Ni Izato, soyo tena Mbenge

Ni Izato, soyo tena Mbenge

Izato

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2019
Posts
5,134
Reaction score
11,071
Imwe, Igele, Izato,..
kwa kabila la Wakikuyu, Ila kwa lugha ya Kiswahili maana yake ni Moja, Mbili, Tatu,...

Kwa nini iwe Izato na wala siyo tena Mbenge kama vile ilivyokuwa hapo awali!?

Sababu kubwa ni baada ya kubaini kuna huduma ya kiroho ya Kikristo yenye kuongozwa na Mch. Mbenge. Kwa muktadha huo nimeona ni vyema kubadili jina hilo la kificho na kuchagua jingine jipya lenye utambulisho wa nambari 3.

Namba 3 katika tafsiri ya lugha za kibiblia, ikiwa ni namba yenye kubeba maana ya kinabii ya jambo lenye fumbo la kinabii ambalo linakwenda kufikia ukamilifu wake wote katika hali ya kimwili, yaani fulfillment.

Ijapokuwa jina Mbenge niliilitumia mahususi lilkiwa limebeba code fulani muhimu nyuma yake kwa tafsiri ya fumbo la kiimani, lakini inanipasa sasa nilibadilishe ili kuzidi kuenzi thamani ya huduma ya kichungaji, ya kusambaza Injili, pamoja na ile ya msalaba.

Kwa hiyo basi niwatambulishe rasmi wana jukwaa kuwa, haitakuwa tena Mbenge, bali sasa ni Izato, wakati dunia ikitarajia kushuhuhudia sehemu kubwa ya unabii ukitimia kupitia nambari 3.
 
Mods naomba kichwa cha habari kisomeke Siyo na si Soyo
 
Katika Injili ya Bwana Yesu Kristo tunaweza kujifunza matumizi ya Namba 3. Hii ni namba yenye kuonyesha kusudio la Mungu linalokwenda kutimilika kama ambavyo lilivyokusudiwa.

Mathalani, tukio zima la kusulubiwa kwa Bwana Yesu, hilo lilikuwa ni kusudio la Mungu mwenyewe. Nalo linapata kufikia utimilivu wake wote kupitia nambari 3

Kumbuka Petro alimkana Bwana Yesu mara 3 rejea Marko 14:66-72

Bwana Yesu aliomba mara 3 muda mfupi kabla ya kukamatwa na kwenda kusulubishwa, rejea Marko 14:32-41

Jina “YESU WA NAZARETH MFALME WA WAYAHUDI” Liliwekwa msalabani kwa lugha 3 rejea Yohana 19;19-20.

Bwana Yesu alikaa msalabani kwa masaa 3 kutoka saa 6 mpaka saa 9 mpaka pale alipokata roho rejea Mathayo 27:45

Kwa matukio yote hayo machache hii namba 3 inayojirudirudia kwa kusudi maalum.

Namba 3 hapa inatuonyesha kwamba tukio lote la kusulubiwa kwa Bwana Yesu ilikuwa kwa Makusudi ya Mungu juu ya wokovu wa wanadamu dhidi ya kifo, mauti, na kizimu, na jukumuu hili kuuili lipate kutimia Mungu kajidhihiriisha kwa wanadamu kwa kupitia ofisi zake ama hadhi zake kuu 3, yaani Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu
 
Katika Injili ya Bwana Yesu Kristo tunaweza kujifunza matumizi ya Namba 3. Hii ni namba yenye kuonyesha kusudio la Mungu linalokwenda kutimilika kama ambavyo lilivyokusudiwa.

Mathalani, tukio zima la kusulubiwa kwa Bwana Yesu, hilo lilikuwa ni kusudio la Mungu mwenyewe. Nalo linapata kufikia utimilivu wake wote kupitia nambari 3

Kumbuka Petro alimkana Bwana Yesu mara 3 rejea Marko 14:66-72

Bwana Yesu aliomba mara 3 muda mfupi kabla ya kukamatwa na kwenda kusulubishwa, rejea Marko 14:32-41

Jina “YESU WA NAZARETH MFALME WA WAYAHUDI” Liliwekwa msalabani kwa lugha 3 rejea Yohana 19;19-20.

Bwana Yesu alikaa msalabani kwa masaa 3 kutoka saa 6 mpaka saa 9 mpaka pale alipokata roho rejea Mathayo 27:45

Kwa matukio yote hayo machache hii namba 3 inayojirudirudia kwa kusudi maalum.

Namba 3 hapa inatuonyesha kwamba tukio lote la kusulubiwa kwa Bwana Yesu ilikuwa kwa Makusudi ya Mungu juu ya wokovu wa wanadamu dhidi ya kifo , mauti, na kuzimu, na jukumuu hili kuu lipate kutimia Mungu kajidhirisha kwetu kwa ofisi ama hadhi kuu 3, yaani Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu
 
Back
Top Bottom