoma kutengwa.

Leo baada ya miaka 2700+ kupita baada ya tukio la mfalme Uzia tunaona Rais Samia anaingia kanisani na mamlaka yake ya kiserikali hata mbele ya madhabahu. Kwani kulikuwa na ubaya gani Rais angeingia kama muumini mwingine akakalia viti kama waalikwa wengine?

Kuingia na jukwaa la kimamlaka maana yake unaingia na mamlaka yako kanisani kitu ambacho ni kosa kubwa sana kwani kanisani pana mamlaka zake za kimungu. Tulijaribu kuonya Rais alipoingia na kiti cha kimamlaka katika kanisa la Roma mwaka jana lakini tunaona jambo hili linajirudia. Najua mliomwalika hamuwezi kukemea au kukataza jambo hili kwa sababu labda mnamuogopa au anatoa michango mingi kwenu au anawapa misamaha ya kodi lakini sisi wengine tutakemea maana Yesu Kristo alitusisitiza kuhubiri kweli.

Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
GridArt_20240122_80647077~2.jpg
 
Nadhani sio busara kuonekana unapinga Kila kitu hata visivyo na maana.
Kanisa ni madhabahu, hatukumuona Raisi Madhabahuni, hatukumuona aki dictate ni Nini kifanyike Ibadani. Mama wa watu alitegewa eneo lake la kukaa na itifaki na wageni wake huku Wenye ibaada Yao wakiendesha kwa mujibu wa Taratibu zao. Yeye akaja akapewa nafasi ya salamu mwishoni kabisa kama mgeni wa heshma katika tendo la kumsimika Mkuu wa kanisa.

Pale pia tuliona wageni wengi tofauti tofauti na hata mwakilishi wa Mufti alikuwapo, Hilo pia ni kosa?

Sikuona Jinsi gani hiyo Mamlaka ya Uraisi ilivyoathiri ibada.
 
Tuelimishe kupitia biblia dhidi ya kosa hilo, ili tuone hauna chuki binafsi ndani ya mada yako.
 
Tanzania serikali haifuatilii wala kujali kanuni za "Separation of Religion and State".

Kibaya zaidi, hata upinzani nao haujali wala kufuatilia.

Matokeo yake Mbowe anamualika Rais kwenye kuchangia kujenga kanisa la kwa kina Mbowe.

Halafu wapinzani wanalalamika rais kuingia na mamlaka ya urais kanisani.
 
Pale haikuwa ibada pekee ilikuwa sherehe ya kusimika mtu tofautisha ibada pekee na sherehe

Alialikwa kama Raisi Sio muumini
 
Nadhani sio busara kuonekana unapinga Kila kitu hata visivyo na maana.
Kanisa ni madhabahu, hatukumuona Raisi Madhabahuni, hatukumuona aki dictate ni Nini kifanyike Ibadani. Mama wa watu alitegewa eneo lake la kukaa na itifaki na wageni wake huku Wenye ibaada Yao wakiendesha kwa mujibu wa Taratibu zao. Yeye akaja akapewa nafasi ya salamu mwishoni kabisa kama mgeni wa heshma katika tendo la kumsimika Mkuu wa kanisa.

Pale pia tuliona wageni wengi tofauti tofauti na hata mwakilishi wa Mufti alikuwapo, Hilo pia ni kosa?

Sikuona Jinsi gani hiyo Mamlaka ya Uraisi ilivyoathiri ibada.
Rais kuwa mgeni wa heshima kwenye shughuli ya kumsimika Mkuu wa Kanisa ni kuvunja kanuni za "Separation of Religion and State".

Huo ndio mwanzo wa Rais kutumia makanisa katika kampeni za kisiasa.
 
Nadhani sio busara kuonekana unapinga Kila kitu hata visivyo na maana.
Kanisa ni madhabahu, hatukumuona Raisi Madhabahuni, hatukumuona aki dictate ni Nini kifanyike Ibadani. Mama wa watu alitegewa eneo lake la kukaa na itifaki na wageni wake huku Wenye ibaada Yao wakiendesha kwa mujibu wa Taratibu zao. Yeye akaja akapewa nafasi ya salamu mwishoni kabisa kama mgeni wa heshma katika tendo la kumsimika Mkuu wa kanisa.

Pale pia tuliona wageni wengi tofauti tofauti na hata mwakilishi wa Mufti alikuwapo, Hilo pia ni kosa?

