Ni hatari Jeshi la Polisi kuzagaa mtaani

Ni hatari Jeshi la Polisi kuzagaa mtaani

Eti yamefanikiwa! Lengo la maandamano haya ni KUMTOA RAIS MADARAKANI sasa yamefanikiwa AMETOKA MADARAKANI? Hata kubadilika hatabadilika ataendelea na moto ule ule.
Kila zama na wakati wake badilikeni
 
Eti yamefanikiwa! Lengo la maandamano haya ni KUMTOA RAIS MADARAKANI sasa yamefanikiwa AMETOKA MADARAKANI? Hata kubadilika hatabadilika ataendelea na moto ule ule.
Kila zama na wakati wake badilikeni
 
Maandamano Ya jeshi la polisi yanaendelea Leo siku Ya pili huku alieamulisha akiva bado yuko huko Marekani

Mimi nitoe tafadhali Kwa polisi mkitoka huko msije kutusumbua kutuomba omba bia kwenye Baar maana mmezoea Sana kuja Baar kutuomba omba bia mkimaliza maandamano mange kimambi awalipe kabisa posho ili tupumue Leo na kuombwa ombwa offa Ya bia maaana kwenye Baar mnakera Sana

😀😀😀
 
Kuna Athari kubwa sana kwa Jeshi la Polisi kuzunguka na magari na silaha mtaani. Nimejaribu kuainisha sababu kadhaa chache;

Moja, lengo lao ni kuleta hofu kwa Wananchi lakini hali hii hujenga usugu na mazoea kuwaona kuwa si lolote si chochote. Mbinu hii ni mbaya sana.

Pili, huweza kuwajengea wananchi ujasiri wa kukabiliana nao, ni hatari sana maana kama kweli atakuepo mtu mwenye nia ovu, anaweza kuangalia the way wanavyojipambanua na mtu huyo akajenga namna ya kuwashambulia Askari. Kwa mfano, Jana nimekutana nao kigogo, wako kwenye gari kama sita! Ni rahisi sana kushambuliwa kama atakuepo mtu mwenye nia ovu.

Tatu, ili uweze kushambuliwa vizuri ni lazima umjue vizuri adui yako, yale magari yao ambayo wamejifunga mikanda ikitokea wamefanyiwa ambush watakumbuka saa ngapi kufungua seat belts na kushambulia?

Nne, askari wa Jana wengi hawana miili ya kazi, sijajua upande wa akili, lakini kwa miili ile kweli wananchi wakilianzisha hakuna atakayepona. Wajitahidi mazoezi.

Tano, ni wachache sana! Wananchi wa Kigogo peke yao wangeweza kuziba barabara na kuwaweka mtu kati tungepoteza Askari wetu kizembe sana.

Ushauri wangu, kama lengo ni kuwatisha wananchi basi tujue tumepanga mkakati wa hovyo saana maana unampa adui ABC kuhusu wewe.

Tujitafakari, umwagaji damu ni hatari kwetu sote. Tuipende nchi yetu
Ficha Upumbavu wako
 
Suala sio maandamano kuwepo au kutokuwepo. Hizi harakati za hawa polisi zinatumia pesa za walipa kodi ambazo zingeweza kusaidia maeneo mengine yenye tija na kipaumbele kwa taifa.

Haya mambo mwisho wa siku yanazaa utata wa 1.5 T.
Hata polisi pia wanakatwa kodi mkuu
 
Najua saaana kuwa ni waoga, kama kweli wanajiaminisha si wangekaa wasubiri kama kuna maandamano au lah? Sioni sababu ya kupoteza resources
Kwamba wasubiri kwamba madhara yatokee kwanza ndo wareact...!???hey
 
Mapolisi wetu asilimia kubwa ni form four failure!! Kuna ofisa mmoja nimesoma naye alipata four ya 32 lakini sasa hivi eti ni OC-CID wilaya fulani hivi!
Dah we upo mbali sana kumbe. Utandawazi wote huu bado unajisemesha kwamba flan alipata 4 ya 32 mwaka 1998...vip kama alirud tena shulen baada ya kupata kazi arifu
 
Umenena kweli tupu, ndio Msingi WA thread yangu. Ni hatari Sana Sana. Kesho na keshokutwa tutamlaunu Nani??
Hautakuwa na wa kumlaumu sabab mi na wew wote hatutakwepo tutakuwa tumeshakufa mda mrefu tu. Generation ya kuweza kufanya ayo ya kesho na kesho kutwa kibongo bongo bado haijazaliwa..hata atakaekuwa kitukuu chako bado generation yao haitakuwa na uthubutu huo. Over
 
Hizo jumuiya za kimataifa hata zikiangalia hazina msaada kwenu mkithubutu kuingia barabarani. Wengi wao ni majizi tu na safari hii kichaa kapewa lungu.
SABABU ZA KUWACHAPA TUNAZO
NIA YA KUWACHAPA TUNAYO
UWEZO WA KUWACHAPA TUNAO
TUTAWACHAPA MJE BARABARANI MUONE
You are one of the good reasons why this country will always be third world country forever.

Poor tanzanians
 
Polisi wanastahili pongezi kwa namna walivyotembeza mkwara.
 
Mazoezi yanafanyika popote pale na huwezi kuwakadiria kwa kuona tu vile wanavyokimbia mchaka mchaka na kuimba. Eti mwenye nia ovu akiona yale mazoez yao atajua udhaif wao..nani kakudanganya. Kuna kitu kinaitwa "ambush" hii kitu ata uwe umetoka SWAT ukitegewa vizuri lazima ukalishwe..usikariri eti jana umeona polisi wamekaa sita kweny gari ukajidanganya ni simpo kuvamiwa. Na usiseme tu kwa miili ile wananch wakilianzisha hakuna wa kupona je umeangalia pande zote au ni kwa askari peke yao...tambua kabisa kwenye vurugu yoyote wakifa askari watano basi kwa raia itakuwa double. Gari lolote la polisi halitembei bila silaha, huwezi kundi kubla la askari km hao alafu kusiwe na silaha impossible, mzungu alirahisisha sana usipige askari na ngumi au jiwe ukategemea naye atakurushia jiwe pia. Sana sana utakuwa umempa sabab ya kukumwaga utumbo nje. Ova
 
Hata polisi pia wanakatwa kodi mkuu

Sawa mkubwa. Sijui wanalipa kiasi gani ila ni ujinga kukata tawi la mti ulilolikalia.

Hata hivyo siwezi kuwalaumu sana. Wanaishi maisha ya shida na taabu mno, nafikiri wameathirika kisaikolojia. Angalia kuanzia makazi yao na maisha yao kwa ujumla utanielewa nnachomaanisha.
 
Pesa Zetu Watuibie,Kuandamana Ni Haki Yetu Kwa Mujibu Wa Katiba,Pia Hawataki! I Do Believe Ssa Yale Maneno Aliyoyasema DONARD TRUMP.Ni Ukweli Usio Na Chenga Yeyote.
Wametishiwa kuandamana, wakaandamana wao... Reverse psychology
 
Sasa unadhani kufeli mtihani wa kidato cha nne ndo hawezi kila kitu we bwege veterani !!
Matendo yao yanadhihirisha hilo!! Au na wewe ni kapolisi uchwara nini?
 
Back
Top Bottom