Tetty
JF-Expert Member
- Jan 6, 2012
- 26,356
- 21,390
Ndiyo maana Kaka yangu Kahtan ,bado tupo pale pale dini hizi mbili haziwezi kuwa sawa na bado kama mkristu ninaamini YESU ni MUNGU na hauwezi kunibadilisha ndiyo IMANI yangu tunachotakiwa kufanya ni kuheshimiana au tuseme tukubali katika kutokubaliana.Tunachotakiwa kufanya kwa sasa siyo kulumbana sidhani kama kuna mfumo kristu hichi kitu hakuna.Shida,ajira,afya,umaskini watanzania bila kujali imani zao wanavikosa.Tunachotakiwa kupopiga vita ni RUSHWA,UFISADI na kutumika mali za umma hovyo na kulinda maliasili zetu.Bado nasisitiza hatuhitaji Dini kwenye hili bali umoja wa watanzania.Kwangu mie naweka UTAIFA kwanza na ninaheshimu IMANI ya mtu mwingine.