Sikuona Jinsi gani hiyo Mamlaka ya Uraisi ilivyoathiri ibada.
At last a voice of reason.Rais alikuwa kanisani kama nani?Kupinga na kukosoa bila mantiki ni ujinga.
Hasa ikitiliwa maanani kwamba anayekosoa anajifanya mwanaharakati wa kupinga pinga.
 
Tanzania serikali haifuatilii wala kujali kanuni za "Separation of Religion and State".

Kibaya zaidi, hata upinzani nao haujali wala kufuatilia.

Matokeo yake Mbowe anamualika Rais kwenye kuchangia kujenga kanisa la kwa kina Mbowe.

Halafu wapinzani wanalalamika rais kuingia na mamlaka ya urais kanisani.
Kumbe kaudini udini kamewateka watu wengi sana Nchi hii. !
Tuzungumzie zaidi matatizo yanayotukabili Nchini kila siku !

Umeme Maji Barabara and so on and so forth !!
Hii Mamlaka kuingia Kanisani au Msikitini hii haituathiri kwa namna yeyote whatsoever !! ๐Ÿ™๐Ÿ™๐Ÿ™
 
Jana wakati wa ibada ya kumuingiza kazini Askofu Malasusa nilishangaa kuona tena Rais Samia akiingia na jukwaa lake la kimamlaka pamoja na kiti chake cha kimamlaka licha ya kwamba tulishawahi kuonya huko nyuma kuwa ni makosa. Kanisani au msikiti ni sehemu za ibada takatifu na wala hatupaswi kuingia na vyeo hata kama tumealikwa maana pale mkuu ni mmoja tu Mungu Mwenyezi.

Kwa bahati mbaya sasa madhabahu ya kanisa yamegeuzwa majukwaa ya kimamlaka ya serikali kiasi kwamba Rais anafika hapo na kutoa tamko au amri za kiserikali kinyume kabisa na kanuni za kikristo.

Mfalme Suleiman pamoja na kwamba yeye ndiye aliyejenga hekalu la Mungu pale Jerusalem lakini hakuwahi kuingia na ufalme wake hekaluni. Mfalme Suleiman aliingia hekaluni na kusali kama muumini wa kawaida.

Mwaka 734 - KK mfalme Uzia alipigwa ukoma na Mungu baada ya kulazimisha kupanda madhabahuni wakati anajua hakuwa na hiyo mamlaka ya kimungu isipokuwa wana wa haruni na walawi wengine. Pamoja na kwamba mfalme Uzia alionywa kwamba alikuwa anafanya makosa alipuuza maonyo hayo kisha kupanda madhabahuni. Mfalme Uzia alipigwa ukoma mpaka kifo chake huku akikaa peke yake katika nyumba ya kutengwa kama ilivyokuwa desturi zamani za kale mtu mwenye ukoma kutengwa.

Leo baada ya miaka 2700+ kupita baada ya tukio la mfalme Uzia tunaona Rais Samia anaingia kanisani na mamlaka yake ya kiserikali hata mbele ya madhabahu. Kwani kulikuwa na ubaya gani Rais angeingia kama muumini mwingine akakalia viti kama waalikwa wengine?

Kuingia na jukwaa la kimamlaka maana yake unaingia na mamlaka yako kanisani kitu ambacho ni kosa kubwa sana kwani kanisani pana mamlaka zake za kimungu. Tulijaribu kuonya Rais alipoingia na kiti cha kimamlaka katika kanisa la Roma mwaka jana lakini tunaona jambo hili linajirudia. Najua mliomwalika hamuwezi kukemea au kukataza jambo hili kwa sababu labda mnamuogopa au anatoa michango mingi kwenu au anawapa misamaha ya kodi lakini sisi wengine tutakemea maana Yesu Kristo alitusisitiza kuhubiri kweli.

Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.View attachment 2879323
Kaalikwa Rais wa Tanzania.

Hakwenda kama muumini wa kanisa.
 
Sawa siku nyingine ataigiza kaanguka kwa maombi ili uone kaacha mamlaka nje
 
Alitaka akasali!!
Ujuaji mwingi kwa vijana unawafanya wakosoe hata vitu visivyo na makosa.

Mimi ningeshangaa kama angeenda kuswali msikitini kama kawaida halafu akaenda na kiti chake cha mamlaka. Sasa mtu amealikwa kama Rais wa JMT halafu akaenda hivyo kama Rais, unalalamika nini?

Kuzoea kukosoa sana na kupenda kusifia sana kunaua uwezo wa kufikiri wa watu.
 
Rais kuwa mgeni wa heshima kwenye shughuli ya kumsimika Mkuu wa Kanisa ni kuvunja kanuni za "Separation of Religion and State".

Huo ndio mwanzo wa Rais kutumia makanisa katika kampeni za kisiasa.
Hivi taasisi za dini huwa sinakosa wageni rasmi wanaofanana na itikadi zao mpaka wamwalike mwanasiasa?

Mwisho wa siku theme ye sherehe inaharibika kama hivi leo.
 
Hivi taasisi za dini huwa sinakosa wageni rasmi wanaofanana na itikadi zao mpaka wamwalike mwanasiasa?

Mwisho wa siku theme ye sherehe inaharibika kama hivi leo.
Sherehe haiwezi kuharibiwa na baadhi ya watu wenye mitazamo yao ya binafsi yao !! ๐Ÿ™๐Ÿ™

Maisha ni kukubali kutokubaliana !
Na maisha yanaendelea !! ๐Ÿ™๐Ÿ™
 
Wabongo mna nongwa kweli. Ndio maana anawapuuza tu.

Unajua ukiwa mtu wa kulalamika kila kitu basi watu wanakuchukulia kuwa wewe ni malalamishi na wanakupuuza.

Hata siku ukilalamikia kitu cha msingi utaonekana ni ulalamishi wako wa siku zote usio na maana.
 
Jana wakati wa ibada ya kumuingiza kazini Askofu Malasusa nilishangaa kuona tena Rais Samia akiingia na jukwaa lake la kimamlaka pamoja na kiti chake cha kimamlaka licha ya kwamba tulishawahi kuonya huko nyuma kuwa ni makosa. Kanisani au msikiti ni sehemu za ibada takatifu na wala hatupaswi kuingia na vyeo hata kama tumealikwa maana pale mkuu ni mmoja tu Mungu Mwenyezi.

Kwa bahati mbaya sasa madhabahu ya kanisa yamegeuzwa majukwaa ya kimamlaka ya serikali kiasi kwamba Rais anafika hapo na kutoa tamko au amri za kiserikali kinyume kabisa na kanuni za kikristo.

Mfalme Suleiman pamoja na kwamba yeye ndiye aliyejenga hekalu la Mungu pale Jerusalem lakini hakuwahi kuingia na ufalme wake hekaluni. Mfalme Suleiman aliingia hekaluni na kusali kama muumini wa kawaida.

Mwaka 734 - KK mfalme Uzia alipigwa ukoma na Mungu baada ya kulazimisha kupanda madhabahuni wakati anajua hakuwa na hiyo mamlaka ya kimungu isipokuwa wana wa haruni na walawi wengine. Pamoja na kwamba mfalme Uzia alionywa kwamba alikuwa anafanya makosa alipuuza maonyo hayo kisha kupanda madhabahuni. Mfalme Uzia alipigwa ukoma mpaka kifo chake huku akikaa peke yake katika nyumba ya kutengwa kama ilivyokuwa desturi zamani za kale mtu mwenye ukoma kutengwa.

Leo baada ya miaka 2700+ kupita baada ya tukio la mfalme Uzia tunaona Rais Samia anaingia kanisani na mamlaka yake ya kiserikali hata mbele ya madhabahu. Kwani kulikuwa na ubaya gani Rais angeingia kama muumini mwingine akakalia viti kama waalikwa wengine?

Kuingia na jukwaa la kimamlaka maana yake unaingia na mamlaka yako kanisani kitu ambacho ni kosa kubwa sana kwani kanisani pana mamlaka zake za kimungu. Tulijaribu kuonya Rais alipoingia na kiti cha kimamlaka katika kanisa la Roma mwaka jana lakini tunaona jambo hili linajirudia. Najua mliomwalika hamuwezi kukemea au kukataza jambo hili kwa sababu labda mnamuogopa au anatoa michango mingi kwenu au anawapa misamaha ya kodi lakini sisi wengine tutakemea maana Yesu Kristo alitusisitiza kuhubiri kweli.

Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.View attachment 2879323
Badala tukocentrate na mambo ya msingi tunahangaika had na mambo madogo madogo!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom