cheusimangala
JF-Expert Member
- Feb 27, 2010
- 2,585
- 497
kuna mkaka mmoja alimtogoza dada mmoja mwaka mmoja na nusu uliopita lkn huyo dada akamkatalia kistaarabu tu,sasa pamoja na muda mrefu kuwa umepita lkn huyo kaka kila siku anampigia huyu dada simu wkt wowote anapojisikia hata usiku wa maneno akimbembeleza na wkt mwingine kumuandikia dada sms za mapenzi as if ni wapenzi na dada hawezi kubadili namba yake na pamoja na kaka kuonywa mara kibao lakini hakomi,mbaya zaidi huyo kaka akijua kuna kijana anayemfuatilia huyo dada au ana uhusiano wowote wa karibu basi anamfuata huyo kijana na kumtishia kua akae mbali na huyo dada akidai kuwa huyo dada ni mchumba wake, na ameshamtishia kaka mmoja aliyekua akimfuatilia huyo dada kwa kutaka kumgonga kwa gari yake,pia amekwenda hadi nyumbani kwa mama wa huyo dada na kulia machozi kama mtoto mdogo na kumtishia huyo mama wa huyo dada kuwa akisikia amejinyonga basi ajue ni kwa sbb binti yake kamkataa.pia anapita kila mahali akitangaza kuwa huyo dada ni mchumba wake,na vitu vingi kama hivyo,SASA WADAU HIVI HUYU KAKA NI AMEKUA CRAZY IN LOVE AU ANAMKOMOA HUYU DADA!!