Mwizukulu mgikuru
JF-Expert Member
- Oct 21, 2021
- 4,735
- 11,090
Naombeni mnipe majibu, ni kweli mwanamke hawezi kumpenda mwanaume fukara? Lakini mbona baba yangu alipendwa na mama yangu akiwa hana kitu, mimi nimezaliwa mpaka nafikia umri wa kujitambua nimekuta baba yangu anaishi kwao, yaani kwenye nyumba ya wazazi wake nayo ilikuwa chumba kimoja na sebure.
Lakini mbona ndoa za uswahili asilimia kubwa zinadumu ukilinganisha na zile za ushuwani? yaani unakuta mtu anaishi na mke wake wamepanga chumba kimoja na wanaishi maisha ya kuungaunga Lakini wanadumu wanazaa watoto wanafanikiwa kujijenga na kuwa na makazi yao.
Lakini mbona mwanamke huyohuyo unaweza kumpa kila kitu na bado akaenda kumpa penzi fukara?
Lakini mbona ndoa za uswahili asilimia kubwa zinadumu ukilinganisha na zile za ushuwani? yaani unakuta mtu anaishi na mke wake wamepanga chumba kimoja na wanaishi maisha ya kuungaunga Lakini wanadumu wanazaa watoto wanafanikiwa kujijenga na kuwa na makazi yao.
Lakini mbona mwanamke huyohuyo unaweza kumpa kila kitu na bado akaenda kumpa penzi fukara